< Mambo ya Walawi 13 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Le Seigneur parla encore à Moïse et à Aaron, disant:
2 “Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au alama nyeupe juu ya ngozi yake ambayo yaweza kuwa ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani ama kwa wanawe, kuhani mmojawapo.
L’homme dans la peau ou dans la chair duquel se sera formée une diversité de couleur, soit une pustule, ou quelque chose de luisant, c’est-à-dire une plaie de lèpre, sera amené à Aaron, le prêtre, ou à un de ses fils, quel qu’il soit;
3 Kuhani atachunguza hicho kidonda kilichopo juu ya ngozi yake, na kama nywele za mahali palipo na kidonda zimebadilika kuwa nyeupe, na ikiwa kidonda kimeingia ndani ya ngozi, basi ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma. Kuhani atakapomchunguza, atamtangaza mtu huyo kuwa ni najisi kwa kawaida ya ibada.
Qui, lorsqu’il verra la lèpre dans la peau, les poils devenus d’une couleur blanche et l’endroit même où paraît la lèpre, plus enfoncé que la peau et le reste de la chair, déclarera que c’est une plaie de lèpre, et d’après sa décision l’homme sera séparé.
4 Kama alama juu ya ngozi yake ni nyeupe, lakini haionekani kuwa imeingia ndani zaidi ya ngozi, na nywele kwenye alama hiyo hazijageuka kuwa nyeupe, kuhani atamtenga mtu huyo mahali pa pekee kwa siku saba.
Si au contraire une blancheur luisante est à la peau, et qu’elle ne soit pas plus enfoncée que le reste de la chair, et que les poils soient de leur couleur primitive, le prêtre le renfermera pendant sept jours,
5 Siku ya saba, kuhani atamchunguza, na kama hakuona badiliko kwenye kile kidonda na hakijaenea juu ya ngozi, atamtenga kwa siku nyingine saba.
Et il le considérera au septième jour; et si la lèpre n’a pas crû davantage, et n’a point dépassé dans la peau ses premières limites, il le renfermera pendant sept autres jours.
6 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama kidonda kimepungua na hakijaenea juu ya ngozi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa ni safi, ni upele tu. Ni lazima mtu huyo afue mavazi yake, naye atakuwa safi.
Et au septième jour il le regardera attentivement; si la lèpre est plus obscure, et qu’elle n’ait pas crû dans la peau, il le déclarera pur, parce que c’est une éruption; et l’homme lavera ses vêtements, et il sera pur.
7 Lakini ikiwa ule upele utaenea juu ya ngozi yake baada ya yeye kujionyesha kwa kuhani na kutangazwa kuwa safi, ni lazima aende tena kwa kuhani.
Que si après qu’il aura été vu par le prêtre, et déclaré pur, la lèpre croit de nouveau, il sera amené vers lui,
8 Kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, atamtangaza kuwa najisi, kwani ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma.
Et il sera condamné pour cause d’impureté.
9 “Wakati mtu yeyote ana ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa kuhani.
Si une plaie de lèpre se trouve dans un homme, il sera amené au prêtre,
10 Kuhani atamchunguza na kama kuna uvimbe mweupe juu ya ngozi ambao umefanya nywele kuwa nyeupe, na kama kuna nyama mbichi ndani ya uvimbe,
Et le prêtre le verra. Or, lorsqu’il y aura une couleur blanche sur la peau, et qu’elle aura changé l’aspect des cheveux, et que la chair vive elle-même aura aussi paru,
11 ni ugonjwa sugu wa ngozi, na kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga tena kwa sababu ni najisi tayari.
La lèpre sera jugée très ancienne et enracinée dans la peau. C’est pourquoi le prêtre le déclarera souillé, et il ne le renfermera point, parce qu’il a une impureté très visible.
12 “Ikiwa ugonjwa utakuwa umeenea kwenye ngozi yake yote kwa kadiri kuhani atakavyoweza kuona, kwamba umeenea kwenye ngozi yote ya huyo mgonjwa kutoka kichwani mpaka wayo,
Mais si la lèpre s’épanouit, courant sur la peau, et qu’elle couvre toute la peau depuis la tête jusqu’aux pieds, dans tout ce qui tombe sous la vue,
13 kuhani atamchunguza, na kama ugonjwa umeenea mwili mzima, atamtangaza huyo mtu kuwa safi. Kwa kuwa mwili wote umekuwa mweupe, yeye ni safi.
