< Maombolezo 4 >

1 Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
Aleph. How is gold maad derk, the beste colour is chaungid? the stonys of the seyntuarie ben scaterid in the heed of alle stretis.
2 Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
Beth. The noble sones of Sion, and clothid with the best gold, hou ben thei arettid in to erthene vessels, in to the werk of the hondis of a pottere?
3 Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
Gimel. But also lamyes maden nakid her tetis, yauen mylk to her whelpis; the douyter of my puple is cruel, as an ostrig in desert.
4 Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
Deleth. The tonge of the soukynge childe cleued to his palat in thirst; litle children axiden breed, and noon was that brak to hem.
5 Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
He. Thei that eeten lustfuli, perischiden in weies; thei that weren nurschid in cradels, biclippiden toordis.
6 Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
Vau. And the wickidnesse of the douyter of my puple is maad more than the synne of men of Sodom, that was distried in a moment, and hondis token not therynne.
7 Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
Zai. Nazareis therof weren whitere than snow, schynyngere than mylk; rodier than elde yuer, fairere than safire.
8 Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
Heth. The face of hem was maad blackere than coolis, and thei weren not knowun in stretis; the skyn cleuyde to her boonys, it driede, and was maad as a tre.
9 Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
Teth. It was betere to men slayn with swerd, than to men slayn with hungur; for these men wexiden rotun, thei weren wastid of the bareynesse of erthe.
10 Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
Joth. The hondis of merciful wymmen sethiden her children; thei weren maad the metis of tho wymmen in the sorewe of the douyter of my puple.
11 Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
Caph. The Lord fillide his strong veniaunce, he schedde out the ire of his indignacioun; and the Lord kyndlide a fier in Sion, and it deuouride the foundementis therof.
12 Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
Lamet. The kyngis of erthe, and alle dwelleris of the world bileueden not, that an aduersarie and enemy schulde entre bi the yatis of Jerusalem.
13 Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
Men. For the synnes of the profetis therof, and for wickidnessis of preestis therof, that schedden out the blood of iust men in the myddis therof.
14 Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
Nun. Blynde men erryden in stretis, thei weren defoulid in blood; and whanne thei miyten not go, thei helden her hemmes.
15 Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”
Samet. Thei crieden to hem, Departe awei, ye defoulide men, departe ye, go ye awei, nyle ye touche; forsothe thei chidden, and weren stirid; thei seiden among hethene men, God schal no more leie to, that he dwelle among hem.
16 Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.
Ayn. The face of the Lord departide hem, he schal no more leie to, that he biholde hem; thei weren not aschamed of the faces of preestis, nether thei hadden merci on eld men.
17 Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.
Phe. The while we stoden yit, oure iyen failiden to oure veyn help; whanne we bihelden ententif to a folc, that myyte not saue vs.
18 Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.
Sade. Oure steppis weren slidir in the weie of oure stretis; oure ende neiyede, oure daies weren fillid, for oure ende cam.
19 Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.
Coph. Oure pursueris weren swiftere than the eglis of heuene; thei pursueden vs on hillis, thei settiden buschementis to vs in desert.
20 Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.
Res. The spirit of oure mouth, Crist the Lord, was takun in oure synnes; to whom we seiden, We schulen lyue in thi schadewe among hethene men.
21 Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.
Syn. Thou douyter of Edom, make ioye, and be glad, that dwellist in the lond of Hus; the cuppe schal come also to thee, thou schalt be maad drunkun, and schalt be maad bare.
22 Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.
Thau. Thou douyter of Sion, thi wickidnesse is fillid; he schal not adde more, that he make thee to passe ouer; thou douyter of Edom, he schal visite thi wickidnesse, he schal vnhile thi synnes.

< Maombolezo 4 >