< Mambo ya Walawi 15 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Yahvé habló a Moisés y a Aarón, diciendo:
2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.
“Hablad a los hijos de Israel y decidles: ‘Cuando un hombre tenga flujo de su cuerpo, a causa de su flujo será impuro.
3 Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:
Esta será su impureza en su flujo: ya sea que su cuerpo corra con su flujo, o que su cuerpo se haya detenido por su flujo, es su impureza.
4 “‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.
“‘Todo lecho sobre el que se acueste el que tiene el flujo será impuro; y todo aquello sobre lo que se siente será impuro.
5 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
El que toque su lecho lavará su ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
6 Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
El que se siente sobre cualquier cosa en la que se haya sentado el hombre que tiene el flujo, lavará su ropa, se bañará con agua y quedará impuro hasta la noche.
7 “‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
“‘El que toque el cuerpo del que tiene el flujo se lavará la ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
8 “‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
“‘Si el que tiene el flujo escupe sobre el que está limpio, entonces lavará su ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
9 “‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi,
“‘Cualquier silla de montar que lleve el enfermo será impura.
10 na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
El que toque cualquier cosa que haya estado debajo de él quedará impuro hasta la noche. El que lleve esas cosas se lavará la ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
11 “‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
“‘Cualquiera que toque el que tiene el flujo, sin haberse lavado las manos con agua, lavará su ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
12 “‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.
“‘La vasija de barro que toque el que tiene él flujo, será rota; y toda vasija de madera será enjuagada en agua.
13 “‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika.
“‘Cuando el que tiene flujo se limpie de su flujo, contará para sí siete días para su purificación, y lavará sus vestidos; y bañará su carne en agua corriente, y quedará limpio.
14 Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani.
“‘Al octavo día tomará dos tórtolas o dos pichones de paloma, y se presentará ante Yahvé a la puerta de la Tienda del Encuentro, y los entregará al sacerdote.
15 Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.
El sacerdote los ofrecerá, uno como ofrenda por el pecado y el otro como holocausto. El sacerdote hará la expiación por él ante Yahvé por su liberación.
16 “‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
“‘Si un hombre tiene una emisión de semen, se lavará con agua toda su carne y quedará impuro hasta la noche.
17 Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni.
Toda la ropa y toda la piel sobre la que haya semen se lavará con agua, y quedará impura hasta la noche.
18 Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
Si un hombre se acuesta con una mujer y hay emisión de semen, ambos se bañarán con agua y quedarán impuros hasta la noche.
19 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
“‘Si una mujer tiene flujo, y su flujo en su carne es de sangre, estará en su impureza siete días. Quien la toque será impuro hasta la noche.
20 “‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi.
“‘Todo lo que ella se acueste en su impureza será impuro. Todo lo que ella se siente será impuro.
21 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
El que toque su lecho lavará su ropa y se bañará en agua, y quedará impuro hasta la noche.
22 Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
El que toque algo sobre lo que ella se siente, lavará su ropa, se bañará con agua y quedará impuro hasta la noche.
23 Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.
Si está en la cama o en cualquier cosa sobre la que ella se siente, cuando la toque será impuro hasta la noche.
24 “‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.
“‘Si alguno se acuesta con ella, y su flujo menstrual está sobre él, será impuro siete días; y toda cama en la que se acueste será impura.
25 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake.
“‘Si una mujer tiene una descarga de su sangre muchos días fuera del tiempo de su período, o si tiene una descarga más allá del tiempo de su período, todos los días de la descarga de su impureza serán como en los días de su período. Será impura.
26 Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi.
Toda cama en la que se acueste durante todos los días de su flujo será para ella como la cama de su período. Todo aquello sobre lo que se siente será impuro, como la impureza de su menstruación.
27 Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Quien toque estas cosas quedará impuro, lavará su ropa y se bañará con agua, y quedará impuro hasta la noche.
28 “‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada.
“‘Pero si se limpia de su flujo, contará para sí siete días, y después de eso quedará limpia.
29 Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
Al octavo día tomará dos tórtolas o dos pichones y los llevará al sacerdote, a la puerta de la Tienda de reunión.
30 Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.
El sacerdote ofrecerá una como ofrenda por el pecado, y la otra como holocausto; y el sacerdote hará expiación por ella ante Yahvé por la impureza de su flujo.
31 “‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu, ambayo yapo katikati yao.’”
“‘Así separarás a los hijos de Israel de su impureza, para que no mueran en su impureza cuando contaminen mi tabernáculo que está en medio de ellos’”.
32 Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa,
Esta es la ley del que tiene flujo, y del que tiene emisión de semen, de modo que es impuro por ello;
33 kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.
y de la que tiene la menstruación, y del hombre o la mujer que tiene flujo, y del que se acuesta con ella que es impuro.