< Mambo ya Walawi 21 >
1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
Gospod je rekel Mojzesu: »Govori duhovnikom, Aronovim sinovom in jim reci: ›Nihče naj ne bo omadeževan zaradi mrtvega med svojim ljudstvom,
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
toda za njegove sorodnike, ki so blizu njemu, to je za njegovo mater, za njegovega očeta, za njegovega sina, za njegovo hčer, za njegovega brata
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
in za njegovo sestro devico, ki je blizu njemu, ki nima nobenega soproga; zaradi nje je lahko omadeževan.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
Toda ta, ki je poglavar med svojim ljudstvom, sebe ne bo omadeževal, da se oskruni.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
Ne bodo delali pleše na svoji glavi, niti ne bodo brili robov svojih brad, niti si ne bodo delali nobenih urezov na mesu.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
Sveti bodo svojemu Bogu in ne bodo oskrunili imena svojega Boga, kajti darujejo Gospodove daritve, narejene z ognjem in kruh njihovega Boga; zato bodo sveti.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
Naj ne vzamejo žene, ki je vlačuga ali oskrunjena niti naj ne vzamejo žene, odslovljene od njenega soproga, kajti on je svet svojemu Bogu.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
Zato ga boš torej posvetil, kajti on daruje kruh tvojega Boga. Tebi bo svet, kajti jaz, Gospod, ki te posvečujem, sem svet.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
Če pa se hči kateregakoli duhovnika oskruni z igranjem vlačuge, je oskrunila svojega očeta. Sežgana naj bo z ognjem.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
Kdor je véliki duhovnik med svojimi brati, na katerega glavo je bilo izlito mazilno olje in ki je uméščen, da si nadene obleke, ne bo odkril svoje glave niti pretrgal svojih oblačil,
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
niti ne bo šel h kateremukoli truplu niti se ne bo omadeževal zaradi svojega očeta ali zaradi svoje matere,
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
niti naj ne gre ven iz svetišča niti ne oskruni svetišča svojega Boga, kajti krona mazilnega olja njegovega Boga je na njem. Jaz sem Gospod.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
Ženo bo vzel v njenem devištvu.
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
Vdove ali ločene ženske ali oskrunjene ali pocestnice; teh ne bo vzel, temveč bo za ženo vzel devico iz svojega lastnega ljudstva.
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
Niti med svojim ljudstvom ne bo oskrunil svojega semena, kajti jaz, Gospod, ga posvečujem.‹«
16 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
»Govori Aronu, rekoč: ›Kdorkoli je od tvojega semena v njihovih rodovih, ki ima kakršnokoli pomanjkljivost, naj se ne približa, da bi daroval kruh svojega Boga.
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
Kajti katerikoli človek je, ki ima pomanjkljivost, se ne bo približal. Slep človek ali hrom ali kdor ima ploščat nos ali katerokoli stvar odveč
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
ali človek, ki ima zlomljeno nogo ali zlomljeno roko
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
ali je grbast ali pritlikav ali, ki ima pomanjkljivost v svojem očesu ali je grintav ali krastav ali ima zmečkana moda;
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
noben človek, ki ima iz semena duhovnika Arona pomanjkljivost, ne bo prišel blizu, da daruje Gospodove daritve narejene z ognjem. Ima pomanjkljivost; ta ne bo prišel blizu, da daruje kruh svojega Boga.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
Jedel bo kruh svojega Boga, tako od najsvetejšega kakor od svetega.
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
Samo ta ne bo šel noter za zagrinjalo niti prišel blizu k oltarju, ker ima pomanjkljivost, da ne oskruni mojih svetišč, kajti jaz, Gospod, jih posvečujem.‹«
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
Mojzes je to povedal Aronu, njegovim sinovom in vsem Izraelovim otrokom.