< Mambo ya Walawi 16 >
1 Bwana akasema na Mose baada ya kifo cha wale wana wawili wa Aroni waliokufa walipokaribia mbele za Bwana.
Y él Señor dijo a Moisés, después de la muerte de los dos hijos de Aarón, cuando tomaron fuego extraño delante del Señor y la muerte los alcanzó;
2 Bwana akamwambia Mose: “Mwambie ndugu yako Aroni asije wakati wowote atakavyo yeye ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, nyuma ya pazia pale mbele ya kiti cha rehema kile kilichoko juu ya Sanduku la Agano, la sivyo atakufa, kwa sababu huwa ninatokea ndani ya wingu juu ya kile kiti cha rehema.
El Señor le dijo a Moisés: Dile a Aarón, tu hermano, que no puede venir en todo momento al lugar santo dentro del velo, delante del propiciatorio, por temor a que la muerte lo alcance; porque seré visto en la nube en la cubierta del cofre.
3 “Hivi ndivyo Aroni atakavyoingia katika mahali patakatifu: atachukua fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
Dejemos que Aarón venga al lugar santo de esta manera: con un buey para el sacrificio por el pecado y un carnero para el sacrificio.
4 Atavaa koti takatifu la kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani; atafunga mshipi wa kitani kiunoni, na kuvaa kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu, kwa hiyo ni lazima aoge kwa maji kabla ya kuyavaa mavazi hayo.
Deja que se ponga el saco de lino sagrado, el pantalón de lino sobre su cuerpo, él cinto de lino ceñido y la mitra de lino sobre la cabeza porque esto es ropa santa, y antes de ponerlos sobre su cuerpo, debe ser lavado con agua.
5 Atachukua mbuzi dume wawili kutoka kwa jumuiya ya Israeli kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
Y que tome de los hijos de Israel dos chivos para el sacrificio por el pecado y un carnero para el holocausto.
6 “Aroni atamtoa huyo fahali kwa ajili ya sadaka yake ya dhambi ili afanye upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake.
Y Aarón debe dar el buey de la ofrenda por el pecado para sí mismo, para que él y su casa se liberen del pecado.
7 Kisha atawachukua wale mbuzi dume wawili na kuwaleta mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
Y él tiene que tomar las dos cabras y ponerlas delante del Señor en la puerta de la tienda de la reunión.
8 Aroni atapiga kura kwa ajili ya hao mbuzi wawili, mmoja kwa ajili ya Bwana na mwingine kwa ajili ya kubebeshwa dhambi.
Y Aarón echará suertes sobre los dos machos cabríos, una suerte para el Señor y una suerte para él macho cabrío expiatorio.
9 Aroni atamleta yule mbuzi ambaye kura ya Bwana imemwangukia na kumtoa dhabihu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Y el macho cabrío que está marcada para el Señor, deja que Aarón haga una ofrenda por el pecado.
10 Lakini mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa kubebeshwa dhambi atatolewa akiwa hai mbele za Bwana, atumike kwa kufanya upatanisho kwa kumwacha aende jangwani akiwa amebebeshwa dhambi.
Pero el macho cabrío expiatorio debe colocarse vivo delante del Señor, para quitar el pecado, para que pueda ser enviada con todas las maldad de ellos a las tierras del desierto.
11 “Aroni atamleta yule fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na nyumba yake, naye atamchinja huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe.
Y Aarón debe dar el becerro de la ofrenda por el pecado para sí mismo y quitar el pecado de sí mismo y de su casa, y matar el becerro de la ofrenda por el pecado que es para sí mismo.
12 Atachukua chetezo kilichojaa makaa yanayowaka kutoka madhabahuni mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba laini uliosagwa vizuri wenye harufu, na kuvipeleka nyuma ya pazia.
Y él tomará un vaso lleno de brasas que se quema del altar delante del Señor y en su mano un poco de incienso, y lo llevará dentro del velo;
13 Ataweka uvumba juu ya moto mbele za Bwana, na moshi wa uvumba utafunika kile kiti cha rehema kilicho juu ya Ushuhuda, ili asife.
