< Mambo ya Walawi 12 >

1 Bwana akamwambia Mose,
خداوند به موسی فرمود:
2 “Waambie Waisraeli: ‘Mwanamke ambaye atapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada kwa siku saba, kama anavyokuwa najisi wakati wa siku zake za hedhi.
«این دستورها را به بنی‌اسرائیل بده: هرگاه زنی پسری بزاید، آن زن تا مدت هفت روز نجس خواهد بود، همان‌گونه که به هنگام عادت ماهانهٔ خود نجس است.
3 Mvulana atatahiriwa siku ya nane.
روز هشتم، پسرش باید ختنه شود.
4 Kisha ni lazima huyo mwanamke asubiri kwa siku thelathini na tatu, ndipo atakaswe kutoka damu kwake. Hataruhusiwa kugusa kitu chochote kilicho kitakatifu au kuingia mahali patakatifu, mpaka siku za kutakaswa kwake zimetimia.
آن زن باید مدت سی و سه روز صبر کند تا از خونریزی خود کاملاً طاهر گردد. در این مدت او نباید به هیچ چیز مقدّس دست بزند و یا وارد خیمۀ ملاقات شود.
5 Kama akimzaa mtoto wa kike, mwanamke huyo atakuwa najisi kwa majuma mawili, kama wakati wake wa hedhi. Kisha atasubiri kwa siku sitini na sita, ndipo atatakaswa kutoka damu kwake.
هرگاه زنی دختری بزاید، آن زن تا دو هفته نجس خواهد بود همان‌گونه که به هنگام عادت ماهانهٔ خود نجس است. او باید شصت و شش روز صبر کند تا از خونریزی خود کاملاً طاهر شود.
6 “‘Siku zake za utakaso kwa ajili ya mwana au binti zitakapotimia, mwanamke huyo atamletea kuhani kwenye ingilio la Hema la Kukutania mwana-kondoo mwenye umri wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, na kinda la njiwa au hua kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
«وقتی مدت طهارت تمام شود، نوزاد، خواه پسر باشد خواه دختر، مادرش باید یک برهٔ یک ساله برای قربانی سوختنی و یک جوجه کبوتر یا قمری برای قربانی گناه تقدیم کند. این هدایا را باید دم در خیمۀ ملاقات نزد کاهن بیاورد.
7 Atavitoa mbele za Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yake, na kisha atakuwa safi kwa desturi ya ibada kutokana na kutokwa damu kwake. “‘Haya ndiyo masharti kwa ajili ya mwanamke atakayezaa mtoto wa kiume au wa kike.
کاهن آنها را برای خداوند قربانی نموده، برای مادر کفاره کند. آنگاه او از خونریزی زایمان طاهر خواهد شد. این است آنچه یک زن بعد از زایمان باید انجام دهد.
8 Kama huyo mwanamke hana uwezo wa kumpata mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa, moja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kwa njia hii, kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake, naye atakuwa safi.’”
ولی اگر آن زن فقیرتر از آن باشد که بتواند یک بره قربانی کند، می‌تواند دو قمری یا دو جوجه کبوتر بیاورد. یکی برای قربانی سوختنی و دیگری برای قربانی گناه. کاهن باید با تقدیم این قربانیها برایش کفاره کند تا دوباره طاهر شود.»

< Mambo ya Walawi 12 >