< Maombolezo 4 >

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
Huru har icke guldet berövats sin glans, den ädla metallen förvandlats! Heliga stenar ligga kringkastade i alla gators hörn.
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Sions ädlaste söner som aktades lika med fint guld, huru räknas de icke nu såsom lerkärl, krukmakarhänders verk!
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
Själva schakalerna räcka spenarna åt sina ungar för att giva dem di; men dottern mitt folk har blivit grym, lik strutsen i öknen.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
Spenabarnets tunga låder av törst vid dess gom; le späda barnen bedja om bröd, men ingen bryter sådant åt dem.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
De som förr åto läckerheter försmäkta nu på gatorna; de som uppföddes i scharlakan måste nu ligga i dyn.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
Så var dottern mitt folks missgärning större än Sodoms synd, Sodoms, som omstörtades i ett ögonblick, utan att människohänder kommo därvid.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
Hennes furstar voro mer glänsande än snö, de voro vitare än mjölk, deras hy var rödare än korall, deras utseende var likt safirens.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
Nu hava deras ansikten blivit mörkare än svart färg, man känner icke igen dem på gatorna; deras hud sitter fastklibbad vid benen, den har förtorkats och blivit såsom trä.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Lyckligare voro de som dräptes med svärd, än de äro, som dräpas av hunger, de som täras bort under kval, utan näring från marken.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
Med egna händer måste ömsinta kvinnor koka sina barn för att hava dem till föda vid dottern mitt folks skada.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
HERREN har uttömt sin förtörnelse, utgjutit sin vredes glöd; i Sion har han tänt upp en eld, som har förtärt dess grundvalar.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
Ingen konung på jorden hade trott det, ingen som bor på jordens krets, att någon ovän eller fiende skulle komma in genom Jerusalems portar.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
För dess profeters synders skull har så skett, för dess prästers missgärningar, därför att de därinne utgöto de rättfärdigas blod.
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
Såsom blinda irra de omkring på gatorna, fläckade av blod. så att ingen finnes, som vågar komma vid deras kläder.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
»Viken undan!» »Oren!», så ropar man framför dem; »Viken undan, viken undan, kommen icke vid den!» ja, flyktiga och ostadiga måste de vara; bland hedningarna säger man om dem: »De skola ej mer finna någon boning.»
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
HERRENS åsyn förskingrar dem, han vill icke mer akta på dem; mot prästerna visas intet undseende, mot de äldste ingen misskund.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
Ännu försmäkta våra ögon i fåfäng väntan efter hjälp; från vårt vårdtorn speja vi efter ett folk som ändå ej kan frälsa oss.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
Han lurar på vara steg, så att vi ej våga gå på våra gator. Vår ände är nära, vara dagar äro ute; ja, vår ande har kommit.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Våra förföljare voro snabbare än himmelens örnar; på bergen jagade de oss, i öknen lade de försåt för oss.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
HERRENS smorde, han som var vår livsfläkt, blev fångad i deras gropar, han under vilkens skugga vi hoppades att få leva bland folken.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Ja, fröjda dig och var glad, du dotter Edom, du som bor i Us' land! Också till dig skall kalken komma; du skall varda drucken och få ligga blottad.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
Din missgärning är ej mer, du dotter Sion; han skall ej åter föra dig bort i fångenskap. Men din missgärning, du dotter Edom, skall han hemsöka; han skall uppenbara dina synder. Alfabetisk sång; se Poesi i Ordförkl.

< Maombolezo 4 >