< Mambo ya Walawi 13 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Yahvé parla à Moïse et à Aaron, et dit:
2 “Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au alama nyeupe juu ya ngozi yake ambayo yaweza kuwa ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani ama kwa wanawe, kuhani mmojawapo.
« Lorsqu'un homme aura une tuméfaction sur la peau de son corps, ou une croûte, ou une tache brillante, et que cela deviendra dans la peau de son corps la plaie de la lèpre, on l'amènera au prêtre Aaron ou à l'un de ses fils, les prêtres.
3 Kuhani atachunguza hicho kidonda kilichopo juu ya ngozi yake, na kama nywele za mahali palipo na kidonda zimebadilika kuwa nyeupe, na ikiwa kidonda kimeingia ndani ya ngozi, basi ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma. Kuhani atakapomchunguza, atamtangaza mtu huyo kuwa ni najisi kwa kawaida ya ibada.
Le prêtre examinera la plaie sur la peau du corps. Si le poil de la plaie est devenu blanc, et si l'aspect de la plaie est plus profond que la peau du corps, c'est la plaie de la lèpre; le prêtre l'examinera donc et le déclarera impur.
4 Kama alama juu ya ngozi yake ni nyeupe, lakini haionekani kuwa imeingia ndani zaidi ya ngozi, na nywele kwenye alama hiyo hazijageuka kuwa nyeupe, kuhani atamtenga mtu huyo mahali pa pekee kwa siku saba.
Si la tache brillante est blanche sur la peau de son corps, que son aspect n'est pas plus profond que la peau et que son poil n'est pas devenu blanc, le prêtre isolera la personne infectée pendant sept jours.
5 Siku ya saba, kuhani atamchunguza, na kama hakuona badiliko kwenye kile kidonda na hakijaenea juu ya ngozi, atamtenga kwa siku nyingine saba.
Le prêtre l'examinera le septième jour. Si, à ses yeux, la plaie est arrêtée et que la plaie ne s'est pas propagée dans la peau, le prêtre l'isolera encore pendant sept jours.
6 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama kidonda kimepungua na hakijaenea juu ya ngozi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa ni safi, ni upele tu. Ni lazima mtu huyo afue mavazi yake, naye atakuwa safi.
Le prêtre l'examinera de nouveau le septième jour. Voici, si la plaie a disparu et que la plaie ne s'est pas propagée dans la peau, alors le prêtre le déclarera pur. C'est une gale. Il lavera ses vêtements et sera pur.
7 Lakini ikiwa ule upele utaenea juu ya ngozi yake baada ya yeye kujionyesha kwa kuhani na kutangazwa kuwa safi, ni lazima aende tena kwa kuhani.
Mais si la gale s'étend sur la peau après qu'il s'est présenté au prêtre pour sa purification, il se présentera de nouveau au prêtre.
8 Kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, atamtangaza kuwa najisi, kwani ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma.
Le prêtre l'examinera; et voici, si la gale s'est étendue sur la peau, le prêtre le déclarera impur. C'est la lèpre.
9 “Wakati mtu yeyote ana ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa kuhani.
« Lorsqu'un homme aura la plaie de la lèpre, on l'amènera au prêtre;
10 Kuhani atamchunguza na kama kuna uvimbe mweupe juu ya ngozi ambao umefanya nywele kuwa nyeupe, na kama kuna nyama mbichi ndani ya uvimbe,
et le prêtre l'examinera. S'il y a une tuméfaction blanche sur la peau, si le poil est devenu blanc et s'il y a de la chair à vif dans la tuméfaction,
11 ni ugonjwa sugu wa ngozi, na kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga tena kwa sababu ni najisi tayari.
c'est une lèpre chronique sur la peau de son corps, et le prêtre le déclarera impur. Il ne l'isolera pas, car il est déjà impur.
