< Mambo ya Walawi 21 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
خداوند به موسی فرمود: «این دستورها را به کاهنان که از نسل هارون هستند بده. یک کاهن نباید با دست زدن به شخص مرده خودش را نجس کند،
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
مگر اینکه مرده از بستگان نزدیک او باشد، مثل: مادر، پدر، پسر، دختر، برادر
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
یا خواهر باکره‌اش که تحت سرپرستی او بوده است.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
اما کاهن نباید به خاطر افرادی که از بستگانش نیستند، خود را نجس سازد.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
«کاهنان نباید موی سر یا گوشه‌های ریش خود را بتراشند و یا بدن خود را زخمی کنند.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
ایشان باید برای خدای خود مقدّس باشند و به نام خدای خویش بی‌احترامی نکنند. آنها برای خداوند هدایای خوراکی بر آتش تقدیم می‌کنند، پس باید مقدّس باشند.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
کاهن نباید با یک فاحشه که خود را بی‌عصمت کرده و یا با زنی که طلاق گرفته، ازدواج کند؛ چون او برای خدای خویش مقدّس است.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
کاهنان را مقدّس بشمارید زیرا ایشان هدایای خوراکی به من تقدیم می‌کنند، و من که خداوند هستم و شما را تقدیس می‌کنم، مقدّس می‌باشم.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
اگر دختر کاهنی فاحشه شود به تقدس پدرش لطمه می‌زند و باید زنده‌زنده سوزانده شود.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
«کاهن اعظم که با روغن مخصوص، مسح و تقدیس شده و لباسهای مخصوص کاهنی را می‌پوشد، نباید هنگام عزاداری موی سر خود را باز کند یا گریبان لباس خود را چاک بزند.
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
او نباید با نزدیک شدن به هیچ جنازه‌ای خود را نجس سازد، حتی اگر شخص مرده پدر یا مادرش باشد.
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
او نباید با خارج شدن از قدس خدا به جهت وارد شدن به خانه‌ای که جنازه‌ای در آن هست، قدس را بی‌حرمت سازد، زیرا تبرک روغن مسح من که یهوه هستم بر سر اوست.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
او باید فقط با یک باکره ازدواج کند.
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
او نباید با زن بیوه یا طلاق داده شده یا زنی که با فاحشه شدن خود را بی‌عصمت کرده است ازدواج کند، بلکه باید دختر باکره‌ای از قوم خود را به زنی بگیرد،
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
تا باعث بدنامی نسل خود در میان قومش نشود، زیرا من که یهوه هستم او را برای کاهنی تقدیس کرده‌ام.»
16 Bwana akamwambia Mose,
خداوند به موسی فرمود:
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
«این دستورها را به هارون بده. در نسلهای آینده هر کدام از فرزندانت که عضوی از بدنش ناقص باشد نباید هدایای خوراکی را به حضور من تقدیم کند.
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
کسی که نقصی در صورت داشته باشد و یا کور، شل، ناقص الخلقه،
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
دست یا پا شکسته،
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
گوژپشت یا کوتوله باشد، چشم معیوب یا مرض پوستی داشته یا بیضه‌هایش آسیب دیده باشد،
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
به سبب نقص جسمی‌اش اجازه ندارد هدایای خوراکی را که بر آتش به خداوند تقدیم می‌شود، تقدیم کند.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
با وجود این باید از خوراک کاهنان که از هدایای تقدیمی به خداوند است به او غذا داده شود هم از هدایای مقدّس و هم از مقدّسترین هدایا.
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
ولی او نباید به پردهٔ مقدّس خیمۀ ملاقات یا به مذبح نزدیک شود چون نقص بدنی دارد و این عمل او خیمۀ ملاقات مرا بی‌حرمت می‌کند، زیرا من که خداوند هستم آن را تقدیس کرده‌ام.»
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
موسی این دستورها را به هارون و پسرانش و تمامی قوم اسرائیل داد.

< Mambo ya Walawi 21 >