< Mambo ya Walawi 15 >

1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Perwerdigar Musa bilen Harun’gha söz qilip mundaq dédi: —
2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.
Israillargha mundaq denglar: — Herqandaq erkekning öz ténidin aqma chiqsa shu kishi shu aqma sewebidin napak sanalsun.
3 Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:
Aqma chiqishtin bolghan napakliq toghrisidiki höküm shuki, aqmisi meyli ténidin éqip tursun yaki éqishtin toxtitilghan bolsun, shu kishi yenila napak sanalsun;
4 “‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.
mundaq aqma bolghan kishi yatqan herbir orun-körpe napak sanilidu we u qaysi nersining üstide oltursa shu nersimu napak sanilidu.
5 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Kimki u yatqan orun-körpige tegse, öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun, andin kech kirgüche napak sanalsun.
6 Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Shuningdek kimki mundaq aqma bolghan kishi olturghan nerside oltursa öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
7 “‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Kimki aqma bolghan kishining ténige tegse, öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun, we kech kirgüche napak sanalsun.
8 “‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Eger aqma bolghan kishi pak birsige tükürse, shu kishi öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun, kech kirgüche napak sanalsun.
9 “‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi,
Qaysibir éger-toqumning üstige [aqma bolghan] kishi minse, shu nerse napak sanalsun.
10 na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Kimki uning tégide qoyulghan nersilerge tegse kech kirgüche napak sanilidu; we kimki shu nersilerni kötürse, öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun, we kech kirgüche napak sanalsun.
11 “‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Aqma bolghan kishi qolini yumastin birkimge tegküzse, shu kishi öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
12 “‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.
Aqma bolghan kishi sapal qachini tutup salsa, shu qacha chéqiwétilsun; yaghach qacha bolsa suda yuyulsun.
13 “‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika.
Qachaniki aqma bar kishi aqma halitidin qutulsa, özining pak qilinishi üchün yette künni hésablap ötküzüp, andin kiyimlirini yuyup, éqin suda yuyunsun; andin pak sanilidu.
14 Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani.
Sekkizinchi küni ikki paxtek yaki ikki bachkini élip, jamaet chédirining kirish aghzigha, Perwerdigarning aldigha keltürüp, kahin’gha tapshursun.
15 Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.
Kahin ulardin birini gunah qurbanliqi üchün, yene birini köydürme qurbanliq üchün sunsun. Bu yol bilen kahin Perwerdigarning aldida uning aqma bolghanliqigha kafaret keltüridu.
16 “‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
Eger bir erkekning meniysi özlükidin chiqip ketken bolsa, u pütün bedinini suda yusun, u kech kirgüche napak sanalsun.
17 Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni.
Shuningdek ademning meniysi qaysi kiyimige yaki térisige yuqup qalsa, suda yuyulsun we kech kirgüche napak sanalsun.
18 Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
Er we ayal kishi bir-birige yéqinlishishi bilen meniy chiqsa, ikkisi yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
19 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
Eger ayal kishiler aqma kélish halitide tursa we aqmisi xun bolsa, u yette kün’giche «ayrim» tursun; kimki uninggha tegse kech kirgüche napak sanalsun.
20 “‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi.
«Ayrim» turush mezgilide, qaysi nersining üstide yatsa, shu nerse napak sanilidu, shundaqla qaysi nersining üstide olturghan bolsa, shu nersimu napak sanalsun.
21 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Herkim uning orun-körpisige tegse öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
22 Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Herkim u olturghan nersige tegse, öz kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
23 Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.
We eger birkim u yatqan yaki olturghan jayda qoyulghan birer nersige tegse, kech kirgüche napak sanalsun.
24 “‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.
Eger bir er kishi shu halettiki ayal bilen birge yatsa, shundaqla uning xun napakliqi shu erge yuqup qalsa, u yette kün’giche napak sanalsun; u yatqan herbir orun-körpimu napak sanalsun.
25 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake.
Eger ayal kishining adet waqtining sirtidimu birnechche kün’giche xuni kélip tursa, yaki xun aqmisi adet waqtidin éship ketken bolsa, undaqta bu napak qan éqip turghan künlirining hemmiside, u adet künliride turghandek sanalsun, yene napak sanalsun.
26 Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi.
Qan kelgen herbir künde u qaysi orun-körpe üstide yatsa, bular u adet künliride yatqan orun-körpilerdek hésablinidu; u qaysi nersining üstide olturghan bolsa, shu nerse adet künlirining napakliqidek napak sanalsun.
27 Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Herkim bu nersilerge tegse napak bolidu; shu kishi kiyimlirini yuyup, suda yuyunsun we kech kirgüche napak sanalsun.
28 “‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada.
Ayal kishi qachan xun kélishtin saqaysa, u yette künni hésablap, ötküzüp bolghanda pak sanilidu.
29 Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
Sekkizinchi küni u ikki paxtek yaki ikki bachkini élip jamaet chédirining kirish aghzigha, kahinning qéshigha keltürsun.
30 Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.
Kahin bularning birini gunah qurbanliqi üchün, yene birini köydürme qurbanliq üchün ötküzsun; bu yol bilen kahin uning napak aqma qénidin pak bolushigha uning üchün Perwerdigarning aldida kafaret keltüridu.
31 “‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu, ambayo yapo katikati yao.’”
Siler mushu yol bilen Israillarni napakliqidin üzünglar; bolmisa, ular napakliqida turiwérip, ularning arisida turghan méning turalghu chédirimni bulghishi tüpeylidin napak halitide ölüp kétidu.
32 Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa,
Aqma kélish halitide bolghan kishi we meniy kétish bilen napak bolghan kishi toghrisida,
33 kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.
Shuningdek xun kélish künliridiki aghriq ayal kishi toghruluq, aqma halette bolghan er we ayal toghruluq, napak halettiki ayal bille yatqan er toghruluq kelgen qanun-belgilime mana shulardur.

< Mambo ya Walawi 15 >