Le prêtre le considérera et il jugera qu’il est attaqué d’une lèpre très pure, parce qu’elle est toute devenue d’une couleur blanche, et à cause de cela, l’homme sera pur.
14 Lakini itokeapo nyama mbichi kwenye ngozi yake, atakuwa najisi.
Mais quand la chair vive aura paru en lui,
15 Kuhani atakapoiona hiyo nyama mbichi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hiyo nyama mbichi ni najisi, ana ugonjwa wa kuambukiza.
Alors, au jugement du prêtre il sera souillé, et il sera compté parmi les impurs; car la chair vive, si elle est entachée de lèpre, est impure.
16 Hiyo nyama mbichi ikigeuka na kuwa nyeupe, ni lazima amwendee kuhani.
Que si de nouveau elle est devenue d’une couleur blanche, et qu’elle couvre l’homme tout entier,
17 Kuhani atamchunguza, na kama vidonda vimekuwa vyeupe, kuhani atamtangaza mgonjwa huyo kuwa safi; kisha atakuwa safi.
Le prêtre le considérera et déclarera qu’il est pur.
18 “Wakati mtu ana jipu juu ya ngozi yake nalo likapona,
Mais si c’est une chair et une peau sur laquelle un ulcère s’est formé et a été guéri,
19 napo mahali palipokuwa na jipu pakatokea uvimbe mweupe, au alama yenye wekundu na weupe, ni lazima akajionyeshe kwa kuhani.
Et qu’à l’endroit de l’ulcère il paraisse une cicatrice blanche, ou roussâtre, l’homme sera amené au prêtre,
20 Kuhani atapachunguza, na kama uvimbe umezama ndani ya ngozi, na nywele zimegeuka kuwa nyeupe, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza uliojitokeza pale jipu lilipokuwa.
Qui, lorsqu’il verra que l’endroit de la lèpre est plus enfoncé que le reste de la chair, et que les poils sont devenus d’une couleur blanche, il le déclarera souillé; car c’est une plaie de lèpre qui s’est formée dans l’ulcère.
21 Lakini ikiwa wakati kuhani anapopachunguza pakawa hapana nywele nyeupe ndani yake, wala hakuna shimo bali pamepungua, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Que si le poil est de sa couleur primitive, et si la cicatrice est un peu obscure, et qu’elle ne soit pas plus enfoncée que la chair voisine, il le renfermera pendant sept jours.
22 Kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Et si toutefois elle croît, il décidera qu’il a la lèpre.
23 Lakini ikiwa ile alama haijabadilika wala kuenea, ni kovu tu kutokana na jipu, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Si au contraire elle s’est arrêtée à sa place, c’est la cicatrice de l’ulcère, et l’homme sera pur.
24 “Wakati mtu ameungua kwenye ngozi yake, pakatokea alama yenye wekundu na weupe, au alama nyeupe ikaonekana penye nyama mbichi pale palipoungua,
Mais si c’est une chair et une peau que le feu aura brûlée, et qui, étant guérie, aura une cicatrice blanche ou rousse,
25 kuhani ataichunguza ile alama, na kama nywele zilizoko juu yake zimegeuka kuwa nyeupe, napo pametokea shimo, basi huo ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza ambao umetokea juu ya jeraha la moto. Kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Le prêtre la considérera, et voilà qu’elle est devenue d’une couleur blanche, et que sa place est plus enfoncée que le reste de la peau: il le déclarera souillé, parce que c’est une plaie de lèpre qui s’est formée dans la cicatrice.
26 Lakini kama kuhani akichunguza na kuona kwamba hakuna nywele nyeupe kwenye alama ile, wala hakuna shimo napo pameanza kupungua, basi kuhani atamtenga kwa siku saba.
Que si la couleur des poils n’est point changée, et si la plaie n’est pas plus enfoncée que le reste de la chair, et que la lèpre elle-même paraisse un peu obscure, il le renfermera pendant sept jours,
27 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Et au septième jour, il le regardera attentivement: si la lèpre a crû sur la peau, il le déclarera souillé.
28 Lakini, kama alama ile haikubadilika na wala haijaenea kwenye ngozi, napo pamepungua, ni uvimbe kutokana na jeraha la moto, na kuhani atamtangaza kuwa safi; ni kovu tu kutokana na kuungua.
Si au contraire la blancheur s’arrête à sa place, n’étant pas assez claire, c’est la plaie de la brûlure; et, à cause de cela, il sera déclaré pur, parce que c’est la cicatrice de la brûlure.
