< Mambo ya Walawi 10 >

1 Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
Nadab et Abihu, fils d'Aaron, prirent chacun leur brasier, y mirent du feu, y déposèrent du parfum, et offrirent devant l'Éternel un feu étranger qu'il ne leur avait pas ordonné.
2 Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
Le feu sortit de devant l'Éternel, les dévora, et ils moururent devant l'Éternel.
3 Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
Moïse dit alors à Aaron: « C'est ce dont Yahvé a parlé, en disant, Je me montrerai saint pour ceux qui s'approchent de moi, et devant tout le peuple, je serai glorifié. » Aaron se tut.
4 Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
Moïse appela Mischaël et Elzaphan, fils d'Uzziel, oncle d'Aaron, et leur dit: « Approchez, portez hors du camp vos frères qui sont devant le sanctuaire. »
5 Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
Ils s'approchèrent donc et les transportèrent dans leurs tuniques hors du camp, comme Moïse l'avait dit.
6 Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
Moïse dit à Aaron, à Eléazar et à Ithamar, ses fils: « Ne laissez pas tomber les cheveux de vos têtes et ne déchirez pas vos vêtements, afin que vous ne mouriez pas et qu'il ne s'irrite pas contre toute l'assemblée; mais que vos frères, toute la maison d'Israël, se lamentent sur le feu que Yahvé a allumé.
7 Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
Tu ne sortiras pas de l'entrée de la tente de la Rencontre, de peur de mourir, car l'huile d'onction de l'Éternel est sur toi. » Ils firent selon la parole de Moïse.
8 Kisha Bwana akamwambia Aroni,
Puis Yahvé dit à Aaron:
9 “Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
« Toi et tes fils, vous ne boirez ni vin ni boisson forte chaque fois que vous entrerez dans la Tente de la Rencontre, sinon vous mourrez. Ceci sera une loi pour toujours, de génération en génération.
10 Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
Tu feras la distinction entre ce qui est saint et ce qui est commun, entre ce qui est impur et ce qui est pur.
11 na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
Tu enseigneras aux enfants d'Israël toutes les lois que l'Éternel leur a dites par Moïse. »
12 Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
Moïse parla à Aaron, à Éléazar et à Ithamar, ses fils qui étaient restés: Prenez l'offrande qui reste des sacrifices consumés par le feu devant l'Éternel, et mangez-la sans levure à côté de l'autel, car elle est très sainte.
13 Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
Vous la mangerez dans un lieu saint, car c'est votre part et la part de vos fils des sacrifices consumés par le feu devant l'Éternel; c'est ce que je vous ordonne.
14 Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
Vous mangerez la poitrine ondulée et la cuisse levée dans un lieu pur, toi, tes fils et tes filles avec toi, car elles sont données comme votre part et la part de vos fils, dans les sacrifices d'actions de grâces des enfants d'Israël.
15 Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
Ils apporteront la cuisse levée et la poitrine agitée, avec les offrandes consumées par le feu de la graisse, pour l'agiter en sacrifice par élévation devant l'Éternel. Ce sera votre part, et celle de vos fils avec vous, comme une part pour toujours, comme Yahvé l'a ordonné. »
16 Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
Moïse s'enquit du bouc du sacrifice pour le péché, et voici qu'il était brûlé. Moïse se mit en colère contre Éléazar et Ithamar, les fils d'Aaron qui restaient, et dit:
17 “Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
« Pourquoi n'avez-vous pas mangé le sacrifice pour le péché dans le lieu du sanctuaire, puisqu'il est très saint et qu'il vous a été donné de porter l'iniquité de l'assemblée, afin de faire l'expiation pour elle devant Yahvé?
18 Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
Voici, son sang n'a pas été apporté dans l'intérieur du sanctuaire. Vous auriez certainement dû le manger dans le sanctuaire, comme je l'ai ordonné. »
19 Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
Aaron dit à Moïse: « Voici, ils ont offert aujourd'hui leur sacrifice pour le péché et leur holocauste devant l'Éternel, et il m'est arrivé des choses comme celles-là. Si j'avais mangé aujourd'hui le sacrifice pour le péché, cela aurait-il été agréable aux yeux de Yahvé? ».
20 Mose aliposikia haya, akaridhika.
Lorsque Moïse entendit cela, cela lui plut.

< Mambo ya Walawi 10 >