< Mambo ya Walawi 20 >
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 “Sema na wana wa Israeli: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi katika Israeli ambaye atamtoa yeyote miongoni mwa watoto wake kuwa sadaka kwa mungu Moleki, mtu huyo lazima auawe. Watu wa jumuiya hiyo watampiga kwa mawe.
And to [the] people of Israel you will say a person a person from [the] people of Israel and of the sojourner[s] - who sojourns in Israel who he will give any of offspring his to Molech certainly he will be put to death [the] people of the land they will stone him with stone[s].
3 Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo, nami nitamkatilia mbali na watu wake. Kwa maana kwa kumtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, amenajisi madhabahu yangu na kulinajisi Jina langu takatifu.
And I I will set face my on the person that and I will cut off him from among people his for one of offspring his he has given to Molech so as to make unclean sanctuary my and to profane [the] name of holiness my.
4 Ikiwa watu wa jumuiya watafumba macho wakati mtu huyo anapomtoa mmoja wa watoto wake kwa mungu Moleki, nao wakaacha kumuua,
And if certainly they will hide [the] people of the land eyes their from the person that when gives he one of offspring his to Molech to not to put to death him.
5 mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu huyo pamoja na jamaa yake, nami nitawakatilia mbali yeye na watu wote waliofanya ukahaba na Moleki.
And I will set I face my on the person that and on clan his and I will cut off him and - all those [who] act as prostitutes after him by acting as prostitutes after Molech from among people their.
6 “‘Mimi nitauelekeza uso wangu dhidi ya mtu anayeenda kwa waaguzi na wenye pepo, na hivyo kujifanyia ukahaba kwa kuwafuata, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
And the person who it will turn to the necromancers and to the soothsayers to act as a prostitute after them and I will set face my on the person that and I will cut off him from among people his.
7 “‘Jitakaseni basi, nanyi kuweni watakatifu, kwa sababu mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
And you will keep yourselves holy and you will be holy for I [am] Yahweh God your.
8 Shikeni amri zangu na kuzifuata. Mimi ndimi Bwana, niwafanyaye ninyi watakatifu.
And you will keep statutes my and you will do them I [am] Yahweh [who] sets apart as holy you.
9 “‘Ikiwa mtu yeyote atamlaani baba yake au mama yake, lazima auawe. Amemlaani baba yake au mama yake, nayo damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe.
If a person a person who he will curse father his and mother his certainly he will be put to death father his and mother his he has cursed blood his [are] on him.
10 “‘Ikiwa mtu atazini na mke wa mtu mwingine, yaani mke wa jirani yake, wazinzi hao wawili lazima wauawe.
And a man who he will commit adultery a wife of a man who he will commit adultery [the] wife of neighbor his certainly he will be put to death the adulterer and the adulteress.
11 “‘Kama mtu atakutana kimwili na mke wa baba yake, hakumheshimu baba yake. Mwanaume huyo na mwanamke huyo wote wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
And a man who he will lie with [the] wife of father his [the] nakedness of father his he has uncovered certainly they will be put to death both of them blood their [are] on them.
12 “‘Ikiwa mtu atakutana kimwili na mke wa mwanawe, lazima wote wawili wauawe. Walichokifanya ni upotovu; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
And a man who he will lie with daughter-in-law his certainly they will be put to death both of them confusion they have done blood their [are] on them.
13 “‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mwanaume mwenzake kama vile mwanaume afanyavyo na mwanamke, wanaume hao wawili wamefanya lililo chukizo sana. Lazima wauawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
And a man who he will lie with a male [the] lyings of a woman an abomination they have done both of them certainly they will be put to death blood their [are] on them.
14 “‘Ikiwa mwanaume ataoa binti pamoja na mama yake, huo ni uovu. Wote watatu ni lazima wachomwe moto, ili kwamba pasiwepo na uovu katikati yenu.
And a man who he will take a woman and mother her [is] wickedness it with fire people will burn him and them and not it will be wickedness in midst of you.
15 “‘Kama mwanaume akikutana kimwili na mnyama, ni lazima auawe, na pia ni lazima mnyama huyo auawe.
And a man who he will give copulation his in an animal certainly he will be put to death and the animal you will kill.
16 “‘Kama mwanamke atamsogelea mnyama kukutana naye kimwili, muueni mwanamke huyo pamoja na mnyama pia. Lazima wauawe; damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.