29 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana kidonda juu ya kichwa au juu ya kidevu,
Un homme ou une femme, si la lèpre se produit en eux à la tête ou à la barbe, le prêtre les verra,
30 kuhani atakichunguza kile kidonda, na kama ataona kuwa kimeingia ndani, na nywele zilizoko juu yake ni njano na nyembamba, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi, kwani ni upele; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza wa kichwa au kidevu.
Et si toutefois cet endroit est plus enfoncé que le reste de la chair, et que le poil soit jaune et plus délié que de coutume, il les déclarera souillés, parce que c’est la lèpre de la tête et de la barbe.
31 Lakini kama kuhani akichunguza aina hii ya kidonda, kionekane kuwa hakina shimo na hakuna nywele nyeusi juu yake, basi atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Si au contraire il voit l’endroit de la tache égal à la chair voisine et le poil noir, il le renfermera pendant sept jours,
32 Siku ya saba kuhani atachunguza kidonda kile, na kama upele haujaenea, na hakuna nywele za manjano juu yake, wala hakuna shimo lolote,
Et au septième jour, il le regardera. Si la tache n’a pas crû, si le poil a gardé sa couleur, et si l’endroit de la plaie est égal au reste de la chair:
33 mtu huyo ni lazima anyolewe, isipokuwa mahali palipo na ugonjwa, naye kuhani atamtenga kwa siku nyingine saba.
L’homme sera rasé, hormis l’endroit de la tache, et il sera renfermé pendant sept autres jours.
34 Siku ya saba kuhani atachunguza tena ule upele; ikiwa haujaenea kwenye ngozi na hakuna shimo mahali pale, kuhani atamtangaza kuwa safi. Lazima afue nguo zake, naye atakuwa safi.
Si, au septième jour, la plaie semble s’être arrêtée à sa place, et n’être pas plus enfoncée que le reste de la chair, il le déclarera pur; or, ses vêtements lavés, il sera pur.
35 Lakini ikiwa upele utaenea juu ya ngozi baada ya kutangazwa kuwa safi,
Si au contraire après sa purification déclarée, la tache croît de nouveau sur la peau,
36 kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, kuhani hana haja ya kutazama kama kuna nywele za manjano, mtu huyo ni najisi.
Il ne recherchera plus si le poil est devenu d’une couleur jaune, parce qu’évidemment il est impur.
37 Hata hivyo, katika uchunguzi wake akiona hapajabadilika, na nywele nyeusi zimeota juu yake, upele umepona. Yeye si najisi, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Mais si la tache s’est arrêtée, et que les poils soient noirs, qu’il reconnaisse que l’homme est guéri, et que hardiment il le proclame pur.
38 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana alama nyeupe juu ya ngozi yake,
Un homme, ou une femme, si une blancheur paraît sur leur peau,
39 kuhani atamchunguza, na kama alama hizo zina weupe uliofifia, ni vipele visivyo na madhara vilivyojitokeza kwenye ngozi; mtu huyo ni safi.
Le prêtre les regardera; s’il découvre qu’une blancheur un peu obscure lait sur la peau, qu’il sache que ce n’est pas une lèpre, mais une tache de couleur blanche, et que l’homme est pur.
40 “Wakati mwanaume hana nywele naye ana upaa, yeye ni safi.
Un homme dont les cheveux tombent de la tête est chauve et pur;
41 Ikiwa hana nywele kwenye ngozi ya kichwa chake, na ana upaa tangu kwenye paji, ni safi.
Et si c’est du front que tombent les cheveux, il est chauve par devant et pur.
42 Lakini kama ana kidonda chenye wekundu na weupe kwenye kichwa chake chenye upaa, au kwenye paji la uso, ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza unaojitokeza kichwani au kwenye paji lake la uso.
Si au contraire sur la partie chauve de derrière et sur la partie chauve de devant une couleur blanche ou rousse se forme,
43 Kuhani atamchunguza, na kama kidonda kilichovimba juu ya kichwa chake au kwenye paji la uso ni chekundu au cheupe kama ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza,
Et que le prêtre la voie, il le condamnera pour cause d’une lèpre non douteuse qui s’est formée sur la partie chauve.
44 mtu huyo ni mgonjwa, na ni najisi. Kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya kidonda kwenye kichwa chake.
Quiconque donc sera entaché de la lèpre, et aura été séparé d’après la décision du prêtre,
45 “Mtu mwenye ugonjwa kama huo wa kuambukiza ni lazima avae nguo zilizoraruka, awachilie nywele zake bila kuzichana, afunike sehemu ya chini ya uso wake, na apige kelele, ‘Najisi! Najisi!’
