< Mambo ya Walawi 12 >
Perwerdigar Musagha söz qilip mundaq dédi: —
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi.
Israillargha söz qilip mundaq dégin: — «Ayal kishi hamilidar bolup oghul tughsa, adet körüp aghriq bolghan künliridikidek yette kün’giche napak sanalsun.
3 Mvulana atatahiriwa siku ya nane.
Sekkizinchi küni oghli bolsa xetne qilinsun.
4 Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia.
Ayal bolsa shuningdin kéyin ottuz üch kün’giche «qan paklinish»ta tursun; paklinish künliri tamam bolmighuche héchbir muqeddes nersige tegmisun, muqeddes jayghimu kirmisun.
5 Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.
Eger u qiz tughsa undaqta adet künliridikidek ikki heptigiche napak turup, andin atmish alte kün’giche «qan paklinish»ta tursun.
6 “‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
Meyli oghul yaki qiz tughsun, qan paklinish künliri tamam bolghandin kéyin u ayal köydürme qurbanliq üchün bir yashqa kirgen qozini, gunah qurbanliqi üchün bir bachka yaki paxtekni élip jamaet chédirining kirish aghzigha, kahinning qéshigha keltürsun.
7 Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake. “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
Kahin uni Perwerdigarning aldida sunup, shu ayal üchün kafaret keltüridu; shuning bilen u xunidin pak bolidu. Oghul yaki qiz tughqan ayal toghrisidiki qanun-belgilime mana shudur.
8 Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”
Eger uning qozigha qurbi yetmise, u ikki paxtek yaki ikki bachka keltürsun; ularning biri köydürme qurbanliq üchün, yene biri gunah qurbanliqi üchün bolidu; shu yol bilen kahin uning üchün kafaret keltüridu; u ayal pak bolidu.