< Maombolezo 1 >

1 Tazama jinsi mji ulivyoachwa ukiwa, mji ambao zamani ulikuwa umejaa watu! Jinsi ambavyo umekuwa kama mama mjane, ambaye wakati fulani alikuwa maarufu miongoni mwa mataifa! Yule ambaye alikuwa malkia miongoni mwa majimbo sasa amekuwa mtumwa.
Comment est-elle assise solitaire, la cité populeuse! Elle est devenue comme une veuve, celle qui était grande parmi les nations. Celle qui était reine parmi les provinces a été soumise au tribut. BETH.
2 Kwa uchungu, hulia sana usiku, machozi yapo kwenye mashavu yake. Miongoni mwa wapenzi wake wote hakuna yeyote wa kumfariji. Rafiki zake wote wamemsaliti, wamekuwa adui zake.
Elle pleure amèrement durant la nuit, et les larmes couvrent ses joues; pas un ne la console, de tous ses amants; tous ses compagnons l'ont trahie, ils sont devenus ses ennemis. GHIMEL.
3 Baada ya mateso na kufanyishwa kazi kikatili, Yuda amekwenda uhamishoni. Anakaa miongoni mwa mataifa, hapati mahali pa kupumzika. Wote ambao wanamsaka wamemkamata katikati ya dhiki yake.
Juda s'en est allé en exil, misérable et condamné à un rude travail; il habite chez les nations, sans trouver le repos; ses persécuteurs l’ont atteint dans d'étroits défilés. DALETH.
4 Barabara zielekeazo Sayuni zaomboleza, kwa kuwa hakuna yeyote anayekuja kwenye sikukuu zake zilizoamriwa. Malango yake yote yamekuwa ukiwa, makuhani wake wanalia kwa uchungu, wanawali wake wanahuzunika, naye yuko katika uchungu wa maumivu makuu.
Les chemins de Sion sont dans le deuil, parce que nul ne vient plus à ses fêtes; Toutes ses portes sont en ruines, ses prêtres gémissent, ses vierges se désolent, et elle-même est dans l'amertume. HÉ.
5 Adui zake wamekuwa mabwana zake, watesi wake wana raha. Bwana amemletea huzuni kwa sababu ya dhambi zake nyingi. Watoto wake wamekwenda uhamishoni, mateka mbele ya adui.
Ses oppresseurs ont le dessus, ses ennemis prospèrent; car Yahweh l'a affligée, à cause de la multitude de ses offenses; ses petits enfants s'en sont allés captifs, devant l'oppresseur. VAV.
6 Fahari yote imeondoka kutoka kwa Binti Sayuni. Wakuu wake wako kama ayala ambaye hapati malisho, katika udhaifu wamekimbia mbele ya anayewasaka.
Et la fille de Sion a perdu toute sa gloire; ses princes sont comme des cerfs qui ne trouvent pas de pâture, et qui s'en vont sans force devant celui qui les poursuit. ZAÏN.
7 Katika siku za mateso yake na kutangatanga, Yerusalemu hukumbuka hazina zote ambazo zilikuwa zake siku za kale. Wakati watu wake walipoanguka katika mikono ya adui, hapakuwepo na yeyote wa kumsaidia. Watesi wake walimtazama na kumcheka katika maangamizi yake.
Jérusalem se souvient, aux jours de son affliction et de sa vie errante, de tous ses biens précieux qu'elle possédait, dès les jours anciens. Maintenant que son peuple est tombé sous la main de l'oppresseur, et que personne ne vient a son aide, ses ennemis la voient, et ils rient de son chômage. HETH.
8 Yerusalemu ametenda dhambi sana kwa hiyo amekuwa najisi. Wote waliomheshimu wanamdharau, kwa maana wameuona uchi wake. Yeye mwenyewe anapiga kite na kugeukia mbali.
Jérusalem a multiplié ses péchés; c'est pourquoi elle est devenue une chose souillée; tous ceux qui l'honoraient la méprisent, car ils ont vu sa nudité; elle-même pousse des gémissements, et détourne la face. TETH.
9 Uchafu wake umegandamana na nguo zake; hakuwaza juu ya maisha yake ya baadaye. Anguko lake lilikuwa la kushangaza, hapakuwepo na yeyote wa kumfariji. “Tazama, Ee Bwana, teso langu, kwa maana adui ameshinda.”
Sa souillure apparaît sous les pans de sa robe; elle ne songeait pas à sa fin. Et elle est tombée d'une manière étrange, et personne ne la console! " Vois, Yahweh, ma misère, car l'ennemi triomphe! " JOD.
10 Adui ametia mikono juu ya hazina zake zote, aliona mataifa ya kipagani wakiingia mahali patakatifu pake, wale uliowakataza kuingia kwenye kusanyiko lako.
L'oppresseur a étendu la main sur tous ses trésors; car elle a vu les nations entrer dans son sanctuaire, les nations au sujet desquelles tu avais donné cet ordre: " Elles n'entreront pas dans ton assemblée. " CAPH.
11 Watu wake wote wanalia kwa uchungu watafutapo chakula; wanabadilisha hazina zao kwa chakula ili waweze kuendelea kuishi. “Tazama, Ee Bwana, ufikiri, kwa maana nimedharauliwa.”
