< Mambo ya Walawi 21 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
And the Lord said unto Moses, Speak unto the priests the sons of Aaron, and say unto them, None [of them] shall defile himself on the dead, among his people;
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
But on his kin, that is near unto him, [that is, ] on his mother, and on his father, and on his son, and on his daughter, and on his brother,
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
And on his sister that is a virgin, that is nigh unto him, who hath had no husband: on her may he defile himself.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
The chief man among his people shall not defile himself, to be profaned thereby.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
They shall not make any baldness upon their head, and the corner of their beard shall they not shave off, and in their flesh shall they not make any incision.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
Holy shall they be unto their God, and they shall not profane the name of their God; for the fire-offerings of the Lord, the bread of their God, do they offer, they shall therefore be holy.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
A woman that is a harlot, or one profaned, shall they not take; and a woman put away from her husband shall they not take; for holy is he unto his God.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
And thou shalt sanctify him; for the bread of thy God doth he offer: holy shall he be unto thee; for I the Lord, who sanctify you, am holy.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
And if the daughter of any priest profane herself by committing incest, her father doth she profane: with fire shall she be burnt.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
And the priest that is highest among his brethren, upon whose head the anointing oil hath been poured, and who hath been consecrated to put on the garments, shall not let the hair of his head grow long, and his garments shall he not rend;
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
Neither shall he go in to any dead body; even on his father, and on his mother shall he not defile himself.
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
And out of the sanctuary shall he not go, that he may not profane the sanctuary of his God; for the crown of the anointing oil of his God is upon him: I am the Lord.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
And he shall take a wife in her virgin state.
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
A widow, and a divorced woman, and one profaned, [and] a harlot, these shall he not take; but a virgin of his own people shall he take for wife;
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
So that he may not profane his seed among his people; for I, the Lord, do sanctify him.
16 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke unto Moses, saying,
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
Speak unto Aaron, saying, Whosoever of thy seed in their generations it be on whom there is any blemish, shall not approach to offer the bread of his God.
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
For whatsoever man it be on whom there is a blemish, shall not approach: a blind, or a lame man, or one that hath a flattened nose, or a man one of whose limbs is too long,
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
Or a man who hath a broken foot, or a broken hand,
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
Or a crookbacked, or a dwarf, or one that hath a blemish in his eye, or the itch, or the scurvy, or the testicles broken.
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
Every man on whom there is a blemish, of the seed of Aaron the priest, shall not come nigh to offer the fire-offerings of the Lord: there is a blemish on him; he shall not come nigh to offer the bread of his God.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
The brewed of his God, both of the most holy, and of the holy things he may eat.
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
Only unto the vail, and unto the altar shall he not come nigh, because there is a blemish on him; that he profane not my holy things; for I the Lord do sanctify them.
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
And Moses spoke thus unto Aaron, and to his sons, and unto all the children of Israel.

< Mambo ya Walawi 21 >