< Mambo ya Walawi 15 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Yahweh spoke to Moses and to Aaron, saying,
2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.
“Speak to the people of Israel, and say to them, 'When any man has an infected fluid that comes out of his body, he becomes unclean.
3 Iwe unaendelea kutiririka kutoka mwilini mwake au umeziba, utamfanya kuwa najisi. Hivi ndivyo usaha wake utakavyomletea unajisi:
His uncleanness is due to this infected fluid. Whether his body flows with fluid or is stopped up, it is unclean.
4 “‘Kitanda chochote atakacholalia mtu mwenye kutokwa na usaha kitakuwa najisi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi.
Every bed on which he lies will be unclean, and everything on which he sits will be unclean.
5 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever touches his bed must wash his clothes and bathe himself in water, and be unclean until evening.
6 Yeyote atakayeketi juu ya kitu chochote alichokalia mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Anyone who sits on anything on which the man with the flow of infected fluid sat, that person must wash his clothes and bathe himself in water, and he will be unclean until evening.
7 “‘Yeyote atakayemgusa mtu mwenye kutokwa na usaha, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Anyone who touches the body of the one who has a flow of infected fluid must wash his clothes and bathe himself in water, and be unclean until evening.
8 “‘Ikiwa mtu mwenye kutokwa na usaha atamtemea mate mtu yeyote ambaye ni safi, mtu huyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
If the person who has such a flow of fluid spits on someone who is clean, then that person must wash his clothes and bathe himself in water, and he will be unclean until evening.
9 “‘Kila tandiko ambalo mtu huyo atalikalia wakati wa kupanda mnyama litakuwa najisi,
Any saddle which he who has a flow rides upon will be unclean.
10 na yeyote atakayegusa kitu chochote alichokuwa amekalia atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayeinua vitu hivyo ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever touches anything that was under that person will be unclean until evening, and anyone who carries those things must wash his clothes and bathe himself in water; he will be unclean until evening.
11 “‘Yeyote atakayeguswa na mtu anayetokwa na usaha bila kunawa mikono yake kwa maji, ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whomever he who has such a flow touches without first having rinsed his hands in water, the person who was touched must wash his clothes and bathe himself in water, and he will be unclean until evening.
12 “‘Chungu cha udongo kitakachoguswa na mtu huyo ni lazima kivunjwe, na kifaa chochote cha mbao kitaoshwa kwa maji.
Any clay pot that the one with such a flow of fluid touches must be broken, and every container of wood must be rinsed in water.
13 “‘Wakati mtu atakapotakasika kutoka usaha wake, anapaswa kuhesabu siku saba kwa utakaso wake. Ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji safi, naye atatakasika.
When he who has a flow is cleansed from his flow, then he must count for himself seven days for his cleansing; then he must wash his clothes and bathe his body in running water. Then he will be clean.
14 Siku ya nane, atachukua hua wawili au makinda mawili ya njiwa, aje mbele za Bwana kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na kumpa kuhani.
On the eighth day he must take two doves or two young pigeons and come before Yahweh at the entrance to the tent of meeting; there he must give the birds to the priest.
15 Kuhani atavitoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya huyo mtu kwa sababu ya kutokwa usaha kwake.
The priest must offer them, one as a sin offering and the other as a burnt offering, and the priest must make atonement for him before Yahweh for his flow.
16 “‘Wakati mtu akitokwa na shahawa, ni lazima aoge mwili mzima kwa maji, na atakuwa najisi mpaka jioni.
If any man has an emission of semen, then he must bathe his whole body in water; he will be unclean until evening.
17 Vazi lolote ama ngozi yoyote yenye shahawa juu yake ni lazima ioshwe kwa maji, na itakuwa najisi mpaka jioni.
Every garment or leather on which there is semen must be washed with water; it will be unclean until evening.
18 Ikiwa mtu atalala na mwanamke, na kukawa na kutoka kwa shahawa, ni lazima wote waoge kwa maji, nao watakuwa najisi mpaka jioni.
If a woman and a man sleep together and there is a transfer of semen to her, they must both bathe themselves in water; they will be unclean until evening.
19 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu ya kawaida ya mwezi, atakuwa najisi kwa siku saba, na yeyote atakayemgusa atakuwa najisi mpaka jioni.
