< Mambo ya Walawi 16 >

1 Bwana akasema na Mose baada ya kifo cha wale wana wawili wa Aroni waliokufa walipokaribia mbele za Bwana.
Poslije smrti dvojice Aronovih sinova, koji su poginuli prinoseći pred Jahvom neposvećenu vatru, progovori Jahve Mojsiju.
2 Bwana akamwambia Mose: “Mwambie ndugu yako Aroni asije wakati wowote atakavyo yeye ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, nyuma ya pazia pale mbele ya kiti cha rehema kile kilichoko juu ya Sanduku la Agano, la sivyo atakufa, kwa sababu huwa ninatokea ndani ya wingu juu ya kile kiti cha rehema.
Jahve reče Mojsiju: “Kaži svome bratu Aronu da ne ulazi u svako doba u Svetište iza zavjese, pred Pomirilište koje se nalazi na Kovčegu, da ne pogine. Jer ja ću se pojavljivati nad Pomirilištem u oblaku.
3 “Hivi ndivyo Aroni atakavyoingia katika mahali patakatifu: atachukua fahali mchanga kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
Neka Aron ulazi u Svetište ovako: s juncem za žrtvu okajnicu i ovnom za žrtvu paljenicu.
4 Atavaa koti takatifu la kitani, pamoja na nguo za ndani za kitani; atafunga mshipi wa kitani kiunoni, na kuvaa kilemba cha kitani. Haya ni mavazi matakatifu, kwa hiyo ni lazima aoge kwa maji kabla ya kuyavaa mavazi hayo.
Neka se obuče u posvećenu košulju od lana; na svoje tijelo neka navuče gaće od lana; neka se opaše lanenim pasom, a na glavu stavi mitru od lana. To je posvećeno ruho koje ima obući pošto se okupa u vodi.
5 Atachukua mbuzi dume wawili kutoka kwa jumuiya ya Israeli kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
Od zajednice izraelske neka primi dva jarca za žrtvu okajnicu i jednoga ovna za žrtvu paljenicu.
6 “Aroni atamtoa huyo fahali kwa ajili ya sadaka yake ya dhambi ili afanye upatanisho kwa ajili yake mwenyewe na nyumba yake.
Pošto Aron prinese junca za žrtvu okajnicu za svoj grijeh i izvrši obred pomirenja za se i za svoj dom,
7 Kisha atawachukua wale mbuzi dume wawili na kuwaleta mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
neka uzme oba jarca i postavi ih pred Jahvu na ulaz u Šator sastanka.
8 Aroni atapiga kura kwa ajili ya hao mbuzi wawili, mmoja kwa ajili ya Bwana na mwingine kwa ajili ya kubebeshwa dhambi.
Neka Aron baci kocke za oba jarca te jednoga odredi kockom Jahvi, a drugoga Azazelu.
9 Aroni atamleta yule mbuzi ambaye kura ya Bwana imemwangukia na kumtoa dhabihu kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Jarca na kojega je kocka pala da bude Jahvi neka Aron prinese za žrtvu okajnicu.
10 Lakini mbuzi aliyechaguliwa kwa kura kuwa wa kubebeshwa dhambi atatolewa akiwa hai mbele za Bwana, atumike kwa kufanya upatanisho kwa kumwacha aende jangwani akiwa amebebeshwa dhambi.
A jarac na kojega je kocka pala da bude Azazelu neka se smjesti živ pred Jahvu, da se nad njim obavi obred pomirenja i otpremi Azazelu u pustinju.
11 “Aroni atamleta yule fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake na nyumba yake, naye atamchinja huyo fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi yake mwenyewe.
Zatim neka Aron prinese junca za žrtvu okajnicu za svoj grijeh; i obavi obred pomirenja za se i za svoj dom: i neka zakolje toga junca za žrtvu okajnicu za svoj grijeh.
12 Atachukua chetezo kilichojaa makaa yanayowaka kutoka madhabahuni mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba laini uliosagwa vizuri wenye harufu, na kuvipeleka nyuma ya pazia.
Potom neka uzme kadionik pun užarena ugljevlja sa žrtvenika ispred Jahve i dvije pune pregršti miomirisnoga tamjana u prah smrvljenoga. Neka to unese iza zavjese.