Aura ses vêtements décousus, la tête nue, le visage couvert de son vêtement, et il criera qu’il est souillé et impur.
46 Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo wa kuambukiza atabaki kuwa najisi. Ni lazima aishi peke yake; ni lazima aishi nje ya kambi.
Pendant tout le temps qu’il sera lépreux et impur, il habitera seul hors du camp.
47 “Kama vazi lolote lina maambukizo ya upele: likiwa ni vazi la sufu au kitani,
Le vêtement de laine ou de lin qui aura une lèpre
48 lolote lililofumwa au kusokotwa likiwa la kitani au la sufu, ngozi yoyote au chochote kilichotengenezwa kwa ngozi,
Dans la chaîne et la trame, ou certainement une peau, ou tout ce qui se fait de peau,
49 tena kama maambukizo kwenye vazi, au ngozi, au lililofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi, ni rangi ya kijani au nyekundu, huo ni upele unaoenea na ni lazima kuhani aonyeshwe.
S’il est souillé d’une tache blanche ou rousse, elle sera réputée lèpre, et montrée au prêtre,
50 Kuhani atachunguza upele huo na kukitenga kifaa hicho kwa siku saba.
Qui après l’avoir considérée l’enfermera pendant sept jours;
51 Siku ya saba atakichunguza, na kama upele umeenea kwenye nguo, au kifaa kilichofumwa au kusokotwa, au ngozi, kwa vyovyote vile itumikavyo, ni upele uangamizao, kifaa hicho ni najisi.
Et au septième jour la regardant de nouveau, s’il découvre qu’elle a crû, c’est une lèpre persévérante: il jugera le vêtement souillé, ainsi que toute chose en laquelle sera trouvée la tache;
52 Ni lazima aichome hiyo nguo, ikiwa ni ya sufu ama kitani iliyofumwa ama kusokotwa, ama chombo chochote cha ngozi chenye maambukizo, kwa kuwa ni upele unaoangamiza; chombo chote ni lazima kichomwe moto.
Et à cause de cela il sera entièrement brûlé par les flammes.
53 “Lakini wakati kuhani atakapokichunguza na kuona kuwa ule upele haujaenea kwenye nguo iliyofumwa au kusokotwa, au vifaa vya ngozi,
Que s’il voit que la tache n’ait pas crû,
54 ataagiza kwamba kifaa chenye maambukizo kisafishwe. Kisha atakitenga kwa siku saba.
Il ordonnera, et on lavera ce qui contient la lèpre, et il l’enfermera pendant sept autres jours.
55 Baada ya kifaa chenye maambukizo kusafishwa, kuhani atakichunguza, na kama upele haujaonyesha badiliko lolote, hata kama haujaenea, ni najisi. Kichome kwa moto, iwe upele umeenea upande mmoja au mwingine.
Et lorsqu’il verra que son aspect primitif n’est pas revenu, et que cependant la lèpre n’a pas crû, il jugera le vêtement impur et le brûlera au feu, parce que la lèpre s’est répandue à la superficie du vêtement, ou dans l’épaisseur.
56 Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kuoshwa, basi atararua sehemu iliyo ambukizwa ya nguo au ngozi au kifaa kilichofumwa au kusokotwa.
Si au contraire l’endroit de la lèpre est plus sombre après que le vêtement aura été lavé, il le déchirera et le séparera du vêtement entier.
57 Lakini kama ikijitokeza tena kwenye nguo au kitu kilichofumwa au kusokotwa, ama kifaa cha ngozi, kwamba ule upele unaenea, chochote chenye upele ni lazima kichomwe kwa moto.
Que s’il paraît encore dans ces endroits qui auparavant étaient sans tache, une lèpre volante et vague, il doit être brûlé au feu.
58 Nguo, au kitu kilichofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi ambacho kimesafishwa na kuondolewa upele, ni lazima kioshwe tena, nacho kitakuwa safi.”
Si elle cesse, il lavera une seconde fois dans l’eau les parties qui sont pures, et elles seront entièrement pures.
59 Haya ni masharti kuhusu maambukizo ya upele kwenye mavazi ya sufu au kitani, yaliyofumwa ama kusokotwa, ama kifaa chochote cha ngozi, kwa ajili ya kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Telle est la loi de la lèpre du vêtement de laine et de lin, de la chaîne et de la trame, et de tout objet qui est fait de peau, pour qu’on sache comment on doit déclarer qu’il est pur ou qu’il est souillé.