< Mambo ya Walawi 11 >
1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
And Jehovah speaketh unto Moses and unto Aaron, saying unto them,
2 “Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
'Speak unto the sons of Israel, saying, This [is] the beast which ye do eat out of all the beasts which [are] on the earth:
3 Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
any dividing a hoof, and cleaving the cleft of the hoofs, bringing up the cud, among the beasts, it ye do eat.
4 “‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
'Only, this ye do not eat — of those bringing up the cud, and of those dividing the hoof — the camel, though it is bringing up the cud, yet the hoof not dividing — it [is] unclean to you;
5 Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
and the rabbit, though it is bringing up the cud, yet the hoof it divideth not — unclean it [is] to you;
6 Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
and the hare, though it is bringing up the cud, yet the hoof hath not divided — unclean it [is] to you;
7 Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
and the sow, though it is dividing the hoof, and cleaving the cleft of the hoof, yet the cud it bringeth not up — unclean it [is] to you.
8 Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
'Of their flesh ye do not eat, and against their carcase ye do not come — unclean they [are] to you.
9 “‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
'This ye do eat of all which [are] in the waters; any one that hath fins and scales in the waters, in the seas, and in the brooks, them ye do eat;
10 Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
and any one that hath not fins and scales in the seas, and in the brooks, of any teeming creature of the waters, and of any creature which liveth, which [is] in the waters — an abomination they [are] to you;
11 Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
yea, an abomination they are to you; of their flesh ye do not eat, and their carcase ye abominate.
12 Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
'Any one that hath not fins and scales in the waters — an abomination it [is] to you.
13 “‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
'And these ye do abominate of the fowl; they are not eaten, an abomination they [are]: the eagle, and the ossifrage, and the ospray,
14 mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
and the vulture, and the kite after its kind,
every raven after its kind,
16 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
and the owl, and the night-hawk, and the cuckoo, and the hawk after its kind,
17 bundi, mnandi, bundi mkubwa,
and the little owl, and the cormorant, and the great owl,
and the swan, and the pelican, and the gier eagle,
19 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
and the stork, the heron after its kind, and the lapwing, and the bat.
20 “‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
'Every teeming creature which is flying, which is going on four — an abomination it [is] to you.
21 Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
'Only — this ye do eat of any teeming thing which is flying, which is going on four, which hath legs above its feet, to move with them on the earth;
22 Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
these of them ye do eat: the locust after its kind, and the bald locust after its kind, and the beetle after its kind, and the grasshopper after its kind;
23 Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
and every teeming thing which is flying, which hath four feet — an abomination it [is] to you.
24 “‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
'And by these ye are made unclean, any one who is coming against their carcase is unclean till the evening;
25 Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
and anyone who is lifting up [aught] of their carcase doth wash his garments, and hath been unclean till the evening: —
26 “‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
even every beast which is dividing the hoof, and is not cloven-footed, and the cud is not bringing up — unclean they [are] to you; any one who is coming against them is unclean.
27 Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
'And any one going on its paws, among all the beasts which are going on four — unclean they [are] to you; any one who is coming against their carcase is unclean until the evening;
28 Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
and he who is lifting up their carcase doth wash his garments, and hath been unclean until the evening — unclean they [are] to you.
29 “‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
'And this [is] to you the unclean among the teeming things which are teeming on the earth: the weasel, and the mouse, and the tortoise after its kind,
30 guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
and the ferret, and the chameleon, and the lizard, and the snail, and the mole;
31 Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
these [are] the unclean to you among all which are teeming; any one who is coming against them in their death is unclean till the evening.
32 Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
'And anything on which any one of them falleth, in their death, is unclean, of any vessel of wood or garment or skin or sack, any vessel in which work is done is brought into water, and hath been unclean till the evening, then it hath been clean;
33 Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
and any earthen vessel, into the midst of which [any] one of them falleth, all that [is] in its midst is unclean, and it ye do break.
34 Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
'Of all the food which is eaten, that on which cometh [such] water, is unclean, and all drink which is drunk in any [such] vessel is unclean;
35 Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
and anything on which [any] of their carcase falleth is unclean (oven or double pots), it is broken down, unclean they [are], yea, unclean they are to you.
36 Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
'Only — a fountain or pit, a collection of water, is clean, but that which is coming against their carcase is unclean;
37 Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
and when [any] of their carcase falleth on any sown seed which is sown — it [is] clean;
38 Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
and when water is put on the seed, and [any] of its carcase hath fallen on it — unclean it [is] to you.
39 “‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
'And when any of the beasts which are to you for food dieth, he who is coming against its carcase is unclean till the evening;
40 Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
and he who is eating of its carcase doth wash his garments, and hath been unclean till the evening; and he who is lifting up its carcase doth wash his garments, and hath been unclean till the evening.
41 “‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
'And every teeming thing which is teeming on the earth is an abomination, it is not eaten;
42 Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
any thing going on the belly, and any going on four, unto every multiplier of feet, to every teeming thing which is teeming on the earth — ye do not eat them, for they [are] an abomination;
43 Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
ye do not make yourselves abominable with any teeming thing which is teeming, nor do ye make yourselves unclean with them, so that ye have been unclean thereby.
44 Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
'For I [am] Jehovah your God, and ye have sanctified yourselves, and ye have been holy, for I [am] holy; and ye do not defile your persons with any teeming thing which is creeping on the earth;
45 Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
for I [am] Jehovah who am bringing you up out of the land of Egypt to become your God; and ye have been holy, for I [am] holy.
46 “‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
'This [is] a law of the beasts, and of the fowl, and of every living creature which is moving in the waters, and of every creature which is teeming on the earth,
47 Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”
to make separation between the unclean and the pure, and between the beast that is eaten, and the beast that is not eaten.'