< Mambo ya Walawi 11 >

1 Bwana akawaambia Mose na Aroni,
And the LORD spoke to Moses and to Aaron, saying to them,
2 “Waambieni Waisraeli: ‘Kati ya wanyama wote waishio juu ya nchi, hawa ndio mtakaowala:
Speak to the children of Israel, saying, These are the beasts which ye may eat among all the beasts that are on the earth.
3 Mwaweza kula mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika sehemu mbili na ambaye hucheua.
Whatever parteth the hoof, and is clovenfooted, and cheweth the cud, among the beasts, that shall ye eat.
4 “‘Kuna wanyama wengine ambao hucheua tu au wenye kwato zilizogawanyika tu, lakini hao kamwe msiwale. Ngamia ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; kwa kawaida ya ibada hiyo ni najisi kwenu.
Nevertheless these shall ye not eat of them that chew the cud, or of them that divide the hoof: the camel, because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean to you.
5 Pelele ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
And the coney, because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean to you.
6 Sungura ingawa hucheua hana kwato zilizogawanyika; huyo ni najisi kwenu.
And the hare, because he cheweth the cud, but divideth not the hoof; he is unclean to you.
7 Naye nguruwe ingawa anazo kwato zilizogawanyika sehemu mbili, hacheui; huyo ni najisi kwenu.
And the swine, though he divideth the hoof, and is clovenfooted, yet he cheweth not the cud; he is unclean to you.
8 Kamwe msile nyama yao wala kugusa mizoga yao; wao ni najisi kwenu.
Of their flesh shall ye not eat, and their carcase shall ye not touch; they are unclean to you.
9 “‘Kuhusu viumbe wote wanaoishi ndani ya maji ya bahari na vijito, mtakula wale wote wenye mapezi na magamba.
These shall ye eat of all that are in the waters: whatever hath fins and scales in the waters, in the seas, and in the rivers, them shall ye eat.
10 Lakini viumbe wote ndani ya bahari au vijito wasio na mapezi na magamba, wakiwa miongoni mwa makundi au viumbe wote ndani ya maji, hao ni machukizo kwenu.
And all that have not fins nor scales in the seas, and in the rivers, of all that move in the waters, and of any living creature which is in the waters, they shall be an abomination to you:
11 Nao watakuwa machukizo kwenu. Msile nyama yao, nayo mizoga yao itakuwa machukizo.
They shall be even an abomination to you; ye shall not eat of their flesh, but ye shall have their carcases in abomination.
12 Chochote kinachoishi ndani ya maji ambacho hakina mapezi na magamba kitakuwa chukizo kwenu.
Whatever hath no fins nor scales in the waters, that shall be an abomination to you.
13 “‘Wafuatao ndio ndege watakaokuwa machukizo kwenu, hivyo msiwale kwa sababu ni chukizo: tai, furukombe, kipungu,
And these are they which ye shall have in abomination among the fowls; they shall not be eaten, they are an abomination: the eagle, and the ossifrage, and the ospray,
14 mwewe mwekundu, aina zote za mwewe mweusi,
And the vulture, and the kite after his kind;
15 aina zote za kunguru,
Every raven after his kind;
16 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga, shakwe, aina zote za kipanga,
And the owl, and the night hawk, and the cuckow, and the hawk after his kind,
17 bundi, mnandi, bundi mkubwa,
And the little owl, and the cormorant, and the great owl,
18 mumbi, mwari, nderi,
And the swan, and the pelican, and the gier eagle,
19 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
And the stork, and the heron after her kind, and the lapwing, and the bat.
20 “‘Wadudu wote warukao ambao hutembea kwa miguu minne watakuwa chukizo kwenu.
All fowls that creep, going upon all four, shall be an abomination to you.
21 Lakini wako viumbe wenye mabawa ambao hutembea kwa miguu minne mtakaowala: wale wenye vifundo katika miguu yao ya kurukaruka juu ya ardhi.
Yet these may ye eat of every flying creeping thing that goeth upon all four, which have legs above their feet, to leap with upon the earth;
22 Miongoni mwa hawa, mtakula nzige wa aina zote, senene, parare au panzi.
Even these of them ye may eat; the locust after its kind, and the bald locust after its kind, and the beetle after its kind, and the grasshopper after its kind.
23 Lakini viumbe wengine wote wenye mabawa na wenye miguu minne ni machukizo kwenu.
But all other flying creeping things, which have four feet, shall be an abomination to you.
24 “‘Mtajinajisi kwa wanyama hawa. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
And for these ye shall be unclean: whoever toucheth the carcase of them shall be unclean until the evening.
25 Yeyote atakayebeba mizoga ya viumbe hawa ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
And whoever beareth any of the carcase of them shall wash his clothes, and be unclean until the evening.
26 “‘Kila mnyama mwenye ukwato ulioachana lakini haukugawanyika kabisa, au yule asiyecheua, huyo ni najisi kwenu; yeyote agusaye mzoga wowote wa hao atakuwa najisi.
The carcases of every beast which divideth the hoof, and is not clovenfooted, nor cheweth the cud, are unclean to you: every one that toucheth them shall be unclean.
27 Miongoni mwa wanyama wote watembeao kwa miguu minne, wale watembeao kwa vitanga vyao ni najisi kwenu; yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
And whatever goeth upon its paws, among all manner of beasts that go on all four, those are unclean to you: whoever toucheth their carcase shall be unclean until the evening.
28 Yeyote atakayebeba mizoga yao ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Wanyama hawa ni najisi kwenu.
And he that beareth the carcase of them shall wash his clothes, and be unclean until the evening: they are unclean to you.
