< Mambo ya Walawi 14 >

1 Bwana akamwambia Mose,
And the Lord said to Moses,
2 “Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
This is the law of the leper on the day when he is made clean: he is to be taken to the priest;
3 Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
And the priest is to go outside the tent-circle; and if, after looking, the priest sees that the mark of the disease has gone from him,
4 kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
Then the priest is to give orders to take, for him who is to be made clean, two living clean birds and some cedar wood and red thread and hyssop.
5 Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
And the priest will give orders for one of the birds to be put to death in a vessel made of earth, over flowing water.
6 Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
And he will take the living bird and the wood and the red thread and the hyssop and put them in the blood of the bird which was put to death over flowing water.
7 Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
And shaking it seven times over the man who is to be made clean, he will say that he is clean and will let the living bird go free into the open country.
8 “Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
And he who is to be made clean will have his clothing washed and his hair cut and have a bath, and he will be clean. And after that he will come back to the tent-circle; but he is to keep outside his tent for seven days.
9 Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
And on the seventh day he is to have all the hair cut off his head and his chin and over his eyes — all his hair is to be cut off — and he will have his clothing washed and his body bathed in water and he will be clean.
10 “Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
And on the eighth day let him take two male lambs, without any marks on them, and one female lamb of the first year, without a mark, and three tenth parts of an ephah of the best meal, mixed with oil, and one log of oil.
11 Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
And the priest who is making him clean will put the man who is being made clean, together with these things, before the door of the Tent of meeting.
12 “Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And the priest is to take one of the male lambs and give it as an offering for wrongdoing, and the log of oil, waving them for a wave offering before the Lord;
13 Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
And he is to put the male lamb to death in the place where they put to death the sin-offering and the burned offering, in the holy place; for as the sin-offering is the property of the priest, so is the offering for wrongdoing: it is most holy.
14 Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And let the priest take some of the blood of the offering for wrongdoing and put it on the point of the right ear of him who is to be made clean, and on the thumb of his right hand and on the great toe of his right foot;
15 Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
And take some of the oil and put it in the hollow of his left hand;
16 na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
And let the priest put his right finger in the oil which is in his left hand, shaking it out with his finger seven times before the Lord;
17 Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
And of the rest of the oil which is in his hand, the priest will put some on the point of the right ear of the man who is to be made clean, and on the thumb of his right hand and on the great toe of his right foot, over the blood of the offering for wrongdoing;
18 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
And the rest of the oil in the priest's hand he will put on the head of him who is to be made clean; and so the priest will make him free from sin before the Lord.
19 “Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
And the priest will give the sin-offering, and take away the sin of him who is to be made clean from his unclean condition; and after that he will put the burned offering to death.
20 na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
And the priest is to have the burned offering and the meal offering burned on the altar; and the priest will take away his sin and he will be clean.
21 “Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
And if he is poor and not able to get so much, then he may take one male lamb as an offering for wrongdoing, to be waved to take away his sin, and one tenth part of an ephah of the best meal mixed with oil for a meal offering, and a log of oil;
22 na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
And two doves or two young pigeons, such as he is able to get; and one will be for a sin-offering and the other for a burned offering.
23 “Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
And on the eighth day he will take them to the priest, to the door of the Tent of meeting before the Lord, so that he may be made clean.
24 Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
And the priest will take the lamb of the offering for wrongdoing and the oil, waving them for a wave offering before the Lord;
25 Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And he will put to death the lamb of the offering for wrongdoing and the priest will take some of the blood of the offering for wrongdoing and put it on the point of the right ear of him who is to be made clean, and on the thumb of his right hand and on the great toe of his right foot;
26 Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
And the priest will put out some of the oil in the hollow of his left hand,
27 na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
Shaking out drops of oil with his right finger before the Lord seven times:
28 Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
And the priest will put some of the oil which is in his hand on the point of the ear of the man who is to be made clean and on the thumb of his right hand and on the great toe of his right foot, on the place where the blood of the offering for wrongdoing was put;
29 Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
And the rest of the oil which is in the priest's hand he will put on the head of him who is to be made clean, to take away his sin before the Lord.
30 Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
And he will make an offering of one of the doves or the young pigeons, such as he is able to get;
31 mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
And of these, he will give one for a sin-offering and one for a burned offering, with the meal offering; and the priest will take away the sin of him who is to be made clean before the Lord.
32 Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
This is the law for the man who has the disease of the leper on him, and who is not able to get that which is necessary for making himself clean.
33 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
And the Lord said to Moses and Aaron,
34 “Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
When you have come into the land of Canaan which I will give you for your heritage, if I put the leper's disease on a house in the land of your heritage,
35 ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
Then let the owner of the house come and say to the priest, It seems to me that there is a sort of leper's disease in the house.
36 Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
And the priest will give orders for everything to be taken out of the house, before he goes in to see the disease, so that the things in the house may not become unclean; and then the priest is to go in to see the house;
37 Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
And if he sees that the walls of the house are marked with hollows of green and red, and if it seems to go deeper than the face of the wall;
38 kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
Then the priest will go out of the door of the house, and keep the house shut up for seven days:
39 Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
And the priest is to come again on the seventh day and have a look and see if the marks on the walls of the house are increased in size;
40 ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
Then the priest will give orders to them to take out the stones in which the disease is seen, and put them out into an unclean place outside the town:
41 Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
And he will have the house rubbed all over inside, and the paste which is rubbed off will be put out into an unclean place outside the town:
42 Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
And they will take other stones and put them in place of those stones, and he will take other paste and put it on the walls of the house.
43 “Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
And if the disease comes out again in the house after he has taken out the stones and after the walls have been rubbed and the new paste put on,
44 kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
Then the priest will come and see it; and if the disease in the house is increased in size, it is the leper's disease working out in the house: it is unclean.
45 Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
And the house will have to be pulled down, the stones of it and the wood and the paste; and everything is to be taken out to an unclean place outside the town.
46 “Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
And, in addition, anyone who goes into the house at any time, while it is shut up, will be unclean till evening.
47 Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
And anyone who has been sleeping in the house will have to have his clothing washed; and anyone who takes food in that house will have to have his clothing washed.
48 “Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
And if the priest comes in, and sees that the disease is not increased after the new paste has been put on the house, then the priest will say that the house is clean, because the disease is gone.
49 Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
And in order to make the house clean, let him take two birds and cedar-wood and red thread and hyssop;
50 Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
And put one of the birds to death in a vessel of earth over flowing water;
51 Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
And take the cedar-wood and the hyssop and the red thread and the living bird and put them in the blood of the dead bird and in the flowing water, shaking it over the house seven times.
52 Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
And he will make the house clean with the blood of the bird and the flowing water and with the living bird and with the cedar-wood and the hyssop and the red thread.
53 Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
But he will let the living bird go out of the town into the open country; so he will take away sin from the house and it will be clean.
54 Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
This is the law for all signs of the leper's disease and for skin diseases;
55 upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
And for signs of disease in clothing, or in a house;
56 kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
And for a growth or a bad place or a bright mark on the skin;
57 kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.
To make clear when it is unclean and when it is clean: this is the law about the disease of the leper.

< Mambo ya Walawi 14 >