Tout son peuple gémit, cherchant du pain; ils donnent leurs joyaux pour des aliments, qui leur rendent la vie. " Vois Yahweh et considère l'abjection où je suis tombée! " LAMED.
12 “Je, si kitu kwenu, ninyi nyote mpitao kando? Angalieni kote mwone. Je, kuna maumivu kama maumivu yangu yale yaliyotiwa juu yangu, yale Bwana aliyoyaleta juu yangu katika siku ya hasira yake kali?
" O vous tous, qui passez par le chemin, regardez et voyez s'il y a une douleur pareille à la douleur qui pèse sur moi, moi que Yahweh a frappée, au jour de son ardente colère! MEM.
13 “Kutoka juu alipeleka moto, akaushusha katika mifupa yangu. Aliitandia wavu miguu yangu na akanirudisha nyuma. Akanifanya mkiwa, na mdhaifu mchana kutwa.
" D'en haut il a lancé dans mes os un feu qui les dévore; il a étendu un filet devant mes pieds, il m'a fait reculer; il m'a jeté dans la désolation, je languis tout le jour. NUN.
14 “Dhambi zangu zimefungwa kwenye nira, kwa mikono yake zilifumwa pamoja. Zimefika shingoni mwangu na Bwana ameziondoa nguvu zangu. Amenitia mikononi mwa wale ambao siwezi kushindana nao.
" Le joug de mes iniquités a été lié dans sa main; unies en faisceau, elles pèsent sur mon cou; il a fait chanceler ma force. Le Seigneur m’a livré à des mains auxquelles je ne puis résister. SAMECH.
15 “Bwana amewakataa wapiganaji wa vita wote walio kati yangu, ameagiza jeshi dhidi yangu kuwaponda vijana wangu wa kiume. Katika shinikizo lake la divai Bwana amemkanyaga Bikira Binti Yuda.
" Le Seigneur a enlevé tous les guerriers qui étaient au milieu de moi; il a appelé contre moi une armée, pour écraser mes jeunes hommes; le Seigneur a foulé au pressoir la vierge, fille de Juda. AÏN.
16 “Hii ndiyo sababu ninalia na macho yangu yanafurika machozi. Hakuna yeyote aliye karibu kunifariji, hakuna yeyote wa kuhuisha roho yangu. Watoto wangu ni wakiwa kwa sababu adui ameshinda.”
" C'est pour cela que je pleure, que mon œil, mon œil se fond en larmes; car il n'y a près de moi personne qui me console, qui me rende la vie; mes fils sont dans la désolation, car l'ennemi l'emporte. " PHÉ.
17 Sayuni ananyoosha mikono yake, lakini hakuna yeyote wa kumfariji. Bwana ametoa amri kwa ajili ya Yakobo kwamba majirani zake wawe adui zake; Yerusalemu umekuwa kitu najisi miongoni mwao.
Sion a tendu les mains... Personne qui la console! Yahweh a mandé contre Jacob ses ennemis qui l'enveloppent; Jérusalem est devenue au milieu d'eux comme une chose souillée. TSADÉ.
18 “Bwana ni mwenye haki, hata hivyo niliasi dhidi ya amri yake. Sikilizeni, enyi mataifa yote, tazameni maumivu yangu. Wavulana wangu na wasichana wangu wamekwenda uhamishoni.
" Yahweh est vraiment juste, car j'ai été rebelle à ses ordres. Oh! écoutez tous, peuples, et voyez ma douleur: mes vierges et mes jeunes gens sont allés en exil! QOPH.
19 “Niliita washirika wangu lakini walinisaliti. Makuhani wangu na wazee wangu waliangamia mjini walipokuwa wakitafuta chakula ili waweze kuishi.
J'ai appelé mes amants, ils m'ont trompée; mes prêtres et mes anciens ont péri dans la ville, en cherchant de la nourriture, pour ranimer leur vie. RESCH.
20 “Angalia, Ee Bwana, jinsi nilivyo katika dhiki! Nina maumivu makali ndani yangu, nami ninahangaika moyoni mwangu, kwa kuwa nimekuwa mwasi sana. Huko nje, upanga unaua watu, ndani, kipo kifo tu.
" Regarde, Yahweh, quelle est mon angoisse! Mes entrailles sont émues; mon cœur est bouleversé au dedans de moi, parce que j'ai été bien rebelle. Au dehors l'épée tue mes enfants; au dedans, c'est la mort! SIN.
21 “Watu wamesikia ninavyolia kwa uchungu, lakini hakuna yeyote wa kunifariji. Adui zangu wote wamesikia juu ya dhiki yangu, wanafurahia lile ulilolitenda. Naomba uilete siku uliyoitangaza ili wawe kama mimi.
" On entend mes gémissements; personne qui me console! Tous mes ennemis, en apprenant mon malheur, se réjouissent de ce que tu as agi. Tu feras venir le jour que tu as annoncé, et ils deviendront tels que moi! THAV.
22 “Uovu wao wote na uje mbele zako; uwashughulikie wao kama vile ulivyonishughulikia mimi kwa sababu ya dhambi zangu zote. Kulia kwangu kwa uchungu ni kwingi na moyo wangu umedhoofika.”
" Que toute leur méchanceté soit présente devant toi, pour que tu les traites comme tu m'as traitée moi-même, à cause de toutes mes offenses! Car mes gémissements sont nombreux, et mon cœur est malade! "

< Maombolezo 1 >