< Mambo ya Walawi 18 >
El Señor le dijo a Moisés:
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
“Dile a los israelitas: Yo soy el Señor tu Dios.
3 Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao.
No sigas los caminos de Egipto, donde vivías, y no sigas los caminos de Canaán, donde te llevaré. No adoptes sus prácticas.
4 Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
Haz lo que te digo y guarda mis reglas. Yo soy el Señor tu Dios.
5 Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.
Si guardas mis reglas y haces lo que te digo, vivirás. Yo soy el Señor.
6 “‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.
“No tengas relaciones sexuales con un pariente cercano.
7 “‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
No avergüences a tu padre teniendo sexo con tu madre. Ella es tu madre; no tengas sexo con ella.
8 “‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.
No tengas sexo con ninguna de las esposas de tu padre y avergüenza a tu padre.
9 “‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
No tengas sexo con tu hermana, si es hija de tu padre o de tu madre, o si nació en la misma casa que tú o en otro lugar.
10 “‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.
No tengas sexo con tu nieta, la hija de tu hijo o la hija de tu hija, porque eso sería algo vergonzoso para ti.
11 “‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.
No tengas sexo con la hija de ninguna de las esposas de tu padre y tu padre, ella es tu hermana.
12 “‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.
No tengas sexo con la hermana de tu padre. Ella es un pariente cercano de tu padre.
13 “‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
No tengas relaciones sexuales con la hermana de tu madre. Ella es un pariente cercano de tu madre.
14 “‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.
No avergüences a tu tío teniendo sexo con su esposa. Ella es tu tía.
15 “‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
No tengas sexo con tu nuera. Ella es la esposa de tu hijo. No tengas sexo con ella.
16 “‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.
No te acuestes con la esposa de tu hermano y avergüénzate de él.
17 “‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.
No tengas sexo con una mujer y su hija. No tengas sexo con la hija de su hijo o la hija de su hija. Son sus parientes cercanos. Eso es algo que detesto.
18 “‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
No te cases con la hermana de tu esposa y tengas sexo con ella mientras tu esposa esté viva. Serán esposas hostiles entre sí.
19 “‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.
No tengas sexo con una mujer durante el tiempo que esté sucia debido a su período.
20 “‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.
No cometas ningún acto sexual con la esposa de otro hombre. Esto te contaminaría y te haría sucio.
21 “‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.
“No le des ninguno de tus hijos como sacrificio humano a Moloc, porque no debes deshonrar el carácter de tu Dios. Yo soy el Señor.
22 “‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.
“No tengas sexo con un hombre como con una mujer. Eso es algo asqueroso.
23 “‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.
No tengas sexo con ningún animal. Esto te contaminaría y te ensuciaría.
24 “‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi.
Una mujer no debe entregarse a un animal para tener sexo con él. Eso es algo asqueroso. No se contaminen y se ensucien haciendo algo así. Esa es la razón por la que estoy expulsando a estas naciones de la tierra, se han contaminado a sí mismos por todas estas prácticas.
25 Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake.
Incluso la tierra se ha contaminado, así que la estoy castigando por los pecados cometidos por la gente que vive allí, y la tierra los vomitará.
26 Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya,
“Peroustedes deben hacer lo que yo os diga y guardar mis reglas. No deben hacer ninguno de estos actos repugnantes, ya sea un israelita o un extranjero que viva entre ustedes.
27 kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi.
Las personas que vivían en la tierra antes de ti practicaban todas estas cosas repugnantes, y la tierra se contaminó.
28 Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.
Si contaminas la tierra, te vomitará como lo hizo con las naciones anteriores a ti.
29 “‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
“Por consiguiente, cualquiera que haga cualquiera de estas cosas repugnantes debe ser expulsado de su pueblo.
30 Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’”
Debes aceptar mi demanda de que no sigas ninguna de estas prácticas repugnantes hechas antes de tu llegada. No se contaminen ni se hagan impuros. Yo soy el Señor su Dios”.