< Mambo ya Walawi 13 >

1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
Yahweh said this to Aaron and Moses/me:
2 “Iwapo mtu yeyote atakuwa na uvimbe au upele au alama nyeupe juu ya ngozi yake ambayo yaweza kuwa ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa Aroni kuhani ama kwa wanawe, kuhani mmojawapo.
“When someone has on his skin a swelling or a rash or a shiny/bright spot that may become (contagious/a dreaded skin disease), he must be brought to Aaron or to one of his sons who are also priests.
3 Kuhani atachunguza hicho kidonda kilichopo juu ya ngozi yake, na kama nywele za mahali palipo na kidonda zimebadilika kuwa nyeupe, na ikiwa kidonda kimeingia ndani ya ngozi, basi ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma. Kuhani atakapomchunguza, atamtangaza mtu huyo kuwa ni najisi kwa kawaida ya ibada.
The priest must examine that part of the person’s skin. If the hair in that area has become white and it appears that the sore is deeper than just on the skin, it is a contagious skin disease. When the priest sees that, he must declare that the person must stay away from other people [MTY].
4 Kama alama juu ya ngozi yake ni nyeupe, lakini haionekani kuwa imeingia ndani zaidi ya ngozi, na nywele kwenye alama hiyo hazijageuka kuwa nyeupe, kuhani atamtenga mtu huyo mahali pa pekee kwa siku saba.
If the spot on the person’s skin is white but it does not appear that the sore is deeper than just on the skin, the priest must tell him to stay away from other people for seven days.
5 Siku ya saba, kuhani atamchunguza, na kama hakuona badiliko kwenye kile kidonda na hakijaenea juu ya ngozi, atamtenga kwa siku nyingine saba.
Then the priest must examine the person again. If the priest sees that the sore has not changed and has not spread, he must tell the person to stay away from people for seven more days.
6 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama kidonda kimepungua na hakijaenea juu ya ngozi, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa ni safi, ni upele tu. Ni lazima mtu huyo afue mavazi yake, naye atakuwa safi.
Then the priest must examine him again. If the sore has faded and has not spread, the priest will allow him to be with other people again; it is only a rash. After the person washes his clothes, he will be allowed to be with other people again.
7 Lakini ikiwa ule upele utaenea juu ya ngozi yake baada ya yeye kujionyesha kwa kuhani na kutangazwa kuwa safi, ni lazima aende tena kwa kuhani.
But if the sore spreads after the priest has examined him, he must go to the priest again.
8 Kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, atamtangaza kuwa najisi, kwani ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, yaani ukoma.
The priest will examine him; and if the sore has spread to more of the skin, it is a contagious skin disease, and the priest will declare that he must stay away from other people.
9 “Wakati mtu yeyote ana ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, ni lazima aletwe kwa kuhani.
When anyone has a contagious skin disease, he must be brought to the priest.
10 Kuhani atamchunguza na kama kuna uvimbe mweupe juu ya ngozi ambao umefanya nywele kuwa nyeupe, na kama kuna nyama mbichi ndani ya uvimbe,
The priest must examine him. And if there is a white swelling in the skin that has caused the hair in that swelling to become white, and if the flesh in that area is painful/sensitive,
11 ni ugonjwa sugu wa ngozi, na kuhani atamtangaza kuwa najisi. Hatamtenga tena kwa sababu ni najisi tayari.
it is a permanent skin disease, and the priest will declare that he must stay away from other people. The priest does not need to tell that person that he must avoid other people, because other people already are wanting to stay away from him.
12 “Ikiwa ugonjwa utakuwa umeenea kwenye ngozi yake yote kwa kadiri kuhani atakavyoweza kuona, kwamba umeenea kwenye ngozi yote ya huyo mgonjwa kutoka kichwani mpaka wayo,
‘If the disease spreads all over someone’s body, and the priest examines that person and sees that it is covering his skin from his head to his feet,
13 kuhani atamchunguza, na kama ugonjwa umeenea mwili mzima, atamtangaza huyo mtu kuwa safi. Kwa kuwa mwili wote umekuwa mweupe, yeye ni safi.
and it has caused all his skin to become white [which will indicate that the disease has ended], the priest will declare that the person does not have to stay away from other people.
