< Waamuzi 1 >
1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
Efter Josua död frågade Israels barn Herran, och sade: Ho skall ibland oss föra örliget emot de Cananeer?
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
Herren sade: Juda skall föra det; si, jag hafver gifvit landet i hans hand.
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
Då sade Juda till sin broder Simeon: Drag med mig upp i min lott, och låt oss strida emot de Cananeer, så vill jag åter draga med dig i din lott. Så drog Simeon med honom.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
Då nu Juda drog ditupp, gaf Herren honom de Cananeer och Phereseer i deras händer; och de slogo i Besek tiotusend män.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
Och de funno AdoniBesek i Besek; och stridde emot honom, och slogo de Cananeer och Phereseer.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
Men AdoniBesek flydde, och de jagade efter honom, fingo honom, och höggo af honom tummarna, både af hans händer och fötter.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Då sade AdoniBesek: Sjutio Konungar, med afhuggna tummar af deras händer och fötter, hemtade upp under mitt bord; såsom jag nu gjort hafver, så hafver Gud vedergullit mig. Och de förde honom till Jerusalem, der blef han död.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
Men Juda barn stridde emot Jerusalem, och vunno det, och slogo det med svärdsegg, och brände staden upp.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
Sedan drogo Juda barn neder, till att strida emot de Cananeer, som bodde på bergen, och söderut, och i dalarna.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Och Juda drog emot de Cananeer, som bodde i Hebron; men Hebron het i förtiden KiriathArba; och slog Sesai, och Ahiman, och Thalmai;
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
Och drog dädan emot Debirs inbyggare; men Debir het i förtiden KiriathSepher.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Och Caleb sade: Den som KiriathSepher slår och vinner, honom vill jag gifva mina dotter Achsa till hustru.
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Då vann det Athniel, Kenas son, Calebs yngsta broders; och han gaf honom sina dotter Achsa till hustru.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Och det begaf sig, då hon indrog, vardt henne rådet, att hon skulle bedas en åker af sin fader; och hon gaf sig ifrån åsnanom. Då sade Caleb till henne: Hvad är dig?
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
Hon sade: Gif mig en välsignelse; ty du hafver gifvit mig ett söderland; gif mig ock ett, som vatten hafver. Då gaf han henne ett, som vatten hade ofvan och nedan.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
Och de Keniters barn, Mose svågers, drogo upp utu Palma staden med Juda barn uti Juda öken, som ligger sunnan för den staden Arad; och gingo till, och bodde ibland folket.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
Och Juda drog åstad med hans broder Simeon, och slogo de Cananeer i Zephat, och gåfvo honom tillspillo, och kallade staden Horma.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
Dertill vann Juda Gaza med dess tillhöring, och Askelon med dess tillhöring, och Ekron med dess tillhöring.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
Och Herren var med Juda, så att han intog berget; förty han kunde icke intaga dem som i dalarna bodde, derföre, att de hade jernvagnar.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
Och de gåfvo Caleb Hebron, såsom Mose sagt hade; och han fördref derut de tre Enaks söner.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
Men BenJamins barn fördrefvo icke de Jebuseer, som bodde i Jerusalem; utan de Jebuseer bodde när BenJamins barn i Jerusalem, allt intill denna dag.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
Sammalunda drogo ock Josephs barn upp till BethEl; och Herren var med dem.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
Och Josephs hus bespejade BethEl, det tillförene het Lus.
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
Och hållarena fingo se en man gå utu staden, och sade till honom: Visa oss huru vi skole komma in i staden, så vilje vi göra barmhertighet med dig.
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
Och när han hade vist dem hvar de skulle komma in, slogo de staden med svärdsegg; men den mannen och all hans slägt läto de gå.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
Då drog den samme mannen in uti de Hetheers land, och byggde en stad, och kallade honom Lus. Den heter ännu i dag så.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
Och Manasse fördref icke BethSean med dess döttrar; icke heller Thaanach med dess döttrar, och icke heller de inbyggare i Dor med dess döttrar, ej heller de inbyggare i Jibleam med dess döttrar, ej heller de inbyggare i Megiddo med dess döttrar; och de Cananeer begynte till att bo i de samma landena.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
Men då Israel kom till magt, gjorde han de Cananeer skattpligtiga, och fördref dem icke.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Sammalunda fördref icke heller Ephraim de Cananeer, som bodde i Gaser; utan de Cananeer bodde ibland dem i Gaser.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Sebulon fördref icke heller dem som bodde i Kitron och Nahalol; utan de Cananeer bodde ibland dem, och voro skattpligtige.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Asser fördref icke dem som bodde i Acco; icke heller dem som bodde i Zidon, i Ahlab, i Achsib, i Helbah, i Aphik och i Rehob;
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
Utan de Asseriter bodde ibland de Cananeer, som i landena bodde; ty de fördrefvo dem icke.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Napthali fördref icke dem som bodde i BethSemes, ej heller i BethAnath; utan bodde ibland de Cananeer, som i landena bodde; men de i BethSemes och i BethAnath vordo skattpligtige.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
Men de Amoreer trängde Dans barn in på bergena, och stadde dem icke till, att de kommo neder i dalarna.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
Och de Amoreer begynte bo på de bergena Heres i Ajalon och Saalbim; dock vardt Josephs hus hand dem för svår, så att de vordo skattpligtige.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
Och de Amoreers gränsa var der man uppgår till Akrabbim, och ifrå klippone, och ifrå höjdene.