< Mambo ya Walawi 1 >
1 Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
Gospod je zaklical k Mojzesu in mu spregovoril iz šotorskega svetišča skupnosti, rekoč:
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
»Spregovori Izraelovim otrokom in jim reci: ›Če katerikoli človek izmed vas prinese dar Gospodu, boste prinesli svojo daritev izmed živine, od tropa in od črede.
3 “‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
Če bo njegov dar žgalna daritev od črede, naj daruje samca brez pomanjkljivosti. Daroval ga bo iz svoje lastne prostovoljne volje pri vratih šotorskega svetišča skupnosti pred Gospodom.
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Svojo roko bo položil na glavo žgalne daritve in ta bo sprejeta zanj, da opravi spravo zanj.
5 Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
Bikca bo zaklal pred Gospodom in duhovniki, Aronovi sinovi, bodo prinesli kri in kri poškropili naokoli nad oltarjem, ki je pri vratih šotorskega svetišča skupnosti.
6 Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
Žgalno daritev bo odrl in jo razrezal na koščke.
7 Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
Sinovi duhovnika Arona bodo na oltar položili ogenj in po vrsti na ogenj položili les.
8 Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
Duhovniki, Aronovi sinovi, bodo položili dele, glavo in tolščo, po vrsti na les, ki je na ognju, ki je na oltarju,
9 Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
toda njegovo drobovino in njegove noge bo umil v vodi. Duhovnik bo vse sežgal na oltarju, da bo žgalna daritev, ognjena daritev, prijetnega vonja Gospodu.
10 “‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
Če bo njegov dar za žgalno daritev od tropov, namreč od ovc ali od koz, bo privedel samca brez pomanjkljivosti.
11 Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
Zaklal ga bo na severni strani oltarja pred Gospodom. Duhovniki, Aronovi sinovi, bodo njegovo kri poškropili naokoli nad oltarjem.
12 Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
Razrezal ga bo na koščke, z njegovo glavo in njegovo tolščo. Duhovnik jih bo po vrsti položil na les, ki je na ognju, ki je na oltarju,
13 Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
toda drobovje in noge bo umil z vodo. Duhovnik bo vse to prinesel in to sežgal na oltarju. To je žgalna daritev, ognjena daritev, prijetnega vonja Gospodu.
14 “‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
Če bo žgalna daritev za njegov dar Gospodu od perjadi, potem bo svojo daritev prinesel od grlic ali od mladih golobov.
15 Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
Duhovnik bo to prinesel na oltar in ji odščipnil vrat in jo sežgal na oltarju; in njena kri bo iztisnjena ob strani oltarja.
16 Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
Njeno golšo bo odtrgal z njenimi peresi in jo odvrgel na vzhodnem delu, poleg oltarja, ob kraju za pepel
17 Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
in nalomi jo s perutmi, toda ne bo je ločil narazen. Duhovnik bo to sežgal na oltarju, na lesu, ki je na ognju. To je žgalna daritev, ognjena daritev, prijetnega vonja Gospodu.‹«