< Mambo ya Walawi 21 >

1 Bwana akamwambia Mose, “Sema na makuhani, wana wa Aroni, uwaambie: ‘Kamwe kuhani asijitie unajisi kwa utaratibu wa kiibada kwa ajili ya mtu wake yeyote anayekufa,
Господ рече още на Моисея: Говори на свещениците, Аароновите синове, и кажи им: Никой от вас да се не оскверни между людете си, заради мъртвец,
2 isipokuwa jamaa wake wa karibu, kama vile mama yake au baba yake, mwanawe au binti yake, ndugu yake,
освен за близък сродник, сиреч, за майка си, за баща си, за сина си, за дъщеря си, или за брата си;
3 au dada yake asiyeolewa ambaye anamtegemea kwa kuwa hana mume, kwa ajili ya hao aweza kujitia unajisi.
също и за сестра си девица, която е близка нему, и която не е била омъжена, заради нея може да се оскверни.
4 Kamwe asijitie unajisi mwenyewe kutokana na wale watu ambao anahusiana nao kwa kuoana, na hivyo kujitia unajisi.
Като началник на людете си да се не оскверни така щото да стане мръсен.
5 “‘Kamwe makuhani wasinyoe nywele za vichwa vyao wala wasinyoe pembeni mwa ndevu zao, au kuweka chale kwenye miili yao.
Да не оплешат главата си, нито да бръснат краищата на брадата си, нито да правят порязвания по месата си.
6 Lazima wawe watakatifu kwa Mungu wao, na kamwe wasilinajisi jina la Mungu wao. Kwa sababu ndio wanaotoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana, chakula cha Mungu wao, hivyo lazima wawe watakatifu.
Свети да бъдат на Бога си, и да не осквернят Името на Бога си; защото те принасят Господните чрез огън приноси, хляба на Бога си; затова, да бъдат свети.
7 “‘Kamwe wasioe wanawake waliojinajisi kwa ukahaba, au waliopewa talaka na waume wao, kwa sababu makuhani ni watakatifu kwa Mungu wao.
Да не вземат жена, която е блудница или осквернена, нито да вземат жена напусната от мъжа си; защото свещеникът е свет на Бога си.
8 Waoneni kuwa watakatifu, kwa sababu ndio wanaotoa chakula cha Mungu wenu. Kumbukeni kuwa ni watakatifu, kwa sababu Mimi Bwana ni mtakatifu, Mimi niwafanyaye ninyi kuwa watakatifu.
Прочее, да го накараш да бъде свет, защото той принася хляба на твоя Бог; свет да ти бъде; защото Аз Господ, Който ви освещавам, съм свет.
9 “‘Ikiwa binti wa kuhani anajitia unajisi kwa kufanya ukahaba, anamwaibisha baba yake; lazima achomwe kwa moto.
И ако дъщерята на някой свещеник се омърси с блудство, тя омърсява баща си; с огън да се изгори.
10 “‘Kuhani mkuu, yule miongoni mwa ndugu zake ambaye amekwisha kutiwa mafuta kwa kumiminiwa juu ya kichwa chake, na ambaye amewekwa wakfu kuvaa mavazi ya ukuhani, kamwe asiache nywele zake bila kufunikwa, wala asirarue nguo zake.
Но оня, който между братята си е велик свещеник, на чиято глава се е изляло мирото за помазване, и който се е посветил, за да облича свещените одежди, да не ткрива главата си, нито да раздира дрехите си,
11 Kamwe asiingie mahali palipo maiti ndani. Kamwe asijitie unajisi, hata kwa ajili ya baba yake au mama yake,
нито да влиза при някой умрял, нито да се осквернява за баща си или за майка си;
12 wala asiondoke mahali patakatifu pa Mungu wake au kupanajisi, kwa sababu amewekwa wakfu kwa mafuta ya Mungu wake. Mimi ndimi Bwana.
нито да излиза от светилището или да осквернява светилището на Бога си; защото посвещаването чрез помазване с мирото на Бога му е станало на него. Аз съм Господ.
13 “‘Mwanamke kuhani atakayemwoa lazima awe bikira.
И той да вземе за жена девица;
14 Kamwe asimwoe mjane, au mwanamke aliyepewa talaka, wala mwanamke aliyejinajisi kwa ukahaba, bali atamwoa tu bikira kutoka miongoni mwa watu wake,
вдовица, или напусната, или осквернена, или блудница да не взема; но девица от людете си да вземе за жена.
15 na hivyo hatawatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake. Mimi ndimi Bwana, nimfanyaye mtakatifu.’”
И тъй, да не осквернява потомството си между людете си; защото Аз съм Господ, Който го освещавам.
16 Bwana akamwambia Mose,
Господ говори още на Моисея, казвайки:
17 “Mwambie Aroni: ‘Kwa vizazi vijavyo, hakuna mzao wako mwenye dosari atakayekaribia kutoa chakula cha Mungu wake.
Говори на Аарона, като му речеш: Който от твоето потомство, във всичките им поколения, има недостатък, той да не пристъпва да принася хляб на Бога си.
18 Hakuna mtu mwenye dosari yoyote awezaye kukaribia: hakuna mtu aliye kipofu au kiwete, au aliyeharibika uso au asiye na viungo kamili,
Защото никой, който има недостатък, не бива да пристъпва: човек сляп, или куц, или със сплескан нос, или с нещо излишно,
19 hakuna mtu mwenye mguu au mkono uliolemaa,
или човек със строшена нога, или строшена ръка,
20 au mwenye kibiongo au aliyedumaa, au aliye na tatizo la macho, au aliye na uvimbe wenye usaha au majipu, au aliyehasiwa.
или гърбав, или завързляк, или с повредени очи, или със суха краста, или с лишаи, или килав.
21 Hakuna mzao wa kuhani Aroni mwenye kilema chochote atakayekaribia kutoa sadaka kwa Bwana ya kuteketezwa kwa moto. Kama ana kilema, kamwe asikaribie kutoa chakula cha Mungu wake.
Ни един човек от потомството на свещеника Аарона, който има недостатък, да не пристъпва за да принесе Господните чрез огън приноси; понеже има недостатък, ни бива да пристъпи да принесе хляба на Бога си.
22 Anaweza kula chakula kitakatifu sana cha Mungu wake, pia hata chakula kitakatifu.
От пресветите и от светите приноси нека яде хляба на Бога си;
23 Lakini kwa sababu ya kilema chake, kamwe asikaribie karibu na pazia wala kukaribia madhabahu, asije akanajisi mahali patakatifu pangu. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye watakatifu.’”
но да не влиза до завесата нито да се приближава при олтара, понеже има недостатък, за да не омърсява светилищата Ми; защото Аз съм Господ, Който ги освещавам.
24 Basi Mose akamwambia Aroni jambo hili na wanawe, pamoja na Waisraeli wote.
И тъй, Моисей каза това на Аарона и на синовете му, и на всичките израилтяни.

< Mambo ya Walawi 21 >