< Mambo ya Walawi 13 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Jošte reèe Gospod Mojsiju i Aronu govoreæi:
2 “Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au alama nyeupe juu ya ngozi yake ambayo yaweza kuwa ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani ama kwa wanawe, kuhani mmojawapo.
Èovjek u koga bi na koži tijela njegova bio otok ili krasta ili bubuljica, i bilo bi na koži tijela njegova nalik na gubu, neka se dovede k Aronu svešteniku ili ka kojemu sinu njegovu svešteniku.
3 Kuhani atachunguza hicho kidonda kilichopo juu ya ngozi yake, na kama nywele za mahali palipo na kidonda zimebadilika kuwa nyeupe, na ikiwa kidonda kimeingia ndani ya ngozi, basi ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma. Kuhani atakapomchunguza, atamtangaza mtu huyo kuwa ni najisi kwa kawaida ya ibada.
I neka sveštenik vidi boljeticu na koži tijela njegova; ako dlaka na boljetici bude pobijeljela i boljetica bude na oèi niža od ostale kože tijela njegova, onda je guba; pa kad je vidi sveštenik proglasiæe ga da je neèist.
4 Kama alama juu ya ngozi yake ni nyeupe, lakini haionekani kuwa imeingia ndani zaidi ya ngozi, na nywele kwenye alama hiyo hazijageuka kuwa nyeupe, kuhani atamtenga mtu huyo mahali pa pekee kwa siku saba.
Ako li bude bijela bubuljica na koži tijela njegova i ne bude na oèi niža od ostale kože niti dlaka na njoj pobijeljela, onda neka zatvori sveštenik za sedam dana èovjeka sa takom boljeticom.
5 Siku ya saba, kuhani atamchunguza, na kama hakuona badiliko kwenye kile kidonda na hakijaenea juu ya ngozi, atamtenga kwa siku nyingine saba.
A sedmoga dana neka vidi sveštenik; ako opazi da je boljetica ostala kako je bila i nije se dalje razišla po koži, neka ga zatvori sveštenik opet za sedam dana.
6 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama kidonda kimepungua na hakijaenea juu ya ngozi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa ni safi, ni upele tu. Ni lazima mtu huyo afue mavazi yake, naye atakuwa safi.
I neka ga sveštenik opet vidi sedmoga dana, pa ako opazi da se boljetica smanjala i nije se dalje razišla po koži, proglasiæe ga sveštenik da je èist; krasta je; i on neka opere haljine svoje i biæe èist.
7 Lakini ikiwa ule upele utaenea juu ya ngozi yake baada ya yeye kujionyesha kwa kuhani na kutangazwa kuwa safi, ni lazima aende tena kwa kuhani.
Ako li se dalje raširi krasta po koži njegovoj, pošto ga sveštenik vidi i proglasi da je èist, nanovo neka se pokaže svešteniku;
8 Kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, atamtangaza kuwa najisi, kwani ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma.
Ako vidi sveštenik da se krasta raširila po koži njegovoj, proglasiæe sveštenik da je neèist; guba je.
9 “Wakati mtu yeyote ana ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa kuhani.
Kad je guba na èovjeku, neka ga dovedu k svešteniku.
10 Kuhani atamchunguza na kama kuna uvimbe mweupe juu ya ngozi ambao umefanya nywele kuwa nyeupe, na kama kuna nyama mbichi ndani ya uvimbe,
I sveštenik neka ga vidi; ako bude bijel otok na koži i dlaka bude pobijeljela, ako bi i zdravo meso bilo na otoku,
11 ni ugonjwa sugu wa ngozi, na kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga tena kwa sababu ni najisi tayari.
Guba je zastarjela na koži tijela njegova; zato æe ga sveštenik proglasiti da je neèist, i neæe ga zatvoriti, jer je neèist.
12 “Ikiwa ugonjwa utakuwa umeenea kwenye ngozi yake yote kwa kadiri kuhani atakavyoweza kuona, kwamba umeenea kwenye ngozi yote ya huyo mgonjwa kutoka kichwani mpaka wayo,
Ako li se guba izaspe po koži i pokriju svu kožu èovjeku od glave do pete, gdje bi god sveštenik oèima pogledao,
13 kuhani atamchunguza, na kama ugonjwa umeenea mwili mzima, atamtangaza huyo mtu kuwa safi. Kwa kuwa mwili wote umekuwa mweupe, yeye ni safi.
Kad sveštenik vidi da je guba pokrila svu kožu na njemu, proglasiæe da je èovjek èist, jer je sve pobijeljelo, pa je èist.
14 Lakini itokeapo nyama mbichi kwenye ngozi yake, atakuwa najisi.
Ali ako se pokaže na njemu divlje meso, biæe neèist.
