< Mambo ya Walawi 15 >

1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
And the Lord spak to Moises and Aaron, `and seide,
2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.
Speke ye to the sones of Israel, and seie ye to hem, A man that suffrith the rennyng out of seed, schal be vncleene;
3 Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:
and thanne he schal be demed to be suget to this vice, whanne bi alle momentis foul vmour `ethir moysture cleueth to his fleisch, and growith togidere.
4 “‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.
Ech bed in which he slepith schal be vncleene, and where euer he sittith.
5 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
If ony man touchith his bed, he schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
6 Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
If a man sittith where he satt, also thilke man schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vnclene `til to euentid.
7 “‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
He that touchith hise fleischis, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
8 “‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
If sich a man castith out spetyng on hym that is cleene, he schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
9 “‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi,
The sadil on which he sittith,
10 na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
schal be vncleene; and ech man that touchith what euer thing is vndur hym that suffrith the fletyng out of seed, schal be defoulid `til to euentid. He that berith ony of these thingis, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
11 “‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Ech man, whom he that is such touchith with hondis not waischun bifore, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
12 “‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.
`A vessel of erthe which he touchith, schal be brokun; but a `vessel of tre schal be waischun in watir.
13 “‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika.
If he that suffrith sich a passioun, is heelid, he schal noumbre seuene daies aftir his clensyng, and whanne the clothis and al `the bodi ben waischun in lyuynge watris, he schal be clene.
14 Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani.
Forsothe in the eiytthe dai he schal take twei turtlis, ethir twei `briddis of a culuer, and he schal come in the `siyt of the Lord at the dore of tabernacle of witnessyng, and schal yyue tho to the preest;
15 Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.
and the preest schal make oon for synne, and the tother in to brent sacrifice; and the preest schal preye for hym bifor the Lord, that he be clensid fro the fletyng out of his seed.
16 “‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
A man fro whom the seed of letcherie, `ethir of fleischli couplyng, goith out, schal waische in watir al his bodi, and he schal be vncleene `til to euentid.
17 Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni.
He schal waische in watir the cloth `and skyn which he hath, and it schal be unclene `til to euentid.
18 Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
The womman with which he `is couplid fleischli, schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
19 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
A womman that suffrith the fletyng out of blood, whanne the moneth cometh ayen, schal be departid bi seuene daies; ech man that touchith hir schal be vncleene `til to euentid,
20 “‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi.
and the place in which sche slepith ether sittith in the daies of hir departyng, schal be defoulid.
21 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
He that touchith her bed, schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
22 Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Who euer touchith ony vessel on which sche sittith, he schal waische hise clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be defoulid `til to euentid.
23 Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.
24 “‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.
If a man is couplid fleischli with hir in the tyme of blood that renneth bi monethis, he schal be vncleene bi seuene daies, and ech bed in which he slepith schal be defoulid.
25 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake.
A womman that suffrith in many daies the `fletyng out of blood, not in the tyme of monethis, ethir which womman ceessith not to flete out blood aftir the blood of monethis, schal be vncleene as longe as sche `schal be suget to this passioun, as if sche is in the tyme of monethis.
26 Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi.
Ech bed in which sche slepith, and `vessel in which sche sittith, schal be defoulid.
27 Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Who euer touchith hir schal waische his clothis, and he schal be waischun in watir, and schal be vncleene `til to euentid.
28 “‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada.
If the blood stondith, and ceessith to flete out, sche schal noumbre seuene daies of hir clensyng,
29 Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
and in the eiytthe dai sche schal offre for hir silf to the preest twei turtlis, ethir twei `briddis of culueris, at the dore of the tabernacle of witnessyng;
30 Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.
and the preest schal make oon for synne, and the tothir in to brent sacrifice; and the preest schal preye for hir bifor the Lord, and for the fletyng out of hir vnclennesse.
31 “‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu, ambayo yapo katikati yao.’”
Therfor ye schulen teche the sones of Israel, that thei eschewe vnclennessis, and that thei die not for her filthis, whanne thei defoulen my tabernacle which is among hem.
32 Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa,
This is the lawe of hym that suffrith fletyng out of seed, and which is defoulid with fleischly couplyng,
33 kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.
and of a womman which is departid in the tymes of monethis, ethir which flowith out in contynuel blood, and of the man that slepith with hir.

< Mambo ya Walawi 15 >