< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
how? to dwell isolation [the] city many people to be like/as widow (many *L(abh)*) in/on/with nation princess in/on/with province to be to/for taskworker
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
to weep to weep in/on/with night and tears her upon jaw her nothing to/for her to be sorry: comfort from all to love: lover her all neighbor her to act treacherously in/on/with her to be to/for her to/for enemy
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
to reveal: remove Judah from affliction and from abundance service he/she/it to dwell in/on/with nation not to find resting all to pursue her to overtake her between: among [the] terror
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
way: road Zion mourning from without to come (in): come meeting: festival all gate her be desolate: destroyed priest her to sigh virgin her to suffer and he/she/it to provoke to/for her
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
to be enemy her to/for head: leader enemy her to prosper for LORD to suffer her upon abundance transgression her infant her to go: went captivity to/for face: before enemy
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
and to come out: come (from from daughter *Q(K)*) Zion all glory her to be ruler her like/as deer not to find pasture and to go: went in/on/with not strength to/for face: before to pursue
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
to remember Jerusalem day affliction her and wandering her all desirable her which to be from day front: old in/on/with to fall: fall people her in/on/with hand: power enemy and nothing to help to/for her to see: see her enemy to laugh upon annihilation her
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
sin to sin Jerusalem upon so to/for filth to be all to honor: honour her to lavish/despise her for to see: see nakedness her also he/she/it to sigh and to return: repent back
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
uncleanness her in/on/with hem her not to remember end her and to go down wonder nothing to be sorry: comfort to/for her to see: see LORD [obj] affliction my for to magnify enemy
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
hand his to spread enemy upon all desire her for to see: see nation to come (in): come sanctuary her which to command not to come (in): come in/on/with assembly to/for you
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
all people her to sigh to seek food: bread to give: give (desire their *Q(K)*) in/on/with food to/for to return: rescue soul: life to see: see LORD and to look [emph?] for to be be vile
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
not to(wards) you all to pass way: journey to look and to see: see if there pain like/as pain my which to abuse to/for me which to suffer LORD in/on/with day burning anger face: anger his
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
from height to send: depart fire in/on/with bone my and to rule her to spread net to/for foot my to return: return me back to give: make me devastated all [the] day sick
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
to bind yoke transgression my in/on/with hand his to intertwine to ascend: establish upon neck my to stumble strength my to give: give me Lord in/on/with hand: power not be able to arise: establish
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
to reject all mighty: strong my Lord in/on/with entrails: among my to call: call to upon me meeting to/for to break youth my wine press to tread Lord to/for virgin daughter Judah
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
upon these I to weep eye my eye my to go down water for to remove from me to be sorry: comfort to return: rescue soul my to be son: child my be desolate: destroyed for to prevail enemy
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
to spread Zion in/on/with hand her nothing to be sorry: comfort to/for her to command LORD to/for Jacob around: neighours him enemy his to be Jerusalem to/for impurity between them
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
righteous he/she/it LORD for lip: word his to rebel to hear: hear please all ([the] people *Q(K)*) and to see: see pain my virgin my and youth my to go: went in/on/with captivity
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
to call: call to to/for to love: lover me they(masc.) to deceive me priest my and old: elder my in/on/with city to die for to seek food to/for them and to return: rescue [obj] soul: life their
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
to see: see LORD for distress to/for me belly my to aggitate to overturn heart my in/on/with entrails: among my for to rebel to rebel from outside be bereaved sword in/on/with house: home like/as death
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
to hear: hear for to sigh I nothing to be sorry: comfort to/for me all enemy my to hear: hear distress: harm my to rejoice for you(m. s.) to make: do to come (in): bring day to call: call out and to be like me
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
to come (in): come all distress: evil their to/for face: before your and to abuse to/for them like/as as which to abuse to/for me upon all transgression my for many sighing my and heart my faint

< Maombolezo 1 >