15 Kuhani atakapoiona hiyo nyama mbichi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hiyo nyama mbichi ni najisi, ana ugonjwa wa kuambukiza.
Pa kad sveštenik vidi divlje meso, proglasiæe ga da je neèist; ono je divlje meso neèisto, guba je.
16 Hiyo nyama mbichi ikigeuka na kuwa nyeupe, ni lazima amwendee kuhani.
A kad bi se divlje meso promijenilo i pobijeljelo, neka doðe k svešteniku.
17 Kuhani atamchunguza, na kama vidonda vimekuwa vyeupe, kuhani atamtangaza mgonjwa huyo kuwa safi; kisha atakuwa safi.
I kad vidi sveštenik da je boljetica pobijeljela, sveštenik æe proglasiti da je èist; èist je.
18 “Wakati mtu ana jipu juu ya ngozi yake nalo likapona,
Kad u koga na koži bude èir, pa proðe,
19 napo mahali palipokuwa na jipu pakatokea uvimbe mweupe, au alama yenye wekundu na weupe, ni lazima akajionyeshe kwa kuhani.
A poslije na mjestu gdje je bio èir izaðe otok bijel ili bubuljica bijela i crvenkasta, neka se pokaže svešteniku.
20 Kuhani atapachunguza, na kama uvimbe umezama ndani ya ngozi, na nywele zimegeuka kuwa nyeupe, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza uliojitokeza pale jipu lilipokuwa.
Ako sveštenik vidi da je na oèi niža od ostale kože i dlaka na njoj pobijeljela, proglasiæe ga sveštenik da je neèist, guba je, izašla je iz èira.
21 Lakini ikiwa wakati kuhani anapopachunguza pakawa hapana nywele nyeupe ndani yake, wala hakuna shimo bali pamepungua, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Ako li sveštenik gledajuæi vidi da nije dlaka na njoj pobijeljela niti je niža od kože, nego se smanjala, onda æe ga zatvoriti sveštenik za sedam dana.
22 Kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Ako se raširi po koži, onda æe ga sveštenik proglasiti da je neèist; bolest je.
23 Lakini ikiwa ile alama haijabadilika wala kuenea, ni kovu tu kutokana na jipu, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Ako li ostane na svom mjestu bubuljica i ne raširi se, požiljak je od èira; zato æe ga sveštenik proglasiti da je èist.
24 “Wakati mtu ameungua kwenye ngozi yake, pakatokea alama yenye wekundu na weupe, au alama nyeupe ikaonekana penye nyama mbichi pale palipoungua,
Ako se ko po koži ožeže ognjem, pa pošto se zalijeèi ostane bubuljica bijela i crvenkasta ili samo bijela,
25 kuhani ataichunguza ile alama, na kama nywele zilizoko juu yake zimegeuka kuwa nyeupe, napo pametokea shimo, basi huo ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza ambao umetokea juu ya jeraha la moto. Kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Neka ga vidi sveštenik; ako dlaka na bubuljici bude pobijeljela i ako na oèi bude niža nego koža, guba je, izašla je iz ožegline; zato æe ga sveštenik proglasiti da je neèist; guba je.
26 Lakini kama kuhani akichunguza na kuona kwamba hakuna nywele nyeupe kwenye alama ile, wala hakuna shimo napo pameanza kupungua, basi kuhani atamtenga kwa siku saba.
Ako li sveštenik vidi da na bubuljici nema bijele dlake niti je niža od kože, nego se smanjala, zatvoriæe ga za sedam dana.
27 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Pa æe je sedmoga dana pogledati sveštenik; ako se bude raširila po koži, tada æe ga sveštenik proglasiti da je neèist; guba je.
28 Lakini, kama alama ile haikubadilika na wala haijaenea kwenye ngozi, napo pamepungua, ni uvimbe kutokana na jeraha la moto, na kuhani atamtangaza kuwa safi; ni kovu tu kutokana na kuungua.
Ako li bubuljica bude ostala na svom mjestu, i ne bude se raširila po koži, nego se smanjala, onda je rana od toga što se ožegao; zato æe ga sveštenik proglasiti da je èist, jer je požiljak od ožegline.
29 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana kidonda juu ya kichwa au juu ya kidevu,
Ako u èovjeka ili u žene bude boljetica na glavi ili na bradi,
30 kuhani atakichunguza kile kidonda, na kama ataona kuwa kimeingia ndani, na nywele zilizoko juu yake ni njano na nyembamba, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi, kwani ni upele; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza wa kichwa au kidevu.
