< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
Phatkhat mi ana dimsetna Jerusalem khopi chu tunvang kho gem a sodoh tai. Chitin namtin laha ana minthang khopi chu tunvang meithai a sodoh tan ahi. Vannoi leiset lengnu dinmun ana lo chu tunvang soh dinmun alo jotai.
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
Jan khovah vah'in mitlhi long chutchut in akap in ana ngailu cheng holah a jong alhamon ding aum tapouvin aloi agol chengse la aheodah leh adou gal in apang gam tauvin ahi.
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
Galhingin Judah akai taovin soh channa leh engbolna athoh tan ahi. Gam dang nammite laha achengun kicholdona mun amujou pouvin ahi. Agalmite uvin a umkimvel’un jamdoh thei louvin akoichah tauve.
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
Jerusalem lampiho akhul lhatan koi macha Pathen houna kin bol dingin ahung doh tapouvin, khopi kotpihola donlouvin aumgamtan athempu hou akhoisa gam tauvin anungah khangthah teu akhankho diu gelnan akap gam tauve.
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
A sugenthei houhi a Pakaiyun apang un ajalou teuchu akhantou tul tul jengun ahi. Pakaiyin achonset jih uva Jerusalem chu aengbol uva achateo galhinga kiman a gamla tah’a kikaimang gamu ahitauve.
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
Jerusalem khopi, ahoinale aloupina chu amang thah ahi tai. Alamkaiteu jong neh ding ham hing mu joulou sakhigol toh abang gam tauvin, agalmiteo masanga jam doh nading tha jong anei jou tapouve.
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
Lung lengvaija Jerusalem avale laitahin, tumasanga aphatlai nikho agel doh’e. Tunla agalmite khutnoija aum tan koimacha apanhu ding aum tapoi. Agalmiteuvin ajep lhu’uvin alhu ho chu aveuvin anuisat’un ahi.
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
Achonset behseh jeh'in Jerusalem ponse bangin paimangin aumtan. Tumasanga anagel thupi hon, tuhin anoisetauve, ajehchu aponu kiho-lhah peha jumle jachat thoha um ahitaove. Hijeh chun hahdoh ngamlou hella khoisa jing jenga um ahitai.
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
Amaho hin a khonung diu kigel phah louhelin jonthanhoina in akisuhboh uve. Amaho a kemsuh jing tauvin, a lhamon diu aphong ding diu koima aum tapoi. Pakai ka hahsetnao nei vetpehun tin akap tauve.
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
Galmiten ajokhophelun anei jouseu akichom tauve. Pakaiyin a Hou-in sunga lut dia anaphallou nam dangte chun ahouin sungu asuh boh pehu chu amudoh tauvin ahi.
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
Amiteu nehding hollin apeng jen jun tauvin, a hinjouna diuvin anei agouvu ajohdohun, vo Pakai neihin veuvin e-chan geija thet le kidah’a ka um’u hitam tin akap tauve.
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
Vo chele vahle, hilang hin hopa ho hiche thilsoh hi ija na gellou u-ham? Pathenin ka chunguva alunghan abuhlhah nale eibol gimnau hi vetem uvin.
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
Aman vanna konin meikong ahin sep lhan kagu kachang’u ahalgo tai. Aman ka lampi uva thang a kamin eile hoitauve. Aman eichom thengselun nilhum lhumin hahsatna eithoh sahun ahi.
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
Ka chonsetnao khaovin eikanun sohchanna nam kolin eihenun ahi. Pakaiyin katha’u eisuh ngoi pehun kagal miteu komah eipedohun akhutuva chatmon ka um taove.
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
Pakaiyin kalah'uva um kami hatteu thaneina asulhan kakhang thahteo suhmangna dingin galmite amangchan ahi, Pakaiyin lengpithei chilna akisuhchip bangin akhopi hoitah chu a suchip tan ahi.
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
Hicheho jouse jeh'in kakapin kamitlhi kamaija alonglha jenjung jingin ahinlah koima eilhamon ding le eitilhembi ding aum pon ahi. Galmiten eijou khup del tauvin, kakhang thahte’u khonung ding jong abing tan ahi.
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
Jerusalemin panpi ngaiyin akhut alhang dohin ahinlah apanpi ding amu joupoi. Pakaiyin Ami Isrealte chunga, aheng akom ho chu agalmi asohdoh pehhan! Ama ho hi ponse banga paimanga um ahitai.
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
Jerusalemin aseiyin Pakai hi adih’e, ajeh chu keiman ama dounan na kana tong’e, chitin namtinin ka thusei hi neingai pehun, ka thoh gimna hi neihet pehun, ka chanute’u leh ka chapate’u khol gamla taha galhingin eikaimang peh tauve.
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
Keiman kaloi kagolte koma kithopina kathumin amahonla eingai peh pouve. Ka themputeu leh ka lamkaiteu khopi sung’a kelin athi gam tauve, ahinkhou kihuhdohna ding aholun amu jou pove.
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
Pakai kalung lengvaina neivetpehin, ka chonset jeh'in ka lungthim ahesoh’e, kholai dung’a kitha tona aumin insung lang’a thilong aki jam’e.
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
Ka lung gim ka khoisatna mitam tahin eijah pehin ahinlah koima chan eihung lhamon pon ahi. Ka galmiten kathoh gimna ajah phatun Pakai nangin neibolnao hi akipa piuvin ahi. Oh Pakai keiho thoh tobang banga amaho nathohsah dinga naseipihnao nikhochu lhunsah loiyin.
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
Pakai ka chonsetnao jeh'a nei engbol bangu chun amahon eibolsetnao hi venlang amahojong engbolin. Ka lengvainao hi atamvalin ka lungthim sung’u asuna lheh jeng’e.

< Maombolezo 1 >