< Maombolezo 4 >

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
Comment l'or s'est-il terni, l’or pur s'est-il altéré, les pierres sacrées ont-elles été dispersées au coin de toutes les rues? BETH.
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Les plus nobles fils de Sion, estimés au poids de l'or fin, comment ont-ils été comptés pour des vases de terre, ouvrage des mains d'un potier? GHIMEL.
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
Même les chacals présentent les mamelles, et allaitent leurs petits; la fille de mon peuple est devenue cruelle, comme les autruches dans le désert. DALETH.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
La langue du nourrisson s'attache à son palais, à cause de la soif; les petits enfants demandent du pain, et personne ne leur en donne. HÉ.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
Ceux qui se nourrissaient de mets délicats tombent d'inanition dans les rues; ceux qu'on portait sur la pourpre embrassent le fumier. VAV.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
Et l'iniquité de la fille de mon peuple a été plus grande que le péché de Sodome, qui fut renversée en un instant, sans que des mains se levassent contre elle. ZAÏN.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
Ses princes surpassaient la neige en éclat, le lait en blancheur; leur corps était plus vermeil que le corail, leur figure était un saphir. HETH.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
Leur aspect est plus sombre que le noir même; on ne les reconnaît plus dans les rues; leur peau est collée à leurs os, elle est sèche comme du bois. TETH.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Plus heureuses sont les victimes de l'épée que les victimes de la faim, qui s'épuisent lentement, blessées, faute des produits des champs! JOD.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
Des femmes compatissantes ont de leurs mains fait cuire leurs enfants; ils leur ont servi de nourriture, dans le désastre de la fille de mon peuple. CAPH.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
Yahweh a épuisé sa fureur; il a répandu l'ardeur de sa colère, et a allumé dans Sion un feu qui en a dévoré les fondements. LAMED.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
Ils ne croyaient pas, les rois de la terre, ni tous les habitants du monde, que l'adversaire, l'ennemi entrerait dans les portes de Jérusalem. MEM.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
C'est à cause des péchés de ses prophètes, des iniquités de ses prêtres, qui répandaient dans son enceinte le sang des justes. NUN.
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
Ils erraient comme des aveugles dans les rues, souillés de sang, de sorte qu'on ne pouvait toucher leurs vêtements. SAMECH.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
" Ecartez-vous! Un impur! " leur criait-on. "Ecartez-vous! Ecartez-vous! Ne le touchez pas! " Ils erraient, et l'on disait parmi les nations: " Qu'ils ne séjournent point ici! " PHÉ.
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
La face irritée de Yahweh les a dispersés; il ne les regarde plus. L'ennemi n'a eu ni respect pour les prêtres, ni pitié pour les vieillards. AÏN.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
Et nous, nos yeux se consumaient encore à attendre un vain secours; du haut de nos tours, nous regardions vers une nation qui ne peut sauver. TSADÉ.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
Ils épiaient nos pas, nous empêchant de marcher dans nos places. Notre fin approche, nos jours sont accomplis; oui, notre fin est arrivée! QOPH.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Ceux qui nous poursuivaient ont été plus légers que les aigles du ciel; ils nous ont pourchassés sur les montagnes; ils nous ont dressé des embûches dans le désert. RESCH.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
Le souffle de nos narines, l'oint de Yahweh, a été pris dans leurs fosses, lui dont nous disions: " A son ombre nous vivrons parmi les nations. " SIN.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Réjouis-toi et sois dans l'allégresse, fille d'Edom, qui habite au pays de Hus! A toi aussi passera la coupe; tu t'enivreras et tu te mettras à nu. THAV.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
Ton iniquité a pris fin, fille de Sion, il ne t'enverra plus en exil. Il visite ton iniquité, fille d'Edom; il met à découvert tes péchés.

< Maombolezo 4 >