Y tomará el incienso sobre el fuego delante del Señor para que el cofre se cubra con una nube del humo del perfume, que está sobre él testimonio para que la muerte no lo alcance.
14 Atachukua sehemu ya damu ya fahali, na kwa kidole chake atanyunyiza sehemu ya mbele ya kiti cha rehema; kisha atanyunyiza sehemu ya hiyo damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kiti cha rehema.
Y tomará algo de la sangre del buey, sacudiendo sus gotas de su dedo encima del propiciatorio en el lado este, y delante del propiciatorio, siete veces.
15 “Kisha atamchinja mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, na kuichukua damu yake nyuma ya pazia, na aifanyie kama alivyofanya kwa damu ya fahali: Atanyunyiza juu ya kiti cha rehema na mbele yake.
Entonces, degollara al macho cabrío de la ofrenda por el pecado, y lleva su sangre al interior del velo y haz con él lo que hizo con la sangre del buey, sacudiendo gotas encima y delante del cofre del pacto.
16 Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu kwa sababu ya unajisi na uasi wa Waisraeli, kwa dhambi zao zozote. Atafanya hivyo kwa ajili ya Hema la Kukutania, ambalo liko miongoni mwao katikati ya unajisi wao.
Y libere el lugar santo de todo lo que sea inmundo entre los hijos de Israel y de su maldad en todos sus pecados; y que haga lo mismo con la Tienda de reunión, que tiene su lugar entre un pueblo impuro.
17 Mtu yeyote haruhusiwi kuwa ndani ya Hema la Kukutania, kuanzia wakati Aroni anapoingia kufanya upatanisho katika Patakatifu pa Patakatifu, hadi atakapotoka nje, baada ya kujifanyia upatanisho yeye mwenyewe na nyumba yake, pamoja na jumuiya yote ya Israeli.
Y ningún hombre puede estar en la Tienda de reunión desde el momento en que Aarón entra para quitar el pecado en el lugar santo hasta que salga, habiéndose hecho a sí mismo, a su casa y a todo el pueblo de Israel libres del pecado.
18 “Kisha atatoka aje kwenye madhabahu yaliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake. Atachukua sehemu ya damu ya fahali na sehemu ya damu ya mbuzi, na kuiweka kwenye pembe za madhabahu.
Y saldrá al altar que está delante del Señor y lo liberará del pecado; y él debe tomar algo de la sangre del buey y la sangre del chivo y ponerla en los cuernos del altar y rodearla;
19 Atanyunyiza baadhi ya hiyo damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, ili kuitakasa na kuiweka wakfu kutokana na unajisi wa Waisraeli.
Sacudir las gotas de sangre de su dedo en él siete veces para santificarlo y limpiarlo de todo lo que sea inmundo entre los hijos de Israel.
20 “Aroni atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, atamleta mbele yule mbuzi aliye hai.
Y cuando haya hecho lo que sea necesario para hacer que el lugar santo y la Tienda de reunión y el altar estén libres de pecado, ponga al chivo viviente delante del Señor;
21 Aroni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai na kuungama juu yake uovu wote na uasi wa Waisraeli, yaani dhambi zao zote, ili kuziweka juu ya kichwa cha huyo mbuzi. Atamwachia huyo mbuzi akimbilie jangwani kwa uangalizi wa mtu aliyepewa wajibu huo.
Y Aarón, poniendo sus dos manos sobre la cabeza del chivo viviente, hará una declaración pública sobre él de todas las malas acciones de los hijos de Israel y de todas sus malas acciones, en todos sus pecados; y los pondrá sobre la cabeza del chivo y lo enviará lejos, al cuidado de un hombre que lo estará esperando allí, lo llevará y soltará en él desierto.
22 Yule mbuzi atachukua juu yake dhambi zao zote mpaka mahali pasipo na watu; naye yule mtu atamwachia akimbilie jangwani.
