< Waamuzi 1 >
1 Baada ya kifo cha Yoshua, Waisraeli wakamuuliza Bwana, “Ni nani atakayetangulia kupanda mbele yetu kwa ajili ya kupigana na Wakanaani?”
Après la mort de Josué, les enfants d'Israël demandèrent à Yahvé: « Qui montera pour nous le premier contre les Cananéens, pour les combattre? »
2 Bwana akajibu, “Yuda ndiye atakayetangulia; nimewapa hiyo nchi mikononi mwao.”
Yahvé dit: « Juda montera. Voici, j'ai livré le pays entre ses mains. »
3 Ndipo watu wa Yuda wakawaambia Wasimeoni ndugu zao, “Pandeni pamoja nasi katika nchi tuliyopewa, ili tupate kupigana na Wakanaani. Sisi pia tutakwenda pamoja nanyi katika sehemu yenu mliyopewa.” Basi Wasimeoni wakaenda pamoja nao.
Juda dit à Siméon, son frère: « Monte avec moi dans mon lot, afin que nous combattions les Cananéens; et moi aussi, je monterai avec toi dans ton lot. » Siméon alla donc avec lui.
4 Yuda aliposhambulia, Bwana akawatia Wakanaani na Waperizi mikononi mwao, nao wakawaua watu 10,000 huko Bezeki.
Juda monta, et Yahvé livra entre leurs mains les Cananéens et les Phéréziens. Ils frappèrent dix mille hommes à Bézek.
5 Huko ndiko walipomkuta huyo Adoni-Bezeki, nao wakapigana naye na kuwafanya Wakanaani na Waperizi wakimbie.
Ils trouvèrent Adoni-Bézek à Bézek, et ils lui livrèrent bataille. Ils battirent les Cananéens et les Phéréziens.
6 Adoni-Bezeki pia alikimbia, nao wakamfuata na kumkamata, wakamkata vidole vyake gumba vya mikono na vya miguu.
Mais Adoni-Bézek s'enfuit. Ils le poursuivirent, l'attrapèrent, et lui coupèrent les pouces et les gros orteils.
7 Ndipo Adoni-Bezeki akasema, “Nimewatendea wafalme sabini kama nilivyotendewa na kuwalisha makombo ya chakula chini ya meza yangu. Sasa Mungu amenilipa haya, kama yale niliyowatendea.” Wakamleta Yerusalemu, naye akafa huko.
Adoni-Bézek dit: « Soixante-dix rois, qui ont eu les pouces et les gros orteils coupés, ont fait les poubelles sous ma table. Ce que j'ai fait, Dieu me l'a fait. » On le conduisit à Jérusalem, où il mourut.
8 Watu wa Yuda wakashambulia pia Yerusalemu na kuiteka. Wakaupiga mji kwa upanga na kuuchoma kwa moto.
Les fils de Juda combattirent contre Jérusalem, la prirent, la frappèrent du tranchant de l'épée et mirent le feu à la ville.
9 Baada ya hayo, watu wa Yuda wakateremka kupigana na Wakanaani walioishi katika nchi ya vilima, yaani, Negebu na nchi chini ya vilima vya magharibi.
Après cela, les fils de Juda descendirent pour combattre les Cananéens qui habitaient dans la montagne, dans le midi et dans la plaine.
10 Yuda wakakabiliana na Wakanaani walioishi Hebroni (ambayo hapo kwanza iliitwa Kiriath-Arba) na kuwashinda Sheshai, Ahimani na Talmai.
Juda marcha contre les Cananéens qui habitaient à Hébron. (Le nom d'Hébron était auparavant Kiriath Arba.) Ils frappèrent Sheshai, Ahiman et Talmai.
11 Kutoka huko wakasonga mbele kukabiliana na watu walioishi Debiri (ambao hapo kwanza uliitwa Kiriath-Seferi.)
De là, il alla contre les habitants de Debir. (Le nom de Debir était auparavant Kiriath Sepher.)
12 Kalebu akasema, “Nitamwoza binti yangu Aksa kwa mtu atakayeweza kupigana na kuteka Kiriath-Seferi.”
Caleb dit: « Je donnerai ma fille Acsa pour femme à l'homme qui frappera Kiriath Sepher et la prendra. »
13 Basi Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa huyo Kalebu, akawashinda, kwa hiyo Kalebu akamtoa binti yake Aksa akaolewa naye.
