< Mambo ya Walawi 1 >

1 Bwana akamwita Mose na kusema naye kutoka kwenye Hema la Kukutania, akamwambia,
Yahvé appela Moïse et lui parla depuis la tente d'assignation, en disant:
2 “Sema na Waisraeli na uwaambie, ‘Yeyote miongoni mwenu aletapo sadaka ya mnyama kwa Bwana, alete mnyama kama sadaka yake kutoka kundi lake la ngʼombe au la kondoo na mbuzi.
Parle aux enfants d'Israël et dis-leur: « Quand quelqu'un d'entre vous présentera une offrande à Yahvé, il offrira une offrande de bétail, du gros et du menu bétail.
3 “‘Kama sadaka hiyo ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la ngʼombe, atamtoa ngʼombe dume asiye na dosari. Ni lazima amlete kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili aweze kukubalika kwa Bwana.
"'Si son offrande est un holocauste de bétail, il offrira un mâle sans défaut. Il l'offrira à l'entrée de la Tente d'assignation, afin qu'il soit agréé devant Yahvé.
4 Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka ya kuteketezwa, nayo itakubaliwa kwa niaba yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake.
Il posera sa main sur la tête de l'holocauste, et celui-ci sera agréé pour lui, afin qu'il fasse l'expiation.
5 Atamchinja yule fahali mchanga mbele za Bwana, kisha wana wa Aroni walio makuhani wataleta damu na kuinyunyiza pande zote za madhabahu yaliyo penye ingilio la Hema la Kukutania.
Il égorgera le taureau devant Yahvé. Les fils d'Aaron, les prêtres, présenteront le sang et en feront l'aspersion tout autour de l'autel qui est à l'entrée de la tente de la Rencontre.
6 Ataichuna hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikata vipande vipande.
Il dépouillera l'holocauste et le coupera en morceaux.
7 Wana wa Aroni kuhani wataweka moto juu ya madhabahu na kupanga kuni juu ya huo moto.
Les fils du sacrificateur Aaron mettront du feu sur l'autel et poseront du bois en ordre sur le feu;
8 Kisha wana wa Aroni walio makuhani watapanga vile vipande vya nyama, pamoja na kichwa na mafuta ya huyo mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
et les fils d'Aaron, les sacrificateurs, poseront les morceaux, la tête et la graisse en ordre sur le bois qui est sur le feu, sur l'autel;
9 Ataziosha sehemu za ndani na miguu yake kwa maji, naye kuhani atavichoma vyote juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, yenye harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
mais il lavera à l'eau les entrailles et les jambes. Le prêtre brûlera tout cela sur l'autel, comme holocauste, une offrande consumée par le feu, d'une odeur agréable à Yahvé.
10 “‘Kama sadaka ni ya kuteketezwa kutoka kwenye kundi la kondoo au mbuzi, atamtoa mnyama dume asiye na dosari.
"'Si son offrande provient du troupeau, des brebis ou des chèvres, pour un holocauste, il offrira un mâle sans défaut.
11 Atamchinjia upande wa kaskazini wa madhabahu mbele za Bwana, nao wana wa Aroni walio makuhani watanyunyizia damu yake pande zote za madhabahu.
Il l'égorgera sur le côté nord de l'autel, devant Yahvé. Les fils d'Aaron, les prêtres, en répandront le sang tout autour de l'autel.
12 Atamkata vipande vipande, naye kuhani atavipanga, pamoja na kichwa na mafuta ya mnyama juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu.
Il le coupera en morceaux, avec sa tête et sa graisse. Le prêtre les disposera en ordre sur le bois qui est sur le feu, sur l'autel,
13 Ataosha sehemu za ndani na miguu kwa maji, naye kuhani atavileta vyote na kuvichoma juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
mais il lavera à l'eau les entrailles et les pattes. Le prêtre offrira le tout et le brûlera sur l'autel. C'est un holocauste, une offrande consumée par le feu, d'une odeur agréable à Yahvé.
14 “‘Kama sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwa Bwana ni ndege, atamtoa hua au kinda la njiwa.
"'Si son offrande à Yahvé est un holocauste d'oiseaux, il offrira son offrande de tourterelles ou de jeunes pigeons.
15 Kuhani atamleta kwenye madhabahu, naye atamvunja shingo na kumnyofoa kichwa na kumchoma juu ya madhabahu. Damu yake itachuruzishwa ubavuni mwa madhabahu.
Le prêtre l'amènera à l'autel, il lui essorera la tête et la brûlera sur l'autel; son sang se répandra sur le côté de l'autel;
16 Ataondoa kifuko cha chakula pamoja na uchafu wake na kuvitupa upande wa mashariki wa madhabahu, mahali pale penye majivu.
il enlèvera son jabot et ses plumes et les jettera à côté de l'autel, à l'orient, à la place des cendres.
17 Atampasua na kumweka wazi katika mabawa yake, lakini asimwachanishe kabisa, kisha kuhani ataichoma juu ya zile kuni zinazowaka juu ya madhabahu. Hii ni sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
Il la déchirera par les ailes, mais il ne la séparera pas. Le prêtre la brûlera sur l'autel, sur le bois qui est sur le feu. C'est un holocauste, un sacrifice consumé par le feu, d'une odeur agréable à Yahvé.

< Mambo ya Walawi 1 >