< Mambo ya Walawi 17 >

1 Bwana akamwambia Mose,
خداوند به موسی فرمود:
2 “Sema na Aroni na wanawe, pamoja na Waisraeli wote, uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana aliloagiza:
«این دستورها را به هارون و پسرانش و به تمام بنی‌اسرائیل بده. این است آنچه خداوند فرموده است:
3 Mwisraeli yeyote atakayetoa dhabihu ya maksai, mwana-kondoo au mbuzi ndani ya kambi au nje yake,
هر اسرائیلی که گاو یا گوسفند یا بزی را در جایی دیگر غیر از داخل یا خارج اردوگاه ذبح کند،
4 badala ya kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kuileta kama sadaka kwa Bwana mbele ya Maskani ya Bwana, mtu huyo atahesabiwa kuwa na hatia ya kumwaga damu; ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
بجای اینکه آن را کنار در خیمۀ ملاقات بیاورد تا به عنوان هدیه به خداوند تقدیم کند، آن شخص خون ریخته و مجرم است و باید از میان قوم خود منقطع شود.
5 Hii ni ili Waisraeli wamletee Bwana dhabihu wanazozifanya sasa mahali pa wazi mashambani. Ni lazima wazilete kwa makuhani, yaani kwa Bwana, katika ingilio la Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu kama sadaka za amani.
هدف از این قانون این است که قوم اسرائیل دیگر در صحرا قربانی نکنند. قوم باید قربانیهای خود را دم در خیمۀ ملاقات پیش کاهن بیاورند و آنها را به عنوان قربانی سلامتی به خداوند تقدیم کنند.
6 Kuhani atanyunyiza damu kwenye madhabahu ya Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania, na kuyateketeza mafuta ya hiyo dhabihu kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
سپس کاهن خون آنها را بر مذبح خداوند که دم در خیمۀ ملاقات است بپاشد و چربی آنها را همچون عطر خوشبویی که مورد پسند خداوند است بسوزاند.
7 Hawatatoa kamwe dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi ambazo wamekuwa wakijifanyia nazo ukahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwao na kwa ajili ya vizazi vijavyo.’
قوم اسرائیل دیگر نباید در صحرا برای ارواح شریر قربانی کنند و به خداوند خیانت ورزند. این برای شما قانونی است همیشگی که باید نسل اندر نسل بجا آورده شود.
8 “Waambie: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwao atakayetoa sadaka ya kuteketezwa au dhabihu
«پس به آنها بگو: هرگاه یک اسرائیلی یا غریبی که در میان قوم ساکن است قربانی سوختنی یا قربانی‌های دیگر تقدیم کند،
9 bila kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kutoa dhabihu kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
اما آن را در جایی غیر از دم در خیمۀ ملاقات برای خداوند قربانی کند، آن شخص باید از میان قوم منقطع شود.
10 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwao ambaye atakunywa damu yoyote, nitakuwa kinyume cha mtu huyo atakayekunywa damu na kumkatilia mbali na watu wake.
«هر کس خون بخورد، چه اسرائیلی باشد، چه غریبی که در میان شما ساکن است، روی خود را از او برگردانده او را از میان قوم منقطع خواهم کرد،
11 Kwa kuwa uhai wa kiumbe uko ndani ya damu, nami nimewapa hiyo damu ili mfanyie upatanisho kwa ajili yenu wenyewe juu ya madhabahu; damu ndiyo ifanyayo upatanisho kwa ajili ya maisha ya mtu.
زیرا جان هر موجودی در خون اوست و من خون را به شما داده‌ام تا برای کفارهٔ جانهای خود، آن را بر روی مذبح بپاشید. خون است که برای جان کفاره می‌کند.
12 Kwa hiyo, ninawaambia Waisraeli, “Hakuna hata mmoja wenu anayeruhusiwa kunywa damu, wala mgeni anayeishi miongoni mwenu haruhusiwi kunywa damu.”
به همین دلیل است که به قوم اسرائیل حکم می‌کنم که نه خودشان خون بخورند و نه غریبی که در میان ایشان ساکن است.
13 “‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye atamwinda mnyama au ndege anayeruhusiwa kuliwa ni lazima aimwage damu na kuifunika kwa udongo,
هر کس به شکار برود، خواه اسرائیلی باشد خواه غریبی که در میان شماست و حیوان یا پرندهٔ حلال گوشتی را شکار کند، باید خونش را بریزد و روی آن را با خاک بپوشاند،
14 kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake. Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli, “Kamwe msinywe damu ya kiumbe chochote, kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake; yeyote atakayekunywa damu ni lazima akatiliwe mbali.”
زیرا جان هر موجودی در خون اوست. به همین دلیل است که به قوم اسرائیل گفتم که هرگز خون نخورند، زیرا حیات هر موجود زنده‌ای در خون آن است. پس هر کس خون بخورد باید از میان قوم اسرائیل منقطع شود.
15 “‘Mtu yeyote, awe mzawa au mgeni, ambaye atakula mzoga wa kitu chochote ama kilichouawa na wanyama mwitu ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni, kisha atakuwa safi.
«هر اسرائیلی یا غریبی که گوشت حیوان مرده یا دریده شده‌ای را بخورد، باید لباس خود را بشوید و غسل کند. او بعد از غروب طاهر خواهد بود.
16 Lakini kama hakufua nguo zake na kuoga, atakuwa na hatia kwa kosa hilo.’”
ولی اگر لباسهایش را نشوید و غسل نکند مجرم خواهد بود.»

< Mambo ya Walawi 17 >