< Mambo ya Walawi 20 >

1 Bwana akamwambia Mose,
Gospod je spregovoril Mojzesu, rekoč:
2 “Sema na wana wa Israeli: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi katika Israeli ambaye atamtoa yeyote miongoni mwa watoto wake kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mtu huyo lazima auawe. Watu wa jumuiya hiyo watampiga kwa mawe.
»Ponovno, Izraelovim otrokom boš rekel: ›Kdorkoli je izmed Izraelovih otrok ali izmed tujcev, ki začasno prebivajo v Izraelu, da izroči karkoli od svojega semena Molohu; ta bo zagotovo usmrčen. Ljudstvo dežele naj ga kamna s kamni.
3 Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa maana kwa kumtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, amenajisi madhabahu yangu na kulinajisi Jina langu takatifu.
Svoj obraz bom naravnal zoper tega človeka in ga iztrebil izmed njegovega ljudstva, ker je od svojega semena dal Molohu, da omadežuje moje svetišče in da oskruni moje sveto ime.
4 Ikiwa watu wa jumuiya watafumba macho wakati mtu huyo anapomtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, nao wakaacha kumuua,
Če ljudstvo dežele kakorkoli skrije svoje oči pred možem, ko ta daje svoje seme Molohu in ga ne ubije,
5 mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo pamoja na jamaa yake, nami nitawakatilia mbali yeye na watu wote waliofanya ukahaba na Moleki.
potem bom svoj obraz naravnal zoper tega moža in zoper njegovo družino in izmed njegovega ljudstva odsekal njega in vse, ki se gredo vlačugat za njim, da bi zagrešili vlačugarstvo z Molohom.
6 “‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
Duša, ki se obrača za takšnimi, ki imajo osebne duhove in za čarovniki, da se gredo vlačugat za njimi, zoper to dušo celo naravnam svoj obraz in ga bom odsekal izmed njegovega ljudstva.
7 “‘Jitakaseni basi, nanyi kuweni watakatifu, kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
Posvečujte se torej in bodite sveti, kajti jaz sem Gospod, vaš Bog.
8 Shikeni amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.
Držali se boste mojih zakonov in jih izvrševali. Jaz sem Gospod, ki vas posvečujem.
9 “‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani baba yake au mama yake, lazima auawe. Amemlaani baba yake au mama yake, nayo damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
Kajti vsak, kdor preklinja svojega očeta ali svojo mater, bo zagotovo usmrčen. Preklinjal je svojega očeta ali svojo mater; njegova kri bo nad njim.
10 “‘Ikiwa mtu atazini na mke wa mtu mwingine, yaani mke wa jirani yake, wazinzi hao wawili lazima wauawe.
Moški, ki zagreši zakonolomstvo z ženo drugega moškega, torej ta, ki zagreši zakonolomstvo z ženo svojega bližnjega, zakonolomec in zakonolomka bosta zagotovo usmrčena.
11 “‘Kama mtu atakutana kimwili na mke wa baba yake, hakumheshimu baba yake. Mwanaume huyo na mwanamke huyo wote wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
Moški, ki leži z ženo svojega očeta, je odkril očetovo nagoto. Oba bosta zagotovo usmrčena. Njuna kri bo nad njima.
12 “‘Ikiwa mtu atakutana kimwili na mke wa mwanawe, lazima wote wawili wauawe. Walichokifanya ni upotovu; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
Če moški leži s svojo snaho, bosta zagotovo oba usmrčena. Storila sta zmešnjavo. Njuna kri naj bo nad njima.
13 “‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mwanaume mwenzake kama vile mwanaume afanyavyo na mwanamke, wanaume hao wawili wamefanya lililo chukizo sana. Lazima wauawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
Če moški leži z moškim prav tako, kakor leži z žensko, sta oba zagrešila ogabnost. Zagotovo bosta oba usmrčena. Njuna kri bo nad njima.
14 “‘Ikiwa mwanaume ataoa binti pamoja na mama yake, huo ni uovu. Wote watatu ni lazima wachomwe moto, ili kwamba pasiwepo na uovu katikati yenu.
Če moški vzame ženo in njeno mater, je to zlo. Sežgani bodo z ognjem, tako on in oni dve, da tam med vami ne bo zla.
15 “‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mnyama, ni lazima auawe, na pia ni lazima mnyama huyo auawe.
Če moški leži z živaljo, bo zagotovo usmrčen, žival pa boste zaklali.
16 “‘Kama mwanamke atamsogelea mnyama kukutana naye kimwili, muueni mwanamke huyo pamoja na mnyama pia. Lazima wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
Če se ženska približa h katerikoli živali in leže dol k njej, boš ubil žensko in žival. Obe bosta zagotovo usmrčeni. Njuna kri bo nad njima.
