< Mambo ya Walawi 2 >

1 “‘Mtu yeyote aletapo sadaka ya nafaka kwa Bwana, sadaka yake itakuwa ya unga laini. Atamimina mafuta juu yake, aweke uvumba juu yake,
«و هرگاه کسی قربانی هدیه آردی بجهت خداوند بگذراند، پس قربانی او از آرد نرم باشد، و روغن بر آن بریزد و کندر بر آن بنهد.۱
2 naye atapeleka kwa makuhani wana wa Aroni. Kuhani atachukua konzi moja iliyojaa unga laini na mafuta pamoja na uvumba wote, na kuuteketeza kama sehemu ya kumbukumbu juu ya madhabahu, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
وآن را نزد پسران هارون کهنه بیاورد، و یک مشت از آن بگیرد یعنی از آرد نرمش و روغنش باتمامی کندرش و کاهن آن را برای یادگاری بسوزاند، تا هدیه آتشین و عطر خوشبو بجهت خداوند باشد.۲
3 Sadaka ya nafaka iliyobaki ni ya Aroni na wanawe, ni sehemu ya sadaka iliyo takatifu sana iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
و بقیه هدیه آردی از آن هارون وپسرانش باشد. این از هدایای آتشین خداوند قدس اقداس است.۳
4 “‘Kama utaleta sadaka ya nafaka iliyookwa jikoni, itakuwa ya unga laini: maandazi yaliyotengenezwa bila kutiwa chachu, yaliyochanganywa na mafuta, au mikate myembamba iliyotengenezwa bila kutiwa chachu, na iliyopakwa mafuta.
و هرگاه قربانی هدیه آردی پخته شده‌ای در تنور بگذرانی، پس قرصهای فطیر از آرد نرم سرشته شده به روغن، یا گرده های فطیر مالیده شده به روغن باشد.۴
5 Iwapo sadaka yako ya nafaka imeandaliwa kwenye kikaango, itakuwa ni ya unga laini uliochanganywa na mafuta, bila chachu.
و اگر قربانی توهدیه آردی بر ساج باشد، پس از آرد نرم فطیرسرشته شده به روغن باشد.۵
6 Ukande na kumimina mafuta juu yake; hii ni sadaka ya nafaka.
و آن را پاره پاره کرده، روغن بر آن بریز. این هدیه آردی است.۶
7 Kama sadaka yako ya nafaka imepikwa kwenye sufuria, itatengenezwa kwa unga laini na mafuta.
واگر قربانی تو هدیه آردی تابه باشد از آرد نرم باروغن ساخته شود.۷
8 Ilete hiyo sadaka ya nafaka iliyotengenezwa kwa vitu hivi kwa Bwana; mkabidhi kuhani ambaye ataipeleka madhabahuni.
و هدیه آردی را که از این چیزها ساخته شود نزد خداوند بیاور، و آن راپیش کاهن بگذار، و او آن را نزد مذبح خواهدآورد.۸
9 Naye atatoa ile sehemu ya kumbukumbu kutoka kwenye hiyo sadaka ya nafaka na kuiteketeza juu ya madhabahu kuwa sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
و کاهن از هدیه آردی یادگاری آن رابردارد و بر مذبح بسوزاند. این هدیه آتشین و عطرخوشبو بجهت خداوند است.۹
10 Sadaka ya nafaka iliyobaki ni ya Aroni na wanawe; ni sehemu ya sadaka iliyo takatifu sana ya sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
و بقیه هدیه آردی از آن هارون و پسرانش باشد. این ازهدایای آتشین خداوند قدس اقداس است.۱۰
11 “‘Kila sadaka ya nafaka unayoleta kwa Bwana ni lazima ifanywe bila kutiwa chachu, kwa kuwa huna ruhusa kuchoma chachu yoyote au asali katika sadaka itolewayo kwa Bwana kwa moto.
«و هیچ هدیه آردی که بجهت خداوندمی گذرانید با خمیرمایه ساخته نشود، زیرا که هیچ خمیرمایه و عسل را برای هدیه آتشین بجهت خداوند نباید سوزانید.۱۱
12 Unaweza kuzileta kwa Bwana kama sadaka ya malimbuko, lakini haziwezi kutolewa juu ya madhabahu kama harufu nzuri ya kupendeza.
آنها را برای قربانی نوبرها بجهت خداوند بگذرانید، لیکن برای عطر خوشبو به مذبح برنیارند.۱۲
13 Koleza sadaka zako zote za nafaka kwa chumvi. Usiache kuweka chumvi ya Agano la Mungu wako katika sadaka zako za nafaka; weka chumvi kwenye sadaka zako zote.
و هرقربانی هدیه آردی خود را به نمک نمکین کن، ونمک عهد خدای خود را از هدیه آردی خودبازمدار، با هر قربانی خود نمک بگذران.۱۳
14 “‘Kama ukileta malimbuko ya sadaka ya nafaka kwa Bwana, utatoa masuke yaliyopondwa ya nafaka mpya iliyookwa kwa moto.
و اگرهدیه آردی نوبرها بجهت خداوند بگذرانی، پس خوشه های برشته شده به آتش، یعنی بلغورحاصل نیکو بجهت هدیه آردی نوبرهای خودبگذران.۱۴
15 Weka mafuta na uvumba juu yake; ni sadaka ya nafaka.
و روغن بر آن بریز و کندر بر آن بنه. این هدیه آردی است.۱۵
16 Kuhani atateketeza ile sehemu ya kumbukumbu kutoka kwenye hiyo sadaka ya nafaka iliyopondwa kwa mafuta, pamoja na uvumba wote, kama sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
و کاهن یادگاری آن رایعنی قدری از بلغور آن و از روغنش با تمامی کندرش بسوزاند. این هدیه آتشین بجهت خداوند است.۱۶

< Mambo ya Walawi 2 >