Sveštenik neka vidi boljeticu; ako na oèi bude niža od ostale kože i na njojzi dlaka žuækasta i tanka, sveštenik æe proglasiti da je neèist; ospa je, guba na glavi ili na bradi;
31 Lakini kama kuhani akichunguza aina hii ya kidonda, kionekane kuwa hakina shimo na hakuna nywele nyeusi juu yake, basi atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
A kad sveštenik vidi boljeticu, i opazi da na oèi nije niža od ostale kože i da nema na njoj crne dlake, tada æe zatvoriti sveštenik za sedam dana onoga na kom je ospa.
32 Siku ya saba kuhani atachunguza kidonda kile, na kama upele haujaenea, na hakuna nywele za manjano juu yake, wala hakuna shimo lolote,
Pa kad sveštenik sedmi dan vidi a ospa se nije dalje razišla niti dlaka na njoj požutjela, niti je na oèi ospa niža od kože,
33 mtu huyo ni lazima anyolewe, isipokuwa mahali palipo na ugonjwa, naye kuhani atamtenga kwa siku nyingine saba.
Tada neka se obrije, ali ospu da ne obrije, i sveštenik neka zatvori još za sedam dana onoga na kom je ospa.
34 Siku ya saba kuhani atachunguza tena ule upele; ikiwa haujaenea kwenye ngozi na hakuna shimo mahali pale, kuhani atamtangaza kuwa safi. Lazima afue nguo zake, naye atakuwa safi.
I sedmoga dana neka sveštenik opet vidi ospu; ako opazi da se ospa nije dalje razišla po koži niti je na oèi niža od ostale kože, tada æe ga proglasiti sveštenik da je èist, pa neka opere haljine svoje, i biæe èist.
35 Lakini ikiwa upele utaenea juu ya ngozi baada ya kutangazwa kuwa safi,
Ako li se raširi ospa po koži, pošto bude proglašen da je èist,
36 kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, kuhani hana haja ya kutazama kama kuna nywele za manjano, mtu huyo ni najisi.
Tada neka ga vidi sveštenik; ako se bude raširila ospa po koži, neka više ne gleda sveštenik ima li žutijeh dlaka; neèist je.
37 Hata hivyo, katika uchunguzi wake akiona hapajabadilika, na nywele nyeusi zimeota juu yake, upele umepona. Yeye si najisi, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Ako li opazi da je ospa ostala gdje je bila i da je crna dlaka izrasla po njoj, zalijeèila se ospa, èist je, i sveštenik æe proglasiti da je èist.
38 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana alama nyeupe juu ya ngozi yake,
Kad u èovjeka ili u žene budu bubuljice po koži tijela njihova, bubuljice bijele,
39 kuhani atamchunguza, na kama alama hizo zina weupe uliofifia, ni vipele visivyo na madhara vilivyojitokeza kwenye ngozi; mtu huyo ni safi.
Sveštenik neka vidi; ako na koži tijela njihova budu bijele bubuljice male, bijela je ospa izašla po koži, èist je.
40 “Wakati mwanaume hana nywele naye ana upaa, yeye ni safi.
Kome opadne kosa s glave, æelav je, èist je.
41 Ikiwa hana nywele kwenye ngozi ya kichwa chake, na ana upaa tangu kwenye paji, ni safi.
Ako mu sprijeda opadne kosa s glave, pola je æelav, i èist je.
42 Lakini kama ana kidonda chenye wekundu na weupe kwenye kichwa chake chenye upaa, au kwenye paji la uso, ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza unaojitokeza kichwani au kwenye paji lake la uso.
Kad na glavi sasvijem æelavoj ili pola æelavoj bude bijela i crvenkasta boljetica, guba je, izašla na glavi svoj æelavoj ili pola æelavoj.
43 Kuhani atamchunguza, na kama kidonda kilichovimba juu ya kichwa chake au kwenye paji la uso ni chekundu au cheupe kama ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza,
I neka ga vidi sveštenik; ako opazi da je bijel i crvenkast otok na glavi svoj æelavoj ili pola æelavoj nalik na gubu po koži ostaloga tijela,
44 mtu huyo ni mgonjwa, na ni najisi. Kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya kidonda kwenye kichwa chake.
Èovjek je gubav, neèist je, i sveštenik æe ga proglasiti da je neèist; guba mu je na glavi.
45 “Mtu mwenye ugonjwa kama huo wa kuambukiza ni lazima avae nguo zilizoraruka, awachilie nywele zake bila kuzichana, afunike sehemu ya chini ya uso wake, na apige kelele, ‘Najisi! Najisi!’
A gubavac na kom je ta bolest, neka ide u haljinama razdrtijem i gologlav, i usta neka zastre, i neka vièe: neèist, neèist.