17 “‘Ikiwa mtu anamwoa dada yake, binti aliyezaliwa na baba yake au mama yake, nao wakakutana kimwili, ni aibu. Lazima wakatiliwe mbali machoni pa watu wao. Huyo mwanaume amemwaibisha dada yake, hivyo atawajibika kwa ajili ya uovu huo.
Če moški vzame svojo sestro, hčer svojega očeta ali hčer svoje matere in vidi njeno nagoto in ona vidi njegovo nagoto. To je zlobna stvar in oba bosta iztrebljena pred očmi svojega ljudstva. Odkril je nagoto svoje sestre. Nosil bo svojo krivičnost.
18 “‘Ikiwa mwanaume atalala na mwanamke aliye katika hedhi yake na kukutana naye kimwili, amefunua mtiririko wa hedhi yake, naye huyo mwanamke amejifunua uchi wake. Wote wawili lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
Če bo moški ležal z žensko, ki je bolna in bo odkril njeno nagoto, je odkril njen studenec in ona je odkrila studenec svoje krvi in oba izmed njiju bosta iztrebljena izmed svojega ljudstva.
19 “‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako wala wa baba yako, kwa maana hilo litamwaibisha jamaa wa karibu; ninyi wawili mtawajibika kwa ajili ya uovu huo.
Ne boš odkril nagote sestre svoje matere niti sestre svojega očeta, kajti on odkriva svoje bližnje sorodstvo. Oba bosta nosila svojo krivičnost.
20 “‘Ikiwa mwanaume atakutana kimwili na shangazi yake, amemwaibisha mjomba wake. Nao watawajibika kwa ajili ya uovu huo; watakufa bila kuzaa mtoto.
Če bo moški ležal z ženo svojega strica, odkriva nagoto svojega strica. Nosila bosta svoj greh; umrla bosta brez otrok.
21 “‘Ikiwa mwanaume ataoa mke wa ndugu yake, hili ni tendo chafu; amemwaibisha ndugu yake. Nao hawatazaa mtoto.
Če bo moški vzel ženo svojega brata, je to nečista stvar. Odkril je nagoto svojega brata; onadva bosta brez otrok.
22 “‘Zishikeni amri na sheria zangu zote na kuzifuata, ili nchi ninayowaleta kuishi isiwatapike.
Vi se boste torej držali vseh mojih zakonov in vseh mojih sodb in jih izvrševali, da vas dežela, kamor vas privedem, da v njej prebivate, ne izpljune.
23 Kamwe msiishi kwa kufuata desturi za mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu. Kwa sababu walifanya mambo haya yote, nami nikachukizwa sana nao.
Ne boste hodili po običajih naroda, ki sem ga pred vami izgnal, kajti zagrešili so vse te stvari in zato so se mi zagnusili.
24 Lakini niliwaambia ninyi, “Mtaimiliki nchi yao; nitawapa ninyi kuwa urithi, nchi inayotiririka maziwa na asali.” Mimi ndimi Bwana Mungu wenu, ambaye amewatenga kutoka mataifa.
Toda vam sem rekel: ›Podedovali boste njihovo deželo in dal vam jo bom, da jo vzamete v last, deželo kjer tečeta mleko in med.‹ Jaz sem Gospod, vaš Bog, ki vas je oddvojil od drugih ljudstev.
25 “‘Kwa hiyo, ninyi lazima mweze kutofautisha kati ya wanyama walio safi na wasio safi, pia kati ya ndege wasio safi na walio safi. Msijitie unajisi kutokana na mnyama yeyote, au ndege, wala kitu chochote kitambaacho juu ya ardhi, vile ambavyo nimevitenga kuwa najisi kwa ajili yenu.
Zato boste postavili razliko med čistimi živalmi in nečistimi in med nečisto perjadjo in čisto, in svojih duš ne boste ognusili z živalmi ali s perjadjo ali s katerokoli vrsto žive stvari, ki se plazi po tleh, ki sem jo kot nečisto oddvojil od vas.
26 Mtakuwa watakatifu kwangu, kwa sababu Mimi, Bwana, ni mtakatifu, nami nimewatenga kutoka mataifa kuwa wangu mwenyewe.
Vi mi boste sveti, kajti jaz, Gospod, sem svet in sem vas oddvojil od drugih ljudstev, da bi bili moji.
27 “‘Mwanaume au mwanamke ambaye ni mchawi, mwaguzi au mwenye kupunga pepo miongoni mwenu lazima auawe. Mtawapiga kwa mawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.’”
Moški ali ženska, ki ima osebnega duha ali da je čarovnik, bosta zagotovo usmrčena. Kamnajo naj ju s kamni. Njuna kri bo nad njima.‹«

< Mambo ya Walawi 20 >