13 Ataweka uvumba juu ya moto mbele za Bwana, na moshi wa uvumba utafunika kile kiti cha rehema kilicho juu ya Ushuhuda, ili asife.
Sad neka stavi tamjan na vatru pred Jahvom da oblak od tamjana zastre Pomirilište što je na Svjedočanstvu. Tako neće poginuti.
14 Atachukua sehemu ya damu ya fahali, na kwa kidole chake atanyunyiza sehemu ya mbele ya kiti cha rehema; kisha atanyunyiza sehemu ya hiyo damu kwa kidole chake mara saba mbele ya kiti cha rehema.
Poslije toga neka uzme krvi od junca i svojim prstom poškropi istočnu stranu Pomirilišta; a ispred Pomirilišta neka svojim prstom poškropi sedam puta tom krvlju.
15 “Kisha atamchinja mbuzi wa sadaka ya dhambi kwa ajili ya watu, na kuichukua damu yake nyuma ya pazia, na aifanyie kama alivyofanya kwa damu ya fahali: Atanyunyiza juu ya kiti cha rehema na mbele yake.
Neka potom zakolje jarca za žrtvu okajnicu za grijeh naroda; neka unese njegovu krv za zavjesu te s njegovom krvi učini kako je učinio s krvlju od junca: neka njome poškropi po Pomirilištu i pred njim.
16 Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu kwa sababu ya unajisi na uasi wa Waisraeli, kwa dhambi zao zozote. Atafanya hivyo kwa ajili ya Hema la Kukutania, ambalo liko miongoni mwao katikati ya unajisi wao.
Tako će obaviti obred pomirenja nad Svetištem zbog nečistoća Izraelaca, zbog njihovih prijestupa i svih njihovih grijeha. A tako neka učini i za Šator sastanka što se među njima nalazi, sred njihovih nečistoća.
17 Mtu yeyote haruhusiwi kuwa ndani ya Hema la Kukutania, kuanzia wakati Aroni anapoingia kufanya upatanisho katika Patakatifu pa Patakatifu, hadi atakapotoka nje, baada ya kujifanyia upatanisho yeye mwenyewe na nyumba yake, pamoja na jumuiya yote ya Israeli.
Kad on uđe da obavi obred pomirenja u Svetištu, neka nikoga drugog ne bude u Šatoru sastanka dok on ne iziđe. Obavivši obred pomirenja za se, za svoj dom i za svu izraelsku zajednicu,
18 “Kisha atatoka aje kwenye madhabahu yaliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake. Atachukua sehemu ya damu ya fahali na sehemu ya damu ya mbuzi, na kuiweka kwenye pembe za madhabahu.
neka ode k žrtveniku koji se nalazi pred Jahvom te nad žrtvenikom obavi obred pomirenja. Neka uzme krvi od junca i krvi od jarca pa stavi na rogove oko žrtvenika.
19 Atanyunyiza baadhi ya hiyo damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, ili kuitakasa na kuiweka wakfu kutokana na unajisi wa Waisraeli.
Neka svojim prstom poškropi žrtvenik istom krvlju sedam puta. Tako će ga očistiti od nečistoća Izraelaca i posvetiti.
20 “Aroni atakapokuwa amemaliza kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, atamleta mbele yule mbuzi aliye hai.
Kad svrši obred pomirenja Svetišta, Šatora sastanka i žrtvenika, neka primakne jarca živoga.
21 Aroni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha mbuzi aliye hai na kuungama juu yake uovu wote na uasi wa Waisraeli, yaani dhambi zao zote, ili kuziweka juu ya kichwa cha huyo mbuzi. Atamwachia huyo mbuzi akimbilie jangwani kwa uangalizi wa mtu aliyepewa wajibu huo.
Neka mu na glavu Aron stavi obje svoje ruke i nad njim ispovjedi sve krivnje Izraelaca, sve njihove prijestupe i sve njihove grijehe. Položivši ih tako jarcu na glavu, neka ga pošalje u pustinju s jednim prikladnim čovjekom.
22 Yule mbuzi atachukua juu yake dhambi zao zote mpaka mahali pasipo na watu; naye yule mtu atamwachia akimbilie jangwani.