46 Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo wa kuambukiza atabaki kuwa najisi. Ni lazima aishi peke yake; ni lazima aishi nje ya kambi.
Dokle je god bolest na njemu, neka bude neèist; neèist je, neka živi sam, iza okola neka mu bude stan.
47 “Kama vazi lolote lina maambukizo ya upele: likiwa ni vazi la sufu au kitani,
I ako na haljini bude guba, na haljini vunenoj ili lanenoj,
48 lolote lililofumwa au kusokotwa likiwa la kitani au la sufu, ngozi yoyote au chochote kilichotengenezwa kwa ngozi,
Ili na osnovi ili na pouèici od lana ili od vune, ili na koži, ili na èem god od kože,
49 tena kama maambukizo kwenye vazi, au ngozi, au lililofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi, ni rangi ya kijani au nyekundu, huo ni upele unaoenea na ni lazima kuhani aonyeshwe.
I ako boljetica bude zelenkasta ili crvenkasta na haljini ili na koži ili na osnovi ili na pouèici ili na èem god od kože, guba je, i neka se pokaže svešteniku.
50 Kuhani atachunguza upele huo na kukitenga kifaa hicho kwa siku saba.
I kad vidi sveštenik bolest, neka zatvori za sedam dana stvar na kojoj je guba.
51 Siku ya saba atakichunguza, na kama upele umeenea kwenye nguo, au kifaa kilichofumwa au kusokotwa, au ngozi, kwa vyovyote vile itumikavyo, ni upele uangamizao, kifaa hicho ni najisi.
I sedmoga dana ako vidi da se dalje razišla bolest po haljini ili po osnovi ili po pouèici ili po koži ili po èemu god od kože, ljuta je guba bolest ona, stvar je neèista.
52 Ni lazima aichome hiyo nguo, ikiwa ni ya sufu ama kitani iliyofumwa ama kusokotwa, ama chombo chochote cha ngozi chenye maambukizo, kwa kuwa ni upele unaoangamiza; chombo chote ni lazima kichomwe moto.
Zato neka spali onu haljinu ili osnovu ili pouèicu od vune ili od lana, ili što god bude od kože, na èem bude bolest; jer je ljuta guba, ognjem neka se spali.
53 “Lakini wakati kuhani atakapokichunguza na kuona kuwa ule upele haujaenea kwenye nguo iliyofumwa au kusokotwa, au vifaa vya ngozi,
Ako li opazi sveštenik da se bolest nije razišla po haljini ili po osnovi ili pouèici, ili po èemu god od kože,
54 ataagiza kwamba kifaa chenye maambukizo kisafishwe. Kisha atakitenga kwa siku saba.
Tada neka zapovjedi sveštenik da se opere ono na èem je bolest, pa onda neka zatvori opet za sedam dana.
55 Baada ya kifaa chenye maambukizo kusafishwa, kuhani atakichunguza, na kama upele haujaonyesha badiliko lolote, hata kama haujaenea, ni najisi. Kichome kwa moto, iwe upele umeenea upande mmoja au mwingine.
Pa neka vidi sveštenik pošto se opere stvar na kojoj je bolest, i ako opazi da bolest nije promijenila boje svoje, ako se i ne bude dalje razišla, stvar je neèista, spali je ognjem; jer je ljuta guba na gornjoj ili na donjoj strani.
56 Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kuoshwa, basi atararua sehemu iliyo ambukizwa ya nguo au ngozi au kifaa kilichofumwa au kusokotwa.
Ako li vidi sveštenik da se mjesto smanjalo pošto je oprano, onda neka ga otkine od haljine ili od kože ili od osnove ili od pouèice.
57 Lakini kama ikijitokeza tena kwenye nguo au kitu kilichofumwa au kusokotwa, ama kifaa cha ngozi, kwamba ule upele unaenea, chochote chenye upele ni lazima kichomwe kwa moto.
Ako li se opet pokaže na haljini ili na osnovi ili na pouèici ili na èem god od kože, guba je koja se širi, ognjem spali ono na èem bude.
58 Nguo, au kitu kilichofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi ambacho kimesafishwa na kuondolewa upele, ni lazima kioshwe tena, nacho kitakuwa safi.”
A haljinu ili osnovu ili pouèicu ili što mu drago od kože, kad opereš, pa otide s njega ta bolest, operi još jednom, i biæe èisto.
59 Haya ni masharti kuhusu maambukizo ya upele kwenye mavazi ya sufu au kitani, yaliyofumwa ama kusokotwa, ama kifaa chochote cha ngozi, kwa ajili ya kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Ovo je zakon za gubu na haljini vunenoj ili lanenoj, ili na osnovi ili na pouèici, ili na èem god od kože, kako se može znati je li što èisto ili neèisto.