14 Lakini itokeapo nyama mbichi kwenye ngozi yake, atakuwa najisi.
But if the person has open sores and they are very painful/sensitive, he has a contagious skin disease,
15 Kuhani atakapoiona hiyo nyama mbichi, atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Hiyo nyama mbichi ni najisi, ana ugonjwa wa kuambukiza.
and when the priest sees that, he will declare that the person must stay away from other people.
16 Hiyo nyama mbichi ikigeuka na kuwa nyeupe, ni lazima amwendee kuhani.
But if the person’s flesh changes and becomes white, he must go to the priest again.
17 Kuhani atamchunguza, na kama vidonda vimekuwa vyeupe, kuhani atamtangaza mgonjwa huyo kuwa safi; kisha atakuwa safi.
The priest must examine him again; and if the sores have become white, the priest will declare that the person who had been infected is now permitted to be with other people again.
18 “Wakati mtu ana jipu juu ya ngozi yake nalo likapona,
‘Then someone has a boil on his skin and it has healed,
19 napo mahali palipokuwa na jipu pakatokea uvimbe mweupe, au alama yenye wekundu na weupe, ni lazima akajionyeshe kwa kuhani.
but in the place where the boil was a white swelling or a bright/shiny spot appears, he must go to the priest.
20 Kuhani atapachunguza, na kama uvimbe umezama ndani ya ngozi, na nywele zimegeuka kuwa nyeupe, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi. Ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza uliojitokeza pale jipu lilipokuwa.
The priest must examine it. And if it seems to be deeper than just on the skin, and if the hair in that spot has become white, it is a contagious skin disease that has appeared where the boil had been. And the priest will declare that the person must stay away from other people.
21 Lakini ikiwa wakati kuhani anapopachunguza pakawa hapana nywele nyeupe ndani yake, wala hakuna shimo bali pamepungua, basi kuhani atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
But when the priest examines it, if there is no white hair in that spot and it is only on the surface of the skin and has become less bright/shiny, then the priest will order him to stay away from other people for seven days.
22 Kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
But if it is spreading, it is contagious and the priest will declare that the person must stay away from other people.
23 Lakini ikiwa ile alama haijabadilika wala kuenea, ni kovu tu kutokana na jipu, kuhani atamtangaza kuwa safi.
But if that spot is unchanged and has not spread, it is only a scar from the boil, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
24 “Wakati mtu ameungua kwenye ngozi yake, pakatokea alama yenye wekundu na weupe, au alama nyeupe ikaonekana penye nyama mbichi pale palipoungua,
‘Then someone has a burn on his skin and a bright/shiny or white spot appears, and the flesh in that area is sensitive/painful,
25 kuhani ataichunguza ile alama, na kama nywele zilizoko juu yake zimegeuka kuwa nyeupe, napo pametokea shimo, basi huo ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza ambao umetokea juu ya jeraha la moto. Kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
the priest must examine the spot. If the hair in that spot has turned white and it seems to be deeper than just on the surface of the skin, it is a contagious skin disease that has appeared where the burn was, and that person must stay away from other people.
26 Lakini kama kuhani akichunguza na kuona kwamba hakuna nywele nyeupe kwenye alama ile, wala hakuna shimo napo pameanza kupungua, basi kuhani atamtenga kwa siku saba.
But when the priest examines it and sees that there is no white hair in that spot and it is only on the surface of the skin, and has faded, the priest will declare that the person must stay away from people for seven days.
27 Siku ya saba kuhani atamchunguza tena, na kama unaenea kwenye ngozi, kuhani atamtangaza kuwa najisi; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza.
On the seventh day, the priest will examine him again. If the sore is spreading, it is a contagious skin disease, and the priest will declare that the person must stay away from other people.
28 Lakini, kama alama ile haikubadilika na wala haijaenea kwenye ngozi, napo pamepungua, ni uvimbe kutokana na jeraha la moto, na kuhani atamtangaza kuwa safi; ni kovu tu kutokana na kuungua.
However, if the spot is not changed and has not spread but has faded, it is only a scar from the burn, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
29 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana kidonda juu ya kichwa au juu ya kidevu,
‘If a man or a woman has a sore on his head or on his chin,
30 kuhani atakichunguza kile kidonda, na kama ataona kuwa kimeingia ndani, na nywele zilizoko juu yake ni njano na nyembamba, kuhani atamtangaza mtu huyo kuwa najisi, kwani ni upele; ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza wa kichwa au kidevu.
the priest must examine it. If it appears to be deeper than [just on the surface of] the skin, and the hair in that spot has thinned out and has become yellowish, it is a contagious skin disease that causes itching. And the priest will declare that the person must stay away from other people.
