< Waamuzi 1 >

1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
И бысть по скончании Иисусове, и вопрошаху сынове Израилевы Господа, глаголюще: кто взыдет нам к Хананею воевода, ратовати на них?
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
И рече Господь: Иуда взыдет: се, дах землю в руку его.
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
И рече Иуда к Симеону брату своему: взыди со мною в жребий мой, и ополчимся на Хананеа: и пойду и аз с тобою в жребий твой. И пойде с ним Симеон.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
И взыде Иуда, и предаде Господь Хананеа и Ферезеа в руце их: и избиша их в Везеце до десяти тысящ мужей.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
И обретоша Адонивезека в Везеце, и секошася с ним: и избиша Хананеа и Ферезеа.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
И побеже Адонивезек: и гнаша вслед его, и яша его, и отсекоша краи рук его и краи ног его.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
И рече Адонивезек: седмидесяти царем обсекох краи рук их и краи ног их, и быша собирающе (от крупиц) под трапезою моею: якоже убо сотворих, тако воздаде ми Бог. И приведоша его во Иерусалим, и умре тамо.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
И воеваша сынове Иудины на Иерусалим, и взяша его, и поразиша его острием меча, и град сожгоша огнем.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
И по сих снидоша сынове Иудины воевати на Хананеа живущаго в горней к югу и в равней.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
И пойде Иуда на Хананеа живущаго в Хевроне. И изыде Хеврон со страны: имя же бе Хеврону прежде Кариафарвок-Сефер: и убиша Сесина и Ахимана и Фолмиа, роды Енаковы.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
И взыдоша оттуду к живущым в Давире: имя же Давиру бе прежде Кариафсефер, Град Писмен.
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
И рече Халев: иже аще поразит Град Писмен и возмет его, дам ему Асхань дщерь мою в жену.
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
И взя его Гофониил сын Кенеза брата Халевова юнейший, и даде ему Халев Асхань дщерь свою в жену.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
И бысть внегда отходити ей, и подвиже ю Гофониил просити у отца своего села, и ропташе (седящи) на осляти, и вопияше со осляти: на землю южную отдал мя еси. И рече ей Халев: что ти есть?
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
И рече ему Асхань: даждь ми благословение: яко на землю южную отдал еси мя, да даси мне и исходища водная. И даде ей Халев по сердцу ея исходища вышних и исходища нижних.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
И сынове Иофора Кинеева, ужика Моисеова, взыдоша от града Финическа к сыном Иудиным в пустыню сущую на юг Иуды ко исходу Аредову, и поидоша, и вселишася с людьми.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
И пойде Иуда с Симеоном братом своим, и изби Хананеа живущаго в Сефефе, и потребиша его: и прозваша имя граду Потребление.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
И взя Иуда Газу и предел ея, и Аскалона и предел его, и Аккарон и предел его, и Азот и окрестная его.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
И бяше Господь со Иудою. И взя гору, яко не возмогоша потребити живущих во юдоли, зане Рихав противоста им, и колесницы железныя бяху там.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
И даша Халеву Хеврон, якоже глагола Моисей: и наследствова тамо три грады сынов Енаковых, и изгна оттуду три сыны Енаковы.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
И Иевусеа живущаго во Иерусалиме не изгнаша сынове Вениаминовы, и живяше Иевусей с сынми Вениамини во Иерусалиме даже до сего дне.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
И взыдоша сынове Иосифли и сии в Вефиль: и Господь бяше с ними.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
И ополчишася, и соглядаша (сынове Иосифовы) Вефиль: имя же бе прежде граду Луза.
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
И видеша стрегущии мужа исходящаго из града, и яша его и рекоша ему: покажи нам вход во град, и сотворим с тобою милость.
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
И показа им вход градный: и поразиша град острием меча, мужа же и сродство его отпустиша.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
И отиде муж в землю Хеттиим, и созда тамо град, и прозва имя ему Луза: сие имя ему даже до дне сего.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
И не разори Манассий Вефсана, иже есть Скифский град, ниже дщерей его, ниже окрестных (предел) его, ниже Фанаха, ниже дщерей его, ниже живущих в Доре, ниже дщерей его, ниже живущих во Иевламе, ниже окрестных его, ниже дщерей его, и живущих в Магеддоне, ниже окрестных его и дщерей его. И нача Хананей жити на земли сей.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
И бысть егда укрепися Израиль, и сотвори Хананеа данника: изгнанием же не изгна его.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
И Ефрем не изгна Хананеа живущаго в Газере: и живяше Хананей среде его в Газере, и бысть ему в данника.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
И Завулон не изгна живущих в Хевроне и живущих во Аммане: и вселися Хананей посреде их и бысть ему данник.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
И Асир не изгна живущих во Акхоре, (и бысть ему данник, ) ни живущих в Доре, ни живущих в Сидоне, ни живущих в Далафе и во Ахазиве, и во Елве и во Афеке и в Роове.
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
И вселися Асир посреде Хананеа живущаго на земли (той), зане не возможе изгнати его.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
И Неффалим не изгна живущих в Вефсамисе, ниже живущих в Вефанахе: и вселися Неффалим среде Хананеа живущаго на земли (сей): живущии же в Вефсамисе и в Вефанахе быша ему данницы.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
И утесни Аморрей сыны Дановы в горе, яко не попусти им низходити во юдоль.
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
И нача Аморрей жити в горе Чрепней, идеже медведи и лисицы, в Мирсиноне и в Салавине: и отяготе рука дому Иосифля на Аморреа, и бысть ему данник.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
И предел Аморрейский идумей от восхода Акравиня, от Камене и выше.

< Waamuzi 1 >