Othniel, fils de Kenaz, frère cadet de Caleb, la prit, et il lui donna pour femme sa fille Acsa.
14 Siku moja Aksa alipokuja kwa Othnieli, alimsihi Othnieli amwombe baba yake, Kalebu, shamba. Aksa aliposhuka kutoka juu ya punda wake, Kalebu akamuuliza, “Je, wataka nikufanyie nini?”
Quand elle arriva, elle lui demanda de demander un champ à son père. Elle descendit de son âne; et Caleb lui dit: « Que veux-tu? »
15 Akamjibu, “Naomba unifanyie jambo moja la hisani. Kwa kuwa umenipa ardhi huko Negebu, nipe pia chemchemi za maji.” Ndipo Kalebu akampa chemchemi za juu na za chini.
Elle lui dit: « Donne-moi une bénédiction; puisque tu m'as établie dans le pays du Midi, donne-moi aussi des sources d'eau. » Et Caleb lui donna les sources supérieures et les sources inférieures.
16 Wazao wa yule Mkeni, baba mkwe wa Mose, wakapanda pamoja na watu wa Yuda kutoka Mji wa Mitende, wakaenda kuishi miongoni mwa watu wa jangwa ya Yuda huko Negebu karibu na mji wa Aradi.
Les fils du Kénite, beau-frère de Moïse, montèrent de la ville des palmiers avec les fils de Juda dans le désert de Juda, qui est au sud d'Arad, et ils allèrent habiter avec le peuple.
17 Basi watu wa Yuda wakaenda na Wasimeoni ndugu zao kushambulia Wakanaani waishio Sefathi, nao wakauangamiza huo mji kabisa. Kwa hiyo huo mji ukaitwa Horma
Juda partit avec Siméon, son frère, et ils frappèrent les Cananéens qui habitaient Zéphath, et la détruisirent par interdit. Le nom de la ville fut appelé Horma.
18 Watu wa Yuda wakatwaa pia Gaza, Ashkeloni na Ekroni, kila mji na vijiji vyake vinavyouzunguka.
Juda prit aussi Gaza et son territoire, Ashkelon et son territoire, et Ekron et son territoire.
19 Bwana alikuwa pamoja na watu wa Yuda. Wakaimiliki nchi ya vilima, lakini hawakuweza kuwafukuza watu waliokaa katika hiyo tambarare, kwa sababu walikuwa na magari ya chuma.
L'Éternel fut avec Juda, et il chassa les habitants de la montagne, car il ne put chasser les habitants de la vallée, parce qu'ils avaient des chars de fer.
20 Kama vile Mose alivyoahidi, Kalebu alipewa Hebroni, naye akawafukuza wana watatu wa Anaki.
On donna Hébron à Caleb, comme Moïse l'avait dit, et il en chassa les trois fils d'Anak.
21 Hata hivyo, Wabenyamini walishindwa kuwafukuza Wayebusi, waliokuwa wanaishi Yerusalemu; hivyo hadi leo Wayebusi huishi humo pamoja na Wabenyamini.
Les fils de Benjamin ne chassèrent pas les Jébusiens qui habitaient Jérusalem, mais les Jébusiens habitent avec les fils de Benjamin à Jérusalem jusqu'à ce jour.
22 Basi nyumba ya Yosefu wakashambulia Betheli, naye Bwana alikuwa pamoja nao.
La maison de Joseph monta aussi contre Béthel, et l'Éternel fut avec eux.
23 Walipotuma watu kwenda kupeleleza Betheli (ambao hapo kwanza uliitwa Luzu),
La maison de Joseph envoya espionner Béthel.
24 wale wapelelezi wakaona mtu anatoka mjini, nao wakamwambia, “Tuonyeshe jinsi ya kuingia mjini nasi tutakutendea wema.”
Les observateurs virent un homme sortir de la ville et ils lui dirent: « Montre-nous l'entrée de la ville, et nous te traiterons avec bienveillance. »
25 Hivyo akawaonyesha, nao wakaupiga mji kwa upanga lakini wakamhifadhi hai yule mtu na jamaa yake yote.
Il leur montra l'entrée de la ville, et ils frappèrent la ville du tranchant de l'épée; mais ils laissèrent partir l'homme et toute sa famille.