12 “Ikiwa ugonjwa utakuwa umeenea kwenye ngozi yake yote kwa kadiri kuhani atakavyoweza kuona, kwamba umeenea kwenye ngozi yote ya huyo mgonjwa kutoka kichwani mpaka wayo,
« Si la lèpre se déclare sur toute la peau, et si la lèpre couvre toute la peau de la personne infectée, depuis sa tête jusqu'à ses pieds, selon ce qui apparaît au prêtre,
13 kuhani atamchunguza, na kama ugonjwa umeenea mwili mzima, atamtangaza huyo mtu kuwa safi. Kwa kuwa mwili wote umekuwa mweupe, yeye ni safi.
alors le prêtre l'examinera. Voici, si la lèpre a couvert toute sa chair, il le déclarera pur de la plaie. Tout est devenu blanc: il est pur.
14 Lakini itokeapo nyama mbichi kwenye ngozi yake, atakuwa najisi.
Mais si de la chair crue apparaît en lui, il sera impur.
15 Kuhani atakapoiona hiyo nyama mbichi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hiyo nyama mbichi ni najisi, ana ugonjwa wa kuambukiza.
Le prêtre examinera la chair crue et le déclarera impur: la chair crue est impure. C'est la lèpre.
16 Hiyo nyama mbichi ikigeuka na kuwa nyeupe, ni lazima amwendee kuhani.
Ou bien, si la chair crue se transforme et devient blanche, il se présentera au sacrificateur.
17 Kuhani atamchunguza, na kama vidonda vimekuwa vyeupe, kuhani atamtangaza mgonjwa huyo kuwa safi; kisha atakuwa safi.
Le prêtre l'examinera. Si la plaie est devenue blanche, le prêtre le déclarera pur de la plaie. Il est pur.
18 “Wakati mtu ana jipu juu ya ngozi yake nalo likapona,
« Lorsque le corps a un furoncle sur la peau, qu'il est guéri,
19 napo mahali palipokuwa na jipu pakatokea uvimbe mweupe, au alama yenye wekundu na weupe, ni lazima akajionyeshe kwa kuhani.
et qu'à la place du furoncle il y a une tuméfaction blanche, ou une tache brillante, d'un blanc rougeâtre, on le montrera au prêtre.
20 Kuhani atapachunguza, na kama uvimbe umezama ndani ya ngozi, na nywele zimegeuka kuwa nyeupe, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza uliojitokeza pale jipu lilipokuwa.
Le prêtre l'examinera. Si son aspect est plus profond que la peau, et si son poil est devenu blanc, le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre. Elle s'est déclarée dans le furoncle.
21 Lakini ikiwa wakati kuhani anapopachunguza pakawa hapana nywele nyeupe ndani yake, wala hakuna shimo bali pamepungua, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Mais si le prêtre l'examine, et qu'il n'y ait pas de poils blancs, et que la plaie ne soit pas plus profonde que la peau, mais qu'elle soit pâle, le prêtre l'isolera pendant sept jours.
22 Kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Si elle se propage dans la peau, le prêtre la déclarera impure. C'est une plaie.
23 Lakini ikiwa ile alama haijabadilika wala kuenea, ni kovu tu kutokana na jipu, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Mais si la tache brillante reste à sa place, et ne s'est pas étendue, c'est la cicatrice de l'ulcère; et le prêtre le déclarera pur.
24 “Wakati mtu ameungua kwenye ngozi yake, pakatokea alama yenye wekundu na weupe, au alama nyeupe ikaonekana penye nyama mbichi pale palipoungua,
« Ou lorsque le corps a sur la peau une brûlure par le feu, et que la chair crue de la brûlure devient une tache brillante, d'un blanc rougeâtre ou blanc,
25 kuhani ataichunguza ile alama, na kama nywele zilizoko juu yake zimegeuka kuwa nyeupe, napo pametokea shimo, basi huo ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza ambao umetokea juu ya jeraha la moto. Kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
le prêtre l'examinera; et voici, si le poil de la tache brillante est devenu blanc, et si son aspect est plus profond que la peau, c'est la lèpre. Elle s'est déclarée chez le brûlé, et le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre.