Y él chivo llevará sobre sí, todos sus pecados a una tierra separada de los hombres, y él enviará al chivo al desierto.
23 “Kisha Aroni ataenda ndani ya Hema la Kukutania na kuvua yale mavazi ya kitani aliyoyavaa kabla ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu, naye atayaacha pale.
Entonces, Aarón entrará en la Tienda de la reunión y se quitará la ropa de lino que se puso cuando entró en el lugar santo, y la dejara allí;
24 Ataoga kwa maji katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake ya kawaida. Kisha atatoka na kutoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yake na sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya watu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, na kwa ajili ya watu.
Y después se bañará su cuerpo en agua en un lugar santo, debe ponerse su ropa y salir y dar su ofrenda quemada y la ofrenda quemada de la gente, para quitar su pecado y el pecado de la gente.
25 Pia atachoma mafuta ya mnyama wa sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
Y la grasa de la ofrenda por el pecado será quemada por él en el altar.
26 “Yule mtu anayemwachia yule mbuzi wa kubebeshwa dhambi ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji; baadaye anaweza kuingia kambini.
Y el hombre que soltó el chivo; como chivo expiatorio debe lavarse la ropa y bañar su cuerpo en agua para luego regresar al campamento de la tienda.
27 Yule fahali na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi, ambao damu yao ilikuwa imeletwa Patakatifu pa Patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho, ni lazima watolewe nje ya kambi. Ngozi zao, nyama, na matumbo pamoja na mavi vitateketezwa kwa moto.
Y el becerro de la ofrenda por el pecado y él chivo de la ofrenda por el pecado, cuya sangre fue tomada para hacer que el lugar santo esté libre del pecado, deben ser sacados fuera del campamento de la Tienda, sus pieles, la carne y sus desperdicios serán quemados con fuego.
28 Mtu atakayevichoma ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; baadaye ataweza kuingia kambini.
Y el hombre por el cual son quemados es lavado, su ropa y su cuerpo bañado en agua, para luego regresar al campamento de la tienda.
29 “Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ni lazima mfunge, wala msifanye kazi yoyote, iwe mzawa au mgeni anayeishi miongoni mwenu,
Y sea para ustedes una orden para siempre: en el séptimo mes, en el décimo día, deben mantenerse a sí mismos sin placer y no hacer ningún tipo de trabajo, los que son israelitas de nacimiento y los de otras tierras. quienes viven entre ustedes.
30 kwa sababu siku hii upatanisho utafanyika kwa ajili yenu ili kuwatakasa. Kisha mtakuwa safi mbele za Bwana kutokana na dhambi zenu zote.
Porque en este día tu pecado será quitado y serás limpio: serás libre de todos tus pecados ante el Señor.
31 Ni Sabato ya mapumziko, na lazima mfunge; ni agizo la kudumu.
Es un sábado especial para ustedes, y ustedes deben humillarse; Es una orden para siempre.
32 Kuhani ambaye ametiwa mafuta na kuwekwa wakfu ili kuingia mahali pa baba yake kama kuhani mkuu atafanya upatanisho. Atavaa mavazi matakatifu ya kitani,
Y el hombre sobre cuya cabeza se ha puesto el aceite santo, y que ha sido señalado como sacerdote en lugar de su padre, hará lo que sea necesario para quitar el pecado, y se pondrá la ropa de lino. incluso las ropas santas.
33 na kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, na pia kwa ajili ya makuhani, pamoja na jumuiya yote ya watu.
Y hará la purificación del lugar santo y la Tienda de reunión y el altar del pecado; Él quitará el pecado de los sacerdotes y de todo el pueblo.
34 “Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Upatanisho utafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa ajili ya dhambi zote za Waisraeli.” Ndivyo ilivyofanyika, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Y sea para siempre una orden para ustedes, para que el pecado de los hijos de Israel se pueda quitar una vez al año. Se hizo lo que el Señor le mandó a Moisés.