< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
Mint maradt magánosan a város, a népben bővelkedő! Olyan lett mint özvegy; aki nagy volt a nemzetek közt, úrnő az országok közt, robotolóvá lett!
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
Sírva sír az éjszakában s könnye az orczáján, nincs vigasztalója néki mind a szeretői közt, mind a barátai hűtelenek hozzá, lettek neki ellenségeivé.
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
Elbujdosott Jehúda az inség és nagy szolgaság miatt; leült a nemzetek közt, nyugalmat nem talált; mind az üldözői utólérték őt a szorosok közepette.
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
Czión útjai gyászosak, ünnepre érkezők hián, mind a kapui elpusztulva, papjai sóhajtanak, hajadonai bánkódók s ő – keserve van.
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
Szorongatói fejjé lettek, ellenségei boldogok, mert az Örökkévaló megbúsította sok bűntette miatt, kisdedei foglyul mentek a szorongató előtt.
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
Eltűnt Czión leányától minden ékessége; olyanok lettek nagyjai mint a szarvasok, melyek legelőt nem találtak, s mentek erőtlenül az üldöző előtt.
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
Megemlékezett Jeruzsálem nyomorúsága és hontalansága napjaiban mind a drágaságairól, melyek voltak a hajdan napjaitól fogva; midőn népe szorongatónak kezébe esett, s nem volt segítője, látták őt a szorongatók, nevettek elenyésztén.
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
Vétket vétett Jeruzsálem, azért lett fertőzetté; mind a tisztelői lekicsinyelték, mert látták meztelenségét, sóhajtott is ő és hátrafordult.
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
Tisztátalansága az uszályain, nem gondolt végére, csodálatosan hanyatlott, nincs neki vigasztalója: lásd, Örökkévaló, nyomorúságomat, mert fennhéjázott az ellenség!
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
Kezét vetette rá a szorongató mind a drágaságaira; bizony látott bemenni szentélyébe nemzeteket, melyekről parancsoltad: ne jussanak be a te gyülekezetedbe!
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
Mind az emberei sóhajtanak, kenyeret koldulnak, odaadták drágaságaikat ételért, hogy lelküket üdíthessék; lásd, Örökkévaló, és tekintsd, hogy lekicsinyelt vagyok!
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
Ne nektek, ti úton járók mind! Tekintsetek ide és lássátok: van-a fájdalom mint az én fájdalmam, mely nekem okoztatott, kit megbúsított az Örökkévaló, haragja föllobbanásának napján?
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
Magasból küldött tüzet csontjaimba és gyötörte őket; hálót terített lábaimnak, hátra vetett engem, tett engem pusztulttá, egész napon sínylővé.
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
Összerovatott keze által bűn tetteim járma, egybefonódnak, nyakamra szállnak, elgyengítette erőmet; odaadott engem az Úr olyannak kezeibe, ki előtt nem állhatok meg.
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
Elvette az Úr mind az erőseimet én bennem, hirdetett ellenem gyülekezést, hogy megtörje ifjaimat, prést tiprott az Úr Jehúda a szűz leányának.
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
Ezek miatt sirok én, szemem, víztől folyik szét, mert távol van tőlem vigasztaló, lelkemet üdítő; lettek fiaim pusztultakká, hogy győzelmeskedett az ellenség.
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
Kitárta Czión a kezeit, nincs neki vigasztalója, Jákóbra rendelte az Örökkévaló körülötte szorongatóit; lett Jeruzsálem fertőzetté közöttük.
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
Igazságos ő, az Örökkévaló, mert parancsa iránt engedetlen voltam; halljátok csak, oh népek mind és lássátok fájdalmamat: hajadonaim és ifjaim fogságba mentek.
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
Hívtam szeretőimet, ők megcsaltak engem, papjaim és véneim a városban múltak ki; mert ételt kerestek maguknak, hogy felüdíthessék lelköket.
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
Lásd, Örökkévaló, hogy megszorúltam, beleim megtüzesedtek, megfordult szívem én bennem, mert fölötte engedetlen voltam; kivülről öldös a kard, a házban mintha halál volna.
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
Hallották, hogy sóhajtok, nincs nekem vigasztalóm, ellenségeim mind hallották veszedelmemet, örvendeztek, hogy te cselekedted; ha majd elhoztad a napot, melyet hirdettél, olyanok lesznek mint én!
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
Jusson minden rosszaságuk te eléd, s bánj velök, amint velem bántál mind a bűntetteim miatt; mert sok a sóhajtásom és sínylő a szivem.

< Maombolezo 1 >