26 Lakini kama kuhani akichunguza na kuona kwamba hakuna nywele nyeupe kwenye alama ile, wala hakuna shimo napo pameanza kupungua, basi kuhani atamtenga kwa siku saba.
Mais si le prêtre l'examine, et que voici, il n'y a pas de poil blanc dans la tache brillante, et qu'elle n'est pas plus profonde que la peau, mais qu'elle s'est effacée, alors le prêtre l'isolera sept jours.
27 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
Le prêtre l'examinera le septième jour. Si la tache s'est étendue sur la peau, le prêtre le déclarera impur. C'est la plaie de la lèpre.
28 Lakini, kama alama ile haikubadilika na wala haijaenea kwenye ngozi, napo pamepungua, ni uvimbe kutokana na jeraha la moto, na kuhani atamtangaza kuwa safi; ni kovu tu kutokana na kuungua.
Si la tache brillante reste à sa place, ne s'est pas étendue dans la peau, mais s'est estompée, c'est l'enflure de la brûlure, et le prêtre le déclarera pur, car c'est la cicatrice de la brûlure.
29 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana kidonda juu ya kichwa au juu ya kidevu,
« Lorsqu'un homme ou une femme aura une plaie sur la tête ou sur la barbe,
30 kuhani atakichunguza kile kidonda, na kama ataona kuwa kimeingia ndani, na nywele zilizoko juu yake ni njano na nyembamba, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi, kwani ni upele; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza wa kichwa au kidevu.
le prêtre examinera la plaie; et voici, si son aspect est plus profond que la peau, et que les poils qui la composent sont jaunes et fins, le prêtre le déclarera impur. C'est une démangeaison. C'est une lèpre de la tête ou de la barbe.
31 Lakini kama kuhani akichunguza aina hii ya kidonda, kionekane kuwa hakina shimo na hakuna nywele nyeusi juu yake, basi atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
Si le prêtre examine la plaie de démangeaison, et que son aspect n'est pas plus profond que la peau, et qu'il n'y a pas de poil noir, alors le prêtre isolera la personne atteinte de démangeaison pendant sept jours.
32 Siku ya saba kuhani atachunguza kidonda kile, na kama upele haujaenea, na hakuna nywele za manjano juu yake, wala hakuna shimo lolote,
Le septième jour, le prêtre examinera la plaie; et voici, si la démangeaison ne s'est pas étendue, s'il n'y a pas de poil jaune et si l'aspect de la démangeaison n'est pas plus profond que la peau,
33 mtu huyo ni lazima anyolewe, isipokuwa mahali palipo na ugonjwa, naye kuhani atamtenga kwa siku nyingine saba.
alors il sera rasé, mais il ne rasera pas la démangeaison. Ensuite, le prêtre isolera celui qui a la démangeaison pendant sept jours encore.
34 Siku ya saba kuhani atachunguza tena ule upele; ikiwa haujaenea kwenye ngozi na hakuna shimo mahali pale, kuhani atamtangaza kuwa safi. Lazima afue nguo zake, naye atakuwa safi.
Le septième jour, le prêtre examinera la démangeaison; et voici, si la démangeaison ne s'est pas étendue dans la peau, et si son aspect n'est pas plus profond que la peau, alors le prêtre le déclarera pur. Il lavera ses vêtements et sera pur.
35 Lakini ikiwa upele utaenea juu ya ngozi baada ya kutangazwa kuwa safi,
Mais si la démangeaison s'étend sur la peau après sa purification,
36 kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, kuhani hana haja ya kutazama kama kuna nywele za manjano, mtu huyo ni najisi.
le prêtre l'examinera; et voici, si la démangeaison s'est étendue sur la peau, le prêtre ne cherchera pas le poil jaune: il est impur.
