< Mambo ya Walawi 21 >
1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
Rzekł też Pan do Mojżesza: Mów do kapłanów, synów Aaronowych, a powiedz im: Niech się nad umarłym nie plugawi żaden kapłan w ludu swym;
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
Tylko przy pokrewnym swoim, powinowatym swoim, przy matce swej, i przy ojcu swym, i przy synu swym, i przy córce swej, i przy bracie swym;
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
Także przy siostrze swej, pannie sobie najbliższej, która nie miała męża; przy tych splugawić się może.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
Nie splugawi się przy przełożonym ludu swego, tak żeby się zmazał.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
Nie będą sobie czynić łysiny na głowie swej, i brody swej nie mają golić, ani na ciele swem czynić będą rzezania.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
Świętymi będą Bogu swemu, i nie splugawią imienia Boga swego; albowiem ofiary ogniste Pańskie, chleb Boga swego, ofiarują; przetoż będą świętymi.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
Niewiasty wszetecznej, i w panieństwie naruszonej, pojmować nie będą; także niewiasty odrzuconej od męża jej, pojmować nie będą; bo święty jest każdy z nich Bogu swemu.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
A tak będziesz go miał za świętego, bo chleb Boga twego ofiaruje; przetoż świętym będzie tobie, bom Ja święty Pan, który poświęcam was.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
Jeźliby się córka kapłańska nierządu dopuściła, ojca swego zelżyła, ogniem spalona będzie.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
Najwyższy też kapłan między bracią swą, na którego głowę wylany jest olejek pomazania, i który poświęcił ręce swe, aby obłoczył szaty święte, głowy swej nie obnaży i szat swoich nie rozedrze;
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
I do żadnego z umarłych nie przystąpi, a nawet i przy ojcu swym, i przy matce swej plugawić się nie będzie.
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
Z świątnicy też nie wynijdzie, aby nie splugawił świątnicy Boga swego, gdyż korona olejku pomazania Boga jego jest na nim: Jam Pan.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
Tenże pannę w panieństwie jej pojmie.
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
Wdowy, i odrzuconej i splugawionej nierządnicy, żadnej z tych nie pojmie; ale pannę z ludu swego za żonę.
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
A nie będzie plugawił nasienia swego w ludu swym; bom Ja Pan, który go poświęcam.
16 Bwana akamwambia Mose,
Przytem rzekł Pan do Mojżesza, mówiąc:
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
Powiedz Aaronowi, i rzecz: Ktobykolwiek z potomstwa swego w narodziech swych, miał na sobie wadę, niechaj nie przystępuje, aby ofiarował chleb Boga swego;
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
Bo żaden mąż, który by miał na sobie wadę, przystępować nie ma; mąż ślepy, albo chromy, albo niezupełnych albo zbytnich członków;
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
Także mąż, który by miał złamaną nogę, albo złamaną rękę;
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
Także garbaty, i płynących oczu, albo który ma bielmo na oku swem, albo krostawy, albo parszywy, albo wypukły:
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
Wszelki mąż, który by miał jaką wadę, z potomstwa Aarona kapłana nie przystąpi, aby ofiarował ofiary ogniste Panu; wada na nim jest, nie przystąpi, aby ofiarował chleb Boga swego.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
Chleba jednak Boga swego z rzeczy najświętszych i poświęconych pożywać będzie.
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
Wszakże za zasłonę nie wnijdzie, i do ołtarza nie przystąpi, bo wada na nim jest, aby nie splugawił świątnicy mojej; bom Ja Pan, który ją poświęcam.
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
To mówił Mojżesz do Aarona, i do synów jego, i do wszystkich synów Izraelskich.