< Waamuzi 9 >
1 Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake,
Yerubbaal'ın oğlu Avimelek, dayılarının bulunduğu Şekem Kenti'ne giderek onlara ve annesinin boyundan gelen herkese şöyle dedi:
2 “Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”
“Şekem halkına şunu duyurun: ‘Sizin için hangisi daha iyi? Gidyon'un yetmiş oğlu tarafından yönetilmek mi, yoksa bir kişi tarafından yönetilmek mi?’ Unutmayın ki ben sizinle aynı etten, aynı kandanım.”
3 Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.”
Dayıları Avimelek'in söylediklerini Şekem halkına ilettiler. Halkın yüreği Avimelek'ten yanaydı. “O bizim kardeşimizdir” dediler.
4 Wakampa shekeli sabini za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake.
Ona Baal-Berit Tapınağı'ndan yetmiş parça gümüş verdiler. Avimelek bu parayla kiraladığı belalı serserileri peşine taktı.
5 Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha.
Sonra Ofra'ya, babasının evine dönüp kardeşlerini, Yerubbaal'ın yetmiş oğlunu bir taşın üzerinde kesip öldürdü. Yalnız Yerubbaal'ın küçük oğlu Yotam kaçıp gizlendiği için sağ kaldı.
6 Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.
Şekem ve Beytmillo halkları toplanarak hep birlikte Şekem'de dikili taş meşesinin olduğu yere gittiler; Avimelek'i orada kral ilan ettiler.
7 Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi.
Olup biteni Yotam'a bildirdiklerinde Yotam Gerizim Dağı'nın tepesine çıkıp yüksek sesle halka şöyle dedi: “Ey Şekem halkı, beni dinleyin, Tanrı da sizi dinleyecek.
8 Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’
Bir gün ağaçlar kendilerine bir kral meshetmek istediler; zeytin ağacına gidip, ‘Gel kralımız ol’ dediler.
9 “Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’
“Zeytin ağacı, ‘İlahları ve insanları onurlandırmak için kullanılan yağımı bırakıp ağaçlar üzerinde sallanmