< Mambo ya Walawi 18 >
2 “Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
“Tell the Israelites: I am the Lord your God.
3 Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao.
Don't follow the ways of Egypt where you used to live, and don't follow the ways of Canaan where I'm going to take you. Don't adopt their practices.
4 Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu.
Do what I tell you and keep my rules. I am the Lord your God.
5 Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.
If you keep my rules and do what I tell you, you will live. I am the Lord.
6 “‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.
Don't have sex with a close relative.
7 “‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
Don't shame your father by having sex with your mother. She is your mother; don't have sex with her.
8 “‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.
Don't have sex with any of your father's wives and shame your father.
9 “‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.
Don't have sex with your sister, whether she's your father's daughter or your mother's daughter, or whether she was born in the same house as you or somewhere else.
10 “‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.
Don't have sex with your granddaughter, your son's daughter or your daughter's daughter, because that would be shameful thing for you.
11 “‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.
Don't have sex with the daughter of any of your father's wives and your father, she is your sister.
12 “‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.
Don't have sex with your father's sister. She is a close relative of your father.
13 “‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.
Don't have sex with your mother's sister. She is a close relative of your mother.
14 “‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.
Don't bring shame on your uncle by having sex with his wife. She is your aunt.
15 “‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.
Don't have sex with your daughter-in-law. She is your son's wife. Don't have sex with her.
16 “‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.
Don't have sex with your brother's wife and bring shame on your brother.
17 “‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.
Don't have sex with both a woman and her daughter. Don't have sex with her son's daughter or her daughter's daughter. They are her close relatives. That is something I loathe.
18 “‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.
Don't marry your wife's sister and have sex with her while your wife is still alive. They will be hostile wives to one other.
19 “‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.
Don't have sex with a woman during the time she is unclean because of her period.
20 “‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.
Don't commit any sex act with any other man's wife. This would pollute you and make you unclean.
21 “‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.
Don't give any of your children as a human sacrifice to Molech, for you must not disgrace the character of your God. I am the Lord.
22 “‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.
Don't have sex with a man as with a woman. That is something disgusting.
23 “‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.
Don't have sex with any animal. This would pollute you and make you unclean.
24 “‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi.
A woman must not give herself to an animal to have sex with it. That is something disgusting. Don't pollute yourselves and make yourselves unclean by doing anything like this. That's the reason I'm expelling these nations from the land—they polluted themselves because of all these practices.
25 Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake.
Even the land has become polluted, so I am punishing it for the sins committed by the people who live there, and the land will vomit them out.
26 Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya,
You, however, must do what I tell you and keep my rules. You must not do any of these disgusting acts, whether an Israelite or a foreigner living among you.
27 kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi.
The people who lived in the land before you practiced all these disgusting things, and the land became polluted.
28 Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.
If you pollute the land, it will vomit you out just like it did the nations before you.
29 “‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao.
Consequently anyone who does any of these disgusting things must be expelled from their people.
30 Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’”
You must accept my demand that you don't follow any of these disgusting practices done before you arrived. Don't pollute yourselves and make yourselves unclean. I am the Lord your God.”