< Maombolezo 4 >
1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
Kā zeltam spožums zudis un šķīstam zeltam jaukums, svētās vietas akmeņi izkaisīti visos ielu stūros!
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Ciānas dārgie bērni, kas bija līdzīgi šķīstam zeltam, kā tie nu top turēti par māla traukiem, par podnieka rokas darbu!
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
Pat zvēri dod krūti un zīdina savus bērnus; bet manas tautas meita palikusi nežēlīga, tā kā strausi tuksnesī.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
Zidama bērna mēle līp pie zoda no tvīkšanas, bērniņi prasa maizes, bet neviena nav, kas tiem to lauž.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
Kas gardumus ēda, nu pamirst pa ielām; kas purpurā uzaudzināti, tie nu apkampj mēslus.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
Un manas tautas meitas noziegums ir lielāks, nekā Sodomas grēki, kas piepeši tapa apgāzta, nevienam nepieliekot rokas.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
Viņas lielkungi bija spožāki nekā sniegs un baltāki nekā piens, viņu ģīmis bija sārtāks nekā krelles, tie bija skaisti kā safīrs.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
Bet nu viņu ģīmis tumšāks nekā melnums, ka tos nepazīst uz ielām; un viņu āda līp pie viņu kauliem, - tā ir izkaltusi kā malka.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Zobena nokautie ir jo laimīgi nekā bada nokautie, jo šie pamirst kā nodurti, tādēļ ka nav zemes augļu.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
Žēlīgu sievu rokas vārījušas savus bērnus, tie viņām bijuši par barību manas tautas meitas postā.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
Tas Kungs izdarījis Savu bardzību, Viņš izgāzis Savas dusmības karstumu un Ciānā iededzinājis uguni, kas aprijis viņas pamatus.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
To nebija ticējuši zemes ķēniņi, nedz kāds no pasaules iedzīvotājiem, ka pretinieki un ienaidnieki ieies pa Jeruzālemes vārtiem.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
Bet tas noticis viņas praviešu grēku dēļ, viņas priesteru noziegumu dēļ, tie viņas vidū izlējuši taisno asinis.
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
Tie skraidīja šurp un turp kā akli pa ielām, sagānīti asinīm, tā ka nevarēja aizskart viņu drēbes.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
Un tiem sauca: atkāpjaties, jūs nešķīstie, atkāpjaties, atkāpjaties, neaizskariet nekā! Kad tie nu skrēja, maldījās, tad starp pagāniem sacīja: tiem vairs ilgāki nebūs mist.
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
Tā Kunga dusmība tos izkaisījusi, Viņš tos vairs neuzlūkos; tie priesterus nav cienījuši un vecus nav žēlojuši.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
Mūsu acis vēl īgst, skatīdamās pēc mūsu palīga, kas veltīgs, mēs gaidīt gaidām uz tautu, kas nevar izglābt.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
Tie mūsu pēdas dzinuši, ka nevarējām staigāt pa savām ielām; mūsu gals ir tuvu, mūsu dienas ir pagalam, jo mūsu gals atnācis.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Mūsu dzinēji bijuši čaklāki nekā ērgļi apakš debess, tie mūs vajājuši pa kalniem, tuksnesī tie mums likuši valgus.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
Tā Kunga svaidītais, uz ko mūsu dzīvība stāvēja, ir gūstīts viņu bedrē, par ko sacījām: apakš viņa ēnas dzīvosim starp pagāniem.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Priecājies un līksmojies, Edoma meita, Uc zemes iedzīvotāja! Tomēr tas biķeris nāks pie tevis arīdzan, tu piedzersies un tapsi kaunā.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
Tavs noziegums ir deldēts, Ciānas meita, Viņš tevi vairs neliks aizvest. Bet tavu noziegumu, Edoma meita, Viņš piemeklēs, tavus grēkus Viņš atklās.