31 Lakini kama kuhani akichunguza aina hii ya kidonda, kionekane kuwa hakina shimo na hakuna nywele nyeusi juu yake, basi atamtenga mtu huyo kwa siku saba.
But when the priest examines that kind of sore, if it seems to be only on the surface of the skin and there is no healthy hair in it, the priest will tell the person to stay away from other people for seven days.
32 Siku ya saba kuhani atachunguza kidonda kile, na kama upele haujaenea, na hakuna nywele za manjano juu yake, wala hakuna shimo lolote,
On the seventh day, the priest will examine the sore again. If it has not spread and if there is no yellow hair in that spot and if it appears to be only on the surface of the skin,
33 mtu huyo ni lazima anyolewe, isipokuwa mahali palipo na ugonjwa, naye kuhani atamtenga kwa siku nyingine saba.
the person must shave the hair near the sore but not the hair on the sore. And the priest will tell him to stay away from other people for seven more days.
34 Siku ya saba kuhani atachunguza tena ule upele; ikiwa haujaenea kwenye ngozi na hakuna shimo mahali pale, kuhani atamtangaza kuwa safi. Lazima afue nguo zake, naye atakuwa safi.
On the seventh day, the priest will examine that spot again. If it has not spread and it appears to be only on the surface of the skin, the priest will declare that the person is permitted to be with people again. The person must wash his clothes, and then he can be with other people.
35 Lakini ikiwa upele utaenea juu ya ngozi baada ya kutangazwa kuwa safi,
But if the sore later spreads,
36 kuhani atamchunguza, na kama upele umeenea kwenye ngozi, kuhani hana haja ya kutazama kama kuna nywele za manjano, mtu huyo ni najisi.
the priest must examine him again. If the itch/sore has spread, the priest does not need to look for yellow hair, because it is clear that the person has a contagious skin disease.
37 Hata hivyo, katika uchunguzi wake akiona hapajabadilika, na nywele nyeusi zimeota juu yake, upele umepona. Yeye si najisi, kuhani atamtangaza kuwa safi.
However, if the priest thinks that the spot has not changed, and healthy hair is growing in that area, it is clear that the itch has healed, and the priest will declare that the person is permitted to be with other people again.
38 “Ikiwa mwanaume au mwanamke ana alama nyeupe juu ya ngozi yake,
‘Then a man or a woman has white spots on the skin,
39 kuhani atamchunguza, na kama alama hizo zina weupe uliofifia, ni vipele visivyo na madhara vilivyojitokeza kwenye ngozi; mtu huyo ni safi.
the priest should examine them. But if the spots are dull white, it is only a rash, and [the priest will declare that] the person is permitted to be with other people.
40 “Wakati mwanaume hana nywele naye ana upaa, yeye ni safi.
‘If a man loses the hair on any part of his head, he does not need to stay away from other people.
41 Ikiwa hana nywele kwenye ngozi ya kichwa chake, na ana upaa tangu kwenye paji, ni safi.
42 Lakini kama ana kidonda chenye wekundu na weupe kwenye kichwa chake chenye upaa, au kwenye paji la uso, ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza unaojitokeza kichwani au kwenye paji lake la uso.
But if he gets a bright/shiny sore on his bald head or on his forehead, he has a contagious skin disease.
43 Kuhani atamchunguza, na kama kidonda kilichovimba juu ya kichwa chake au kwenye paji la uso ni chekundu au cheupe kama ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza,
The priest must examine him. If the swollen sore is a bright spot like [the spot on someone who has] a contagious skin disease,
44 mtu huyo ni mgonjwa, na ni najisi. Kuhani atamtangaza kuwa najisi kwa sababu ya kidonda kwenye kichwa chake.
the priest will declare that the man has a contagious skin disease and must not be with other people.
45 “Mtu mwenye ugonjwa kama huo wa kuambukiza ni lazima avae nguo zilizoraruka, awachilie nywele zake bila kuzichana, afunike sehemu ya chini ya uso wake, na apige kelele, ‘Najisi! Najisi!’
