< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
HOW DOTH the city sit solitary, that was full of people! How is she become as a widow! She that was great among the nations, and princess among the provinces, how is she become tributary!
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
She weepeth sore in the night, and her tears are on her cheeks; she hath none to comfort her among all her lovers; all her friends have dealt treacherously with her, they are become her enemies.
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
Judah is gone into exile because of affliction, and because of great servitude; she dwelleth among the nations, she findeth no rest; all her pursuers overtook her within the straits.
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
The ways of Zion do mourn, because none come to the solemn assembly; all her gates are desolate, her priests sigh; her virgins are afflicted, and she herself is in bitterness.
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
Her adversaries are become the head, her enemies are at ease; for the LORD hath afflicted her for the multitude of her transgressions; her young children are gone into captivity before the adversary.
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
And gone is from the daughter of Zion all her splendour; her princes are become like harts that find no pasture, and they are gone without strength before the pursuer.
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
Jerusalem remembereth in the days of her affliction and of her anguish all her treasures that she had from the days of old; now that her people fall by the hand of the adversary, and none doth help her, the adversaries have seen her, they have mocked at her desolations.
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
Jerusalem hath grievously sinned, therefore she is become as one unclean; all that honoured her despise her, because they have seen her nakedness; she herself also sigheth, and turneth backward.
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
Her filthiness was in her skirts, she was not mindful of her end; therefore is she come down wonderfully, she hath no comforter. 'Behold, O LORD, my affliction, for the enemy hath magnified himself.'
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
The adversary hath spread out his hand upon all her treasures; for she hath seen that the heathen are entered into her sanctuary, concerning whom Thou didst command that they should not enter into Thy congregation.
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
All her people sigh, they seek bread; they have given their pleasant things for food to refresh the soul. 'See, O LORD, and behold, how abject I am become.'
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
'Let it not come unto you, all ye that pass by! Behold, and see if there be any pain like unto my pain, which is done unto me, wherewith the LORD hath afflicted me in the day of His fierce anger.
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
From on high hath He sent fire into my bones, and it prevaileth against them; He hath spread a net for my feet, He hath turned me back; He hath made me desolate and faint all the day.
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
The yoke of my transgressions is impressed by His hand; they are knit together, they are come up upon my neck; He hath made my strength to fail; the Lord hath delivered me into their hands, against whom I am not able to stand.
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
The Lord hath set at nought all my mighty men in the midst of me; He hath called a solemn assembly against me to crush my young men; the Lord hath trodden as in a winepress the virgin the daughter of Judah.'
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
'For these things I weep; mine eye, mine eye runneth down with water; because the comforter is far from me, even he that should refresh my soul; my children are desolate, because the enemy hath prevailed.'
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
Zion spreadeth forth her hands; there is none to comfort her; the LORD hath commanded concerning Jacob, that they that are round about him should be his adversaries; Jerusalem is among them as one unclean.
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
'The LORD is righteous; for I have rebelled against His word; hear, I pray you, all ye peoples, and behold my pain: my virgins and my young men are gone into captivity.
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
I called for my lovers, but they deceived me; my priests and mine elders perished in the city, while they sought them food to refresh their souls.
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
Behold, O LORD, for I am in distress, mine inwards burn; my heart is turned within me, for I have grievously rebelled. Abroad the sword bereaveth, at home there is the like of death.
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
They have heard that I sigh, there is none to comfort me; all mine enemies have heard of my trouble, and are glad, for Thou hast done it; Thou wilt bring the day that Thou hast proclaimed, and they shall be like unto me.
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
Let all their wickedness come before Thee; and do unto them, as Thou hast done unto me for all my transgressions; for my sighs are many and my heart is faint.'

< Maombolezo 1 >