29 “‘Kuhusu wanyama watambaao juu ya ardhi, hawa ni najisi kwenu: kicheche, panya, aina yoyote ya mijusi mikubwa,
These also shall be unclean to you among the creeping things that creep upon the earth; the weasel, and the mouse, and the tortoise after its kind,
30 guruguru, kenge, mijusi ya ukutani, goromoe na kinyonga.
And the ferret, and the chameleon, and the lizard, and the snail, and the mole.
31 Hao wote watambaao juu ya ardhi ni najisi kwenu. Yeyote agusaye mizoga yao atakuwa najisi mpaka jioni.
These are unclean to you among all that creep: whoever doth touch them, when they are dead, shall be unclean until the evening.
32 Ikiwa mmoja wao atakufa na kuangukia juu ya kitu fulani, chombo hicho, hata kikiwa cha matumizi gani, kitakuwa najisi, kiwe kimetengenezwa kwa mti, nguo, ngozi au gunia. Kiweke ndani ya maji; kitakuwa najisi mpaka jioni, kisha kitakuwa safi tena.
And upon whatever any of them, when they are dead, doth fall, it shall be unclean; whether it is any vessel of wood, or raiment, or skin, or sack, whatever vessel it is, in which any work is done, it must be put into water, and it shall be unclean until the evening; so it shall be cleansed.
33 Ikiwa mmoja wa wanyama aliyekufa ataangukia ndani ya chungu, kila kilichomo katika chungu hicho kitakuwa najisi, nawe ni lazima uvunje chungu hicho.
And every earthen vessel, into which any of them falleth, whatever is in it shall be unclean; and ye shall break it.
34 Chakula chochote ambacho chaweza kuliwa lakini kikawa kimeingia maji kutoka kwenye chungu hicho ni najisi, na kitu chochote cha majimaji ambacho chaweza kunyweka kutoka kwenye chungu hicho ni najisi.
Of all food which may be eaten, that on which such water cometh shall be unclean: and all drink that may be drunk in every such vessel shall be unclean.
35 Chochote ambacho mzoga wa mmojawapo utaangukia kitakuwa najisi. Jiko au chungu cha kupikia ni lazima kivunjwe. Ni najisi, nawe ni lazima uvihesabu kuwa najisi.
And every thing on which any part of their carcase falleth shall be unclean; whether an oven, or ranges for pots, they shall be broken down: for they are unclean, and shall be unclean to you.
36 Lakini chemchemi au kisima, mahali pa kuchota maji, patakuwa safi, lakini yeyote atakayegusa moja ya mizoga hii ni najisi.
Nevertheless a fountain or pit, in which there is plenty of water, shall be clean: but that which toucheth their carcase shall be unclean.
37 Kama mzoga ukianguka juu ya mbegu zozote ambazo ni za kupanda, zinabaki safi.
And if any part of their carcase shall fall upon any sowing seed which is to be sown, it shall be clean.
38 Lakini kama mbegu imetiwa maji na mzoga ukaanguka juu yake, hiyo mbegu ni najisi kwenu.
But if any water shall be put upon the seed, and any part of their carcase shall fall on it, it shall be unclean to you.
39 “‘Kama mnyama ambaye mnaruhusiwa kumla akifa, yeyote atakayeugusa mzoga wake atakuwa najisi mpaka jioni.
And if any beast, of which ye may eat, shall die; he that toucheth its carcase shall be unclean until the evening.
40 Yeyote atakayekula sehemu ya mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni. Yeyote atakayebeba mzoga huo ni lazima afue nguo zake, naye atakuwa najisi mpaka jioni.
And he that eateth of its carcase shall wash his clothes, and be unclean until the evening: he also that beareth its carcase shall wash his clothes, and be unclean until the evening.
41 “‘Kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi ni chukizo; kisiliwe.
And every creeping thing that creepeth upon the earth shall be an abomination; it shall not be eaten.
42 Msile kiumbe chochote kitambaacho juu ya ardhi, kiwe kitambaacho kwa tumbo lake, au kitambaacho kwa miguu minne au kwa miguu mingi; ni chukizo.
Whatever goeth upon the belly, and whatever goeth upon all four, or whatever hath many feet among all creeping things that creep upon the earth, them ye shall not eat; for they are an abomination.
43 Msijitie unajisi kwa chochote katika viumbe hivi. Msijitie unajisi kwa viumbe hivyo au kutiwa unajisi navyo.
Ye shall not make yourselves abominable with any creeping thing that creepeth, neither shall ye make yourselves unclean with them, that ye should be defiled by them.
44 Mimi ndimi Bwana Mungu wenu; jitakaseni mwe watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu. Msijitie unajisi wenyewe kwa kiumbe chochote kile kiendacho juu ya ardhi.
For I am the LORD your God: ye shall therefore sanctify yourselves, and ye shall be holy; for I am holy: neither shall ye defile yourselves with any manner of creeping thing that creepeth upon the earth.
45 Mimi ndimi Bwana niliyewapandisha mtoke Misri ili niwe Mungu wenu. Kwa hiyo kuweni watakatifu kwa sababu Mimi ni mtakatifu.
For I am the LORD that bringeth you out of the land of Egypt, to be your God: ye shall therefore be holy, for I am holy.
46 “‘Haya ndiyo masharti kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe hai kiendacho ndani ya maji, na kila kiumbe kiendacho juu ya ardhi.
This is the law of the beasts, and of the fowl, and of every living creature that moveth in the waters, and of every creature that creepeth upon the earth:
47 Ni lazima mpambanue kati ya kilicho najisi na kilicho safi, kati ya viumbe hai vinavyoweza kuliwa na vile visivyoweza kuliwa.’”
To make a difference between the unclean and the clean, and between the beast that may be eaten and the beast that may not be eaten.

< Mambo ya Walawi 11 >