And a woman who she will draw near to any animal to stretch out with with it and you will kill the woman and the animal certainly they will be put to death blood their [are] on them.
17 “‘Ikiwa mtu anamwoa dada yake, binti aliyezaliwa na baba yake au mama yake, nao wakakutana kimwili, ni aibu. Lazima wakatiliwe mbali machoni pa watu wao. Huyo mwanaume amemwaibisha dada yake, hivyo atawajibika kwa ajili ya uovu huo.
And a man who he will take sister his [the] daughter of father his or [the] daughter of mother his and he will see nakedness her and she she will see nakedness his [is] a shame it and they will be cut off to [the] eyes of [the] sons of people their [the] nakedness of sister his he has uncovered iniquity his he will bear.
18 “‘Ikiwa mwanaume atalala na mwanamke aliye katika hedhi yake na kukutana naye kimwili, amefunua mtiririko wa hedhi yake, naye huyo mwanamke amejifunua uchi wake. Wote wawili lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
And a man who he will lie with a woman menstruating and he will uncover nakedness her spring her he has made naked and she she has uncovered [the] spring of blood her and they will be cut off both of them from among people their.
19 “‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako wala wa baba yako, kwa maana hilo litamwaibisha jamaa wa karibu; ninyi wawili mtawajibika kwa ajili ya uovu huo.
And [the] nakedness of [the] sister of mother your and [the] sister of father your not you will uncover for relative his he has made naked iniquity their they will bear.
20 “‘Ikiwa mwanaume atakutana kimwili na shangazi yake, amemwaibisha mjomba wake. Nao watawajibika kwa ajili ya uovu huo; watakufa bila kuzaa mtoto.
And a man who he will lie with aunt his [the] nakedness of uncle his he has uncovered sin their they will bear childless they will die.
21 “‘Ikiwa mwanaume ataoa mke wa ndugu yake, hili ni tendo chafu; amemwaibisha ndugu yake. Nao hawatazaa mtoto.
And a man who he will take [the] wife of brother his [is] impurity it [the] nakedness of brother his he has uncovered childless they will be.
22 “‘Zishikeni amri na sheria zangu zote na kuzifuata, ili nchi ninayowaleta kuishi isiwatapike.
And you will keep all statutes my and all judgments my and you will do them and not it will vomit up you the land where I [am] about to bring you there towards to dwell in it.
23 Kamwe msiishi kwa kufuata desturi za mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu. Kwa sababu walifanya mambo haya yote, nami nikachukizwa sana nao.
And not you will walk in [the] statutes of the nation which I [am] about to send away from before you for all these [things] they have done and I loathed them.
24 Lakini niliwaambia ninyi, “Mtaimiliki nchi yao; nitawapa ninyi kuwa urithi, nchi inayotiririka maziwa na asali.” Mimi ndimi Bwana Mungu wenu, ambaye amewatenga kutoka mataifa.
And I have said to you you you will take possession of ground their and I I will give it to you to take possession of it a land flowing of milk and honey I [am] Yahweh God your who I have separated you from the peoples.
25 “‘Kwa hiyo, ninyi lazima mweze kutofautisha kati ya wanyama walio safi na wasio safi, pia kati ya ndege wasio safi na walio safi. Msijitie unajisi kutokana na mnyama yeyote, au ndege, wala kitu chochote kitambaacho juu ya ardhi, vile ambavyo nimevitenga kuwa najisi kwa ajili yenu.
And you will separate between the animal[s] pure and unclean and between the bird[s] unclean and pure and not you will make detestable selves your by animal[s] and by bird[s] and by all that it creeps the ground which I have separated for you to declare unclean.
26 Mtakuwa watakatifu kwangu, kwa sababu Mimi, Bwana, ni mtakatifu, nami nimewatenga kutoka mataifa kuwa wangu mwenyewe.
And you will be to me holy for [am] holy I Yahweh and I have separated you from the peoples to belong to me.
27 “‘Mwanaume au mwanamke ambaye ni mchawi, mwaguzi au mwenye kupunga pepo miongoni mwenu lazima auawe. Mtawapiga kwa mawe; nayo damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao wenyewe.’”
And a man or a woman that he will be among them a necromancer or a soothsayer certainly they will be put to death with stone[s] people will stone them blood their [are] on them.