26 Yule mtu akaenda hadi nchi ya Wahiti, ambapo aliujenga mji na kuuita Luzu, ambao ndio jina lake hadi leo.
L'homme alla dans le pays des Hittites, bâtit une ville et l'appela Luz, nom qu'elle porte encore aujourd'hui.
27 Lakini Manase hawakuwafukuza watu wa Beth-Shani na vijiji vyake, au watu wa Taanaki na vijiji vyake, au watu wa Dori na vijiji vyake, au watu wa Ibleamu na vijiji vyake, au watu wa Megido na vijiji vyake, lakini Wakanaani waliazimu kuishi katika nchi ile.
Manassé ne chassa pas les habitants de Beth Shean et de ses villes, ni de Taanach et de ses villes, ni les habitants de Dor et de ses villes, ni les habitants d'Ibleam et de ses villes, ni les habitants de Megiddo et de ses villes; mais les Cananéens demeurèrent dans ce pays.
28 Israeli walipopata nguvu, wakawatia Wakanaani katika kazi ya kulazimishwa, lakini kamwe hawakuwafukuza watoke kabisa.
Lorsqu'Israël fut devenu fort, il mit les Cananéens au travail forcé et ne les chassa pas complètement.
29 Wala Efraimu hawakuwafukuza kabisa Wakanaani walioishi Gezeri, bali Wakanaani waliendelea kuishi humo miongoni mwao.
Ephraïm ne chassa pas les Cananéens qui habitaient à Guézer, mais les Cananéens habitèrent à Guézer au milieu d'eux.
30 Vivyo hivyo Zabuloni hawakuwafukuza Wakanaani walioishi huko Kitroni, wala walioishi Nahaloli, ambao walibaki miongoni mwao; bali waliwatia katika kazi ya kulazimishwa.
Zabulon ne chassa pas les habitants de Kitron ni ceux de Nahalol, mais les Cananéens habitèrent parmi eux et furent soumis au travail forcé.
31 Wala Asheri hawakuwafukuza wale walioishi huko Ako, Sidoni, Alabu, Akzibu, Helba, Afeki wala Rehobu
Asher ne chassa pas les habitants d'Acco, ni ceux de Sidon, ni ceux d'Ahlab, ni ceux d'Achzib, ni ceux d'Helba, ni ceux d'Aphik, ni ceux de Rehob;
32 na kwa sababu ya jambo hili Waasheri wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi.
mais les Asher habitèrent parmi les Cananéens, habitants du pays, car ils ne les chassèrent pas.
33 Wala Naftali hawakuwafukuza wale walioishi Beth-Shemeshi wala wale walioishi Beth-Anathi; lakini Naftali nao pia wakaishi miongoni mwa Wakanaani, wenyeji wa nchi, nao wale walioishi Beth-Shemeshi na Beth-Anathi wakawa watumishi wao katika kazi ya kulazimishwa.
Nephtali ne chassa pas les habitants de Beth Shemesh ni ceux de Beth Anath, mais il habita au milieu des Cananéens, habitants du pays. Néanmoins, les habitants de Beth Shemesh et de Beth Anath furent soumis au travail forcé.
34 Waamori wakawazuilia Wadani kwenye nchi ya vilima, kwa maana hawakuwaacha washuke kuingia kwenye sehemu tambarare.
Les Amorrhéens forcèrent les enfants de Dan à aller dans la montagne, car ils ne leur permirent pas de descendre dans la vallée;
35 Waamori pia wakaendelea kukaa katika Mlima Heresi, katika Aiyaloni na Shaalbimu, lakini mkono wa nyumba ya Yosefu ukawalemea, nao wakashindwa hata wakalazimika kuingia katika kazi ya kulazimishwa.
mais les Amorrhéens habitèrent au mont Hérès, à Aijalon et à Shaalbim. Mais la main de la maison de Joseph l'emporta, de sorte qu'ils furent soumis au travail forcé.
36 Mpaka wa Waamori ulikuwa kuanzia Genge la Akrabimu, kuendelea hadi Sela na kuelekea juu.
La frontière des Amoréens s'étendait depuis la montée d'Akrabbim, depuis le rocher et vers le haut.