When a woman menstruates, her impurity will continue for seven days, and whoever touches her will be unclean until evening.
20 “‘Chochote atakacholalia wakati wake wa hedhi kitakuwa najisi, na chochote atakachokikalia kitakuwa najisi.
Everything she lies on during her period will be unclean; everything that she sits on will also be unclean.
21 Yeyote atakayegusa kitanda chake ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever touches her bed must wash his clothes and bathe himself in water; that person will be unclean until evening.
22 Yeyote atakayegusa chochote atakachokalia ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever touches anything that she sits on must wash his clothes and bathe himself in water; that person will be unclean until evening.
23 Kiwe ni kitanda ama chochote alichokuwa amekikalia, ikiwa mtu yeyote atakigusa, atakuwa najisi mpaka jioni.
Whether it is on the bed or on anything on which she sits, if he touches it, that person will be unclean until evening.
24 “‘Ikiwa mwanaume atalala naye na ile damu ya mwezi ikamgusa, atakuwa najisi kwa siku saba; kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanaume kitakuwa najisi.
If any man sleeps with her, and if her impure flow touches him, he will be unclean for seven days. Every bed on which he lies will be unclean.
25 “‘Ikiwa mwanamke atatokwa na damu kwa siku nyingi zaidi ya siku zake za mwezi, au amekuwa na damu inayoendelea zaidi ya kipindi chake, atakuwa najisi kwa kipindi chote cha shida hiyo, kama ilivyokuwa katika siku za hedhi yake.
If a woman has a flow of blood for many days that is not in the time of her menstruation, or if she has a flow beyond the time of her menstruation, during all the days of the flow of her uncleanness, she will be as if she were in the days of her period. She is unclean.
26 Kitanda chochote atakachokilalia huyo mwanamke wakati anaendelea kutokwa na damu kitakuwa najisi, kama kilivyokuwa kitanda chake wakati wa siku zake za hedhi, na chochote atakachokalia kitakuwa najisi, kama wakati wake wa hedhi.
Every bed on which she lies all during her flow of blood will be to her just like the bed on which she lies during her menstruation, and everything on which she sits will be unclean, just like the uncleanness of her menstruation.
27 Yeyote agusaye vitu hivyo atakuwa najisi; ni lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever touches any of those things will be unclean; he must wash his clothes and bathe himself in water, and he will be unclean until evening.
28 “‘Wakati atakapotakasika kutoka hedhi yake, ni lazima ahesabu siku saba, na baada ya hapo atakuwa safi kwa kawaida ya ibada.
But if she is cleansed from her flow of blood, then she will count for herself seven days, and after that she will be clean.
29 Siku ya nane ni lazima achukue hua wawili au makinda mawili ya njiwa, na kumletea kuhani kwenye mlango wa Hema la Kukutania.
On the eighth day she will take to her two doves or two young pigeons and bring them to the priest at the entrance to the tent of meeting.
30 Kuhani atatoa dhabihu, mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na huyo mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa. Kwa njia hii, atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana kwa sababu ya unajisi wa kutokwa damu kwake.
The priest will offer one bird as a sin offering and the other as a burnt offering, and he will make atonement for her before Yahweh for her unclean flow of blood.
31 “‘Ni lazima uwatenge Waisraeli kutokana na vitu ambavyo vinawafanya najisi, ili wasife katika unajisi wao kwa kunajisi makao yangu, ambayo yapo katikati yao.’”
This is how you must separate the people of Israel from their uncleanness, so they will not die due to their uncleanness, by defiling my tabernacle, where I live among them.
32 Haya ni masharti kwa ajili ya mtu mwenye kutokwa na usaha, kwa ajili ya yeyote atakayetokwa na shahawa,
These are the regulations for anyone who has a flow of fluid, for any man whose semen goes out of him and makes him unclean,
33 kwa ajili ya mwanamke katika siku zake za hedhi, kwa ajili ya mwanaume au mwanamke atokwaye na usaha, na kwa ajili ya mwanaume alalaye na mwanamke ambaye ni najisi kwa kawaida ya ibada.
for any woman who has a menstrual period, for anyone with a flow of fluid, whether male or female, and for any man who sleeps with an unclean woman.'”