Tako će jarac na sebi odnijeti sve njihove krivnje u pusti kraj. Otpremivši jarca u pustinju,
23 “Kisha Aroni ataenda ndani ya Hema la Kukutania na kuvua yale mavazi ya kitani aliyoyavaa kabla ya kuingia katika Patakatifu pa Patakatifu, naye atayaacha pale.
neka se Aron vrati u Šator sastanka, sa sebe svuče lanenu odjeću u koju se bio obukao kad je ulazio u Svetište i neka je ondje ostavi.
24 Ataoga kwa maji katika mahali patakatifu na kuvaa mavazi yake ya kawaida. Kisha atatoka na kutoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yake na sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya watu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe, na kwa ajili ya watu.
Neka potom opere svoje tijelo vodom na posvećenu mjestu, na se obuče svoju odjeću te iziđe da prinese svoju žrtvu paljenicu i žrtvu paljenicu naroda i obavi obred pomirenja za se i za narod.
25 Pia atachoma mafuta ya mnyama wa sadaka ya dhambi juu ya madhabahu.
Loj sa žrtve okajnice neka sažeže u kad na žrtveniku.
26 “Yule mtu anayemwachia yule mbuzi wa kubebeshwa dhambi ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji; baadaye anaweza kuingia kambini.
Onaj koji je odveo jarca Azazelu neka opere svoju odjeću, svoje tijelo u vodi okupa i poslije toga može opet doći u tabor.
27 Yule fahali na mbuzi waliotolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi, ambao damu yao ilikuwa imeletwa Patakatifu pa Patakatifu kwa ajili ya kufanya upatanisho, ni lazima watolewe nje ya kambi. Ngozi zao, nyama, na matumbo pamoja na mavi vitateketezwa kwa moto.
A junca žrtve okajnice i jarca žrtve okajnice od kojih je krv bila donesena u Svetište da se obavi obred pomirenja neka odnesu izvan tabora pa neka na vatri spale njihove kože, njihovo meso i njihovu nečist.
28 Mtu atakayevichoma ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji; baadaye ataweza kuingia kambini.
Tko ih bude spaljivao, neka opere svoju odjeću, svoje tijelo okupa u vodi i poslije toga može opet doći u tabor.
29 “Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Katika siku ya kumi ya mwezi wa saba ni lazima mfunge, wala msifanye kazi yoyote, iwe mzawa au mgeni anayeishi miongoni mwenu,
Ovaj zakon neka za vas trajno vrijedi. U sedmom mjesecu, deseti dan toga mjeseca, postite i ne obavljajte nikakva posla: ni domorodac ni stranac koji među vama boravi.
30 kwa sababu siku hii upatanisho utafanyika kwa ajili yenu ili kuwatakasa. Kisha mtakuwa safi mbele za Bwana kutokana na dhambi zenu zote.
Jer toga dana nad vama se ima izvršiti obred pomirenja da se očistite od svih svojih grijeha te da pred Jahvom budete čisti.
31 Ni Sabato ya mapumziko, na lazima mfunge; ni agizo la kudumu.
Neka je to za vas subotnji počinak kad postite. Trajan je to zakon.
32 Kuhani ambaye ametiwa mafuta na kuwekwa wakfu ili kuingia mahali pa baba yake kama kuhani mkuu atafanya upatanisho. Atavaa mavazi matakatifu ya kitani,
Neka obred pomirenja obavi onaj svećenik koji bude pomazan i posvećen za vršenje svećeničke službe namjesto svoga oca. Neka se obuče u posvećeno laneno ruho;
33 na kufanya upatanisho kwa ajili ya Patakatifu pa Patakatifu, Hema la Kukutania na madhabahu, na pia kwa ajili ya makuhani, pamoja na jumuiya yote ya watu.
on neka obavi obred pomirenja za posvećeno Svetište, za Šator sastanka i za žrtvenik. Zatim neka izvrši obred pomirenja nad svećenicima i nad svim narodom zajednice.
34 “Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu: Upatanisho utafanywa mara moja tu kwa mwaka kwa ajili ya dhambi zote za Waisraeli.” Ndivyo ilivyofanyika, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
Tako neka to bude za vas trajan zakon; jednom na godinu neka se nad Izraelcima obavi obred pomirenja za sve njihove grijehe.” Mojsije je učinio kako mu je Jahve naredio.

< Mambo ya Walawi 16 >