‘Anyone who has a contagious skin disease must wear torn clothes and not comb his hair. [When he is near other people], he must cover the lower part to his face and call out, “Do not come near me! I have a contagious skin disease!”
46 Kwa muda wote atakaokuwa na ugonjwa huo wa kuambukiza atabaki kuwa najisi. Ni lazima aishi peke yake; ni lazima aishi nje ya kambi.
He is not allowed to be with other people as long as he has the disease. He must live alone, outside the camp.’”
47 “Kama vazi lolote lina maambukizo ya upele: likiwa ni vazi la sufu au kitani,
“Sometimes a person’s clothing gets mildew on it. It may be clothing that is woven from wool or made from linen or from leather.
48 lolote lililofumwa au kusokotwa likiwa la kitani au la sufu, ngozi yoyote au chochote kilichotengenezwa kwa ngozi,
49 tena kama maambukizo kwenye vazi, au ngozi, au lililofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi, ni rangi ya kijani au nyekundu, huo ni upele unaoenea na ni lazima kuhani aonyeshwe.
If the contaminated/mildewed part is greenish or reddish, it is a spreading mildew, and it must be shown to the priest.
50 Kuhani atachunguza upele huo na kukitenga kifaa hicho kwa siku saba.
The priest will examine it, and then put it in a separate place by itself for seven days.
51 Siku ya saba atakichunguza, na kama upele umeenea kwenye nguo, au kifaa kilichofumwa au kusokotwa, au ngozi, kwa vyovyote vile itumikavyo, ni upele uangamizao, kifaa hicho ni najisi.
On the seventh day he must examine it again. If the mildew has spread, it is clear that it is a type of mildew that destroys clothing, and that clothing must not be worn again.
52 Ni lazima aichome hiyo nguo, ikiwa ni ya sufu ama kitani iliyofumwa ama kusokotwa, ama chombo chochote cha ngozi chenye maambukizo, kwa kuwa ni upele unaoangamiza; chombo chote ni lazima kichomwe moto.
The owner must burn completely the item that has the mildew in it, whatever kind of item it is.
53 “Lakini wakati kuhani atakapokichunguza na kuona kuwa ule upele haujaenea kwenye nguo iliyofumwa au kusokotwa, au vifaa vya ngozi,
But when the priest examines it, if the mildew has not spread,
54 ataagiza kwamba kifaa chenye maambukizo kisafishwe. Kisha atakitenga kwa siku saba.
he will tell the person [who owns it] to wash it. Then he must put it in a separate place for another seven days.
55 Baada ya kifaa chenye maambukizo kusafishwa, kuhani atakichunguza, na kama upele haujaonyesha badiliko lolote, hata kama haujaenea, ni najisi. Kichome kwa moto, iwe upele umeenea upande mmoja au mwingine.
Then the priest will examine it again. If the color of the mildew has not changed, even though it has not spread, that item must not be worn again. It does not matter if the mildew is on the inside of the clothing or on the outside; it must be burned.
56 Kama kuhani ataona kuwa ile alama imefifia baada ya kuoshwa, basi atararua sehemu iliyo ambukizwa ya nguo au ngozi au kifaa kilichofumwa au kusokotwa.
But when the priest examines it [after it has been washed], if the mildew has faded, he must tear out that part that had the mildew in it.
57 Lakini kama ikijitokeza tena kwenye nguo au kitu kilichofumwa au kusokotwa, ama kifaa cha ngozi, kwamba ule upele unaenea, chochote chenye upele ni lazima kichomwe kwa moto.
But if the mildew reappears in that item, it is clear that it is spreading, and the whole item must be burned.
58 Nguo, au kitu kilichofumwa au kusokotwa, au kifaa chochote cha ngozi ambacho kimesafishwa na kuondolewa upele, ni lazima kioshwe tena, nacho kitakuwa safi.”
But after the clothing is washed and the mildew disappears, it must be washed again, and then it can be worn again.
59 Haya ni masharti kuhusu maambukizo ya upele kwenye mavazi ya sufu au kitani, yaliyofumwa ama kusokotwa, ama kifaa chochote cha ngozi, kwa ajili ya kuvitangaza kuwa safi au najisi.
Those are the regulations concerning mildew on things made of wool or linen or leather, for deciding whether those things can continue to be worn or not.”

< Mambo ya Walawi 13 >