< Mambo ya Walawi 14 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord spoke to Moses, saying:
2 “Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
This is the rite for a leper, when he is to be cleansed. He shall be brought to the priest,
3 Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
who, departing from the camp, when he has found the leprosy to be cleansed,
4 kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
shall instruct him who is to be purified to offer for himself two living sparrows, which it is lawful to eat, and cedar wood, and vermillion, and hyssop.
5 Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
And he shall order that one of the sparrows be immolated in an earthen vessel over living waters.
6 Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
But the other living one, with the cedar wood, and the scarlet, and the hyssop, he shall dip in the blood of the immolated sparrow.
7 Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
And he shall sprinkle him who is to be cleansed seven times, so that he may be purified justly. And he shall release the living sparrow, so that it may fly away into the field.
8 “Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
And when the man will have washed his clothes, he shall shave all the hair from his body, and he shall be washed with water. And having been purified, he shall enter into the camp, only to this extent: that he may remain outside his own tent for seven days.
9 Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
And on the seventh day he shall shave the hair of his head, and his beard, and his eyebrows, as well as the hair of his entire body. And having washed his clothes again, and his body,
10 “Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
on the eighth day, he shall take two immaculate lambs, and a one-year-old female sheep without blemish, and three tenths of fine wheat flour, which has been sprinkled with oil, as a sacrifice, and separately, one twelfth hin of oil.
11 Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
And when the priest purifying the man has presented him and all these things in the sight of the Lord at the door of the tabernacle of the testimony,
12 “Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
he shall take a lamb and offer it for transgression, with the twelfth hin of oil. And having offered all these before the Lord,
13 Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
he shall immolate the lamb, where the victim for sin is usually immolated with the holocaust, that is, in the holy place. For just as with the one for sin, so also the victim for transgression belongs to the priest. It is the Holy of holies.
14 Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And taking some of the blood of the victim, which was immolated for transgression, the priest shall place it upon the tip of the right ear of him who is being cleansed, and upon the thumb of his right hand, and likewise the foot.
15 Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
And he shall send some of the twelfth hin of oil into his own left hand,
16 na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
and he shall dip his right finger in it, and he shall sprinkle it in the sight of the Lord seven times.
17 Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
But the oil which remains in his left hand, he shall pour over the tip of the right ear of him who is being cleansed, and upon the thumb of his right hand as well as the foot, and upon the blood which was shed for transgression,
18 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
and upon his head.
19 “Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
And he shall pray for him in the sight of the Lord, and he shall accomplish the sacrifice on behalf of sin. Then he shall immolate the holocaust,
20 na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
and place it upon the altar with its libations, and the man will be duly cleansed.
21 “Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
But if he is poor, and his hand is not able to find what has been said, he shall take a lamb as an offering for transgression, so that the priest may pray for him, and a tenth part of fine wheat flour sprinkled with oil, as a sacrifice, and a twelfth hin of oil,
22 na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
and two turtledoves or two young pigeons, of which one may be for sin, and the other as a holocaust.
23 “Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
And he shall offer them on the eighth day of his purification to the priest at the door of the tabernacle of the testimony in the sight of the Lord.
24 Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And he, receiving the lamb for transgression, and the twelfth hin of oil, shall lift them up together.
25 Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And when the lamb has been immolated, he shall place some of its blood upon the tip of the right ear of him who is being cleansed, and upon the thumb of his right hand, as well as the foot.
26 Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
Yet truly, he shall send part of the oil into his own left hand,
27 na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
and dipping the finger of his right hand in it, he shall sprinkle it seven times before the Lord.
28 Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And he shall touch the tip of the right ear of him who is being cleansed, and the thumb of his right hand, as well as the foot, in the place of the blood which was shed for transgression.
29 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
But the remaining part of the oil which is in his left hand, he shall send upon the head of the one being purified, to appease the Lord on his behalf.
30 Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
And he shall offer a turtledove or a young pigeon,
31 mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
one for transgression, and the other as a holocaust, with their libations.
32 Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
This is the sacrifice of a leper, who is not able to obtain all of the things concerning his cleansing.
33 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
And the Lord spoke to Moses and Aaron, saying:
34 “Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
When you will have entered into the land of Canaan, which I will give to you as a possession, if there is the mark of leprosy in a building,
35 ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
he whose house it is shall go and report to the priest, saying: “It seems to me that the mark of leprosy is in my house.”
36 Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
And he shall instruct them to carry all things out of the house, before he would enter it and see whether it is leprosy, lest all that is in the house become unclean. And after this, he shall enter to examine the leprosy of the house.
37 Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
And when he will have seen in its walls something like little hollows, deformed with paleness or redness, and lower than the remaining surface,
38 kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
he shall exit by the door of the house, and immediately close it up for seven days.
39 Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
And returning on the seventh day, he shall examine it. If he finds that the leprosy has spread,
40 ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
he shall order the stones in which the leprosy is, to be dug out and cast outside the city in an unclean place,
41 Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
and that the house be scraped on the inside all around, and that the dust of the scrapings be scattered outside the city in an unclean place,
42 Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
and that other stones be put back, in place of those which had been taken away, and that the house be plastered with other mortar.
43 “Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
But if, after the stones have been dug out, and the dust wiped away, and it is plastered with other clay,
44 kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
the priest, upon entering, will have seen that the leprosy has returned, and that the walls are sprinkled with spots, then it is a persistent leprosy and the house is unclean.
45 Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
And so they shall promptly destroy it, and shall cast its stones and timber, and also all the dust, outside the town in an unclean place.
46 “Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
Whoever enters into the house when it is closed up shall be unclean until evening.
47 Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
And whoever will have slept in it, or eaten anything, shall wash his clothes.
48 “Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
But if the priest, upon entering, will have seen that the leprosy has not spread in the house, after it had been newly plastered, he shall purify it, restoring it to health.
49 Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
And for its purification, he shall take two sparrows, and cedar wood, and vermillion, as well as hyssop,
50 Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
and, having immolated one sparrow in an earthen vessel over living waters,
51 Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
he shall take the cedar wood, and the hyssop, and the scarlet, and the living sparrow, and he shall dip all these in the blood of the immolated sparrow, and also in the living water, and he shall sprinkle the house seven times.
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
And he shall purify it as much with the blood of the sparrow as with the living water, and with the living sparrow, and the cedar wood, and the hyssop, and the vermillion.
53 Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
And when he has released the sparrow to fly freely away into the field, he shall pray for the house, and it shall be justly cleansed.
54 Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
This is the law of every kind of leprosy and plague:
55 upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
of the leprosy of garments and houses,
56 kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
of scars and erupting pustules, of a shining spot, when the appearance is also variegated,
57 kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.
so that it can be known at what time a thing is clean or unclean.

< Mambo ya Walawi 14 >