37 Hata hivyo, katika uchunguzi wake akiona hapajabadilika, na nywele nyeusi zimeota juu yake, upele umepona. Yeye si najisi, kuhani atamtangaza kuwa safi.
Mais si, à ses yeux, la démangeaison est arrêtée et qu'un poil noir y a poussé, alors la démangeaison est guérie. Il est pur. Le prêtre le déclarera pur.
38 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana alama nyeupe juu ya ngozi yake,
« Lorsqu'un homme ou une femme aura sur la peau de son corps des taches brillantes, d'un blanc éclatant,
39 kuhani atamchunguza, na kama alama hizo zina weupe uliofifia, ni vipele visivyo na madhara vilivyojitokeza kwenye ngozi; mtu huyo ni safi.
le prêtre les examinera. Si les taches brillantes sur la peau de leur corps sont d'un blanc terne, c'est une éruption cutanée inoffensive. La peau a éclaté. Il est pur.
40 “Wakati mwanaume hana nywele naye ana upaa, yeye ni safi.
« Si les cheveux d'un homme sont tombés de sa tête, il est chauve. Il est pur.
41 Ikiwa hana nywele kwenye ngozi ya kichwa chake, na ana upaa tangu kwenye paji, ni safi.
Si ses cheveux sont tombés de la partie antérieure de sa tête, il est chauve du front. Il est pur.
42 Lakini kama ana kidonda chenye wekundu na weupe kwenye kichwa chake chenye upaa, au kwenye paji la uso, ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza unaojitokeza kichwani au kwenye paji lake la uso.
Mais s'il y a une plaie d'un blanc rougeâtre dans la tête chauve ou sur le front chauve, c'est la lèpre qui éclate dans sa tête chauve ou sur son front chauve.
43 Kuhani atamchunguza, na kama kidonda kilichovimba juu ya kichwa chake au kwenye paji la uso ni chekundu au cheupe kama ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza,
Le prêtre l'examinera. Voici, si l'enflure de la plaie est d'un blanc rougeâtre dans sa tête chauve ou dans son front chauve, comme l'apparence de la lèpre sur la peau du corps,
44 mtu huyo ni mgonjwa, na ni najisi. Kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya kidonda kwenye kichwa chake.
c'est un homme lépreux. Il est impur. Le prêtre le déclarera impur. Sa plaie est sur sa tête.
45 “Mtu mwenye ugonjwa kama huo wa kuambukiza ni lazima avae nguo zilizoraruka, awachilie nywele zake bila kuzichana, afunike sehemu ya chini ya uso wake, na apige kelele, ‘Najisi! Najisi!’
« Le lépreux qui a la plaie portera des vêtements déchirés, et les cheveux de sa tête seront détachés. Il se couvrira la lèvre supérieure et criera: 'Impur! Impur!
46 Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo wa kuambukiza atabaki kuwa najisi. Ni lazima aishi peke yake; ni lazima aishi nje ya kambi.
Pendant tout le temps que durera la plaie, il sera impur. Il est impur. Il habitera seul. Sa demeure sera en dehors du camp.
47 “Kama vazi lolote lina maambukizo ya upele: likiwa ni vazi la sufu au kitani,
Le vêtement dans lequel se trouve la plaie de la lèpre, soit un vêtement de laine ou un vêtement de lin,
48 lolote lililofumwa au kusokotwa likiwa la kitani au la sufu, ngozi yoyote au chochote kilichotengenezwa kwa ngozi,
soit un vêtement de chaîne ou de trame, de lin ou de laine, soit un vêtement de cuir ou un objet en cuir,
49 tena kama maambukizo kwenye vazi, au ngozi, au lililofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi, ni rangi ya kijani au nyekundu, huo ni upele unaoenea na ni lazima kuhani aonyeshwe.
si la plaie est verdâtre ou rougeâtre dans le vêtement, dans le cuir, dans la chaîne ou la trame, ou dans un objet en cuir, c'est la plaie de la lèpre; on la montrera au sacrificateur.
50 Kuhani atachunguza upele huo na kukitenga kifaa hicho kwa siku saba.
Le prêtre examinera la plaie et l'isolera pendant sept jours.
51 Siku ya saba atakichunguza, na kama upele umeenea kwenye nguo, au kifaa kilichofumwa au kusokotwa, au ngozi, kwa vyovyote vile itumikavyo, ni upele uangamizao, kifaa hicho ni najisi.
Le septième jour, il examinera la plaie. Si la plaie s'est étendue dans le vêtement, soit dans la chaîne, soit dans la trame, soit dans la peau, quel que soit l'usage auquel la peau est destinée, la plaie est une moisissure destructrice. Il est impur.
52 Ni lazima aichome hiyo nguo, ikiwa ni ya sufu ama kitani iliyofumwa ama kusokotwa, ama chombo chochote cha ngozi chenye maambukizo, kwa kuwa ni upele unaoangamiza; chombo chote ni lazima kichomwe moto.
Il brûlera le vêtement, qu'il s'agisse de la chaîne ou de la trame, de laine ou de lin, ou de tout ce qui est en cuir, dans lequel se trouve la plaie, car c'est une moisissure destructrice. Il le brûlera au feu.
53 “Lakini wakati kuhani atakapokichunguza na kuona kuwa ule upele haujaenea kwenye nguo iliyofumwa au kusokotwa, au vifaa vya ngozi,
« Si le prêtre l'examine et que la plaie ne s'est pas étendue dans le vêtement, ni dans la chaîne, ni dans la trame, ni dans aucune partie de la peau,
54 ataagiza kwamba kifaa chenye maambukizo kisafishwe. Kisha atakitenga kwa siku saba.
le prêtre ordonnera qu'on lave l'objet dans lequel se trouve la plaie, et il l'isolera encore sept jours.
55 Baada ya kifaa chenye maambukizo kusafishwa, kuhani atakichunguza, na kama upele haujaonyesha badiliko lolote, hata kama haujaenea, ni najisi. Kichome kwa moto, iwe upele umeenea upande mmoja au mwingine.
Puis le prêtre l'examinera, après que la plaie aura été lavée; et voici, si la plaie n'a pas changé de couleur, et si la plaie ne s'est pas étendue, elle est impure; vous la brûlerez au feu. C'est une tache de moisissure, que la plaie soit en dedans ou en dehors.
56 Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kuoshwa, basi atararua sehemu iliyo ambukizwa ya nguo au ngozi au kifaa kilichofumwa au kusokotwa.
Si le prêtre regarde, et que la plaie ait pâli après avoir été lavée, il l'arrachera du vêtement, ou de la peau, ou de la chaîne, ou de la trame;
57 Lakini kama ikijitokeza tena kwenye nguo au kitu kilichofumwa au kusokotwa, ama kifaa cha ngozi, kwamba ule upele unaenea, chochote chenye upele ni lazima kichomwe kwa moto.
et si elle reparaît dans le vêtement, soit dans la chaîne, soit dans la trame, ou dans quoi que ce soit de peau, elle se propage. Vous brûlerez au feu ce qui contient la plaie.
58 Nguo, au kitu kilichofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi ambacho kimesafishwa na kuondolewa upele, ni lazima kioshwe tena, nacho kitakuwa safi.”
Le vêtement, soit la chaîne, soit la trame, soit tout ce qui est de peau, que vous laverez, si la plaie en est sortie, vous le laverez une seconde fois, et il sera pur. »
59 Haya ni masharti kuhusu maambukizo ya upele kwenye mavazi ya sufu au kitani, yaliyofumwa ama kusokotwa, ama kifaa chochote cha ngozi, kwa ajili ya kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Voici la loi concernant la plaie de la moisissure dans un vêtement de laine ou de lin, soit dans la chaîne, soit dans la trame, soit dans tout ce qui est en peau, pour le déclarer pur ou pour le déclarer impur.