< Maombolezo 5 >
1 Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
ヱホバよ我らにありし所の事をおもひたまへ 我らの恥辱をかへりみ觀たまへ
2 Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
われらの産業は外國人に歸し われらの家屋は他國人の有となれり
3 Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
われらは孤子となりて父あらず われらの母は寡婦にひとし
4 Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
われらは金を出して自己の水を飮み おのれの薪を得るにも價をはらふ
5 Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
われらを追ふ者われらの頸に迫る 我らは疲れて休むことを得ず
6 Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
食物を得て饑を凌がんとてエジプト人およびアッスリヤ人に手を與へたり
7 Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
われらの父は罪ををかして已に世にあらず 我らその罪を負ふなり
8 Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
奴僕等われらを制するに誰ありて我らを之が手よりすくひ出すものなし
9 Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
荒野の刀兵の故によりて我ら死を冒して食物を得
10 Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
饑饉の烈しき熱氣によりてわれらの皮膚は爐のごとく熱し
11 Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
シオンにて婦人等をかされユダの邑々にて處女等けがさる
12 Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
侯伯たる者も敵の手にて吊され 老たる者の面も尊とばれず
13 Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
少き者は石磨を擔はせられ 童子は薪を負ふてよろめき
14 Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
長老は門にあつまることを止め 少き者はその音樂を廢せり
15 Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
我らが心の快樂はすでに罷み われらの跳舞はかはりて悲哀となり
16 Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
われらの冠冕は首より落たり われら罪ををかしたれば禍なるかな
17 Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
これが爲に我らの心うれへ これらのために我らが目くらくなれり
18 kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
シオンの山は荒はて 山犬はその上を歩くなり
19 Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
ヱホバよなんぢは永遠に在す なんぢの御位は世々かぎりなし
20 Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
何とて我らを永く忘れ われらを斯ひさしく棄おきたまふや
21 Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
ヱホバよねがはくは我らをして汝に歸らしめたまへ われら歸るべし 我らの日を新にして昔日の日のごとくならしめたまへ
22 isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.
さりとも汝まつたく我らを棄たまひしや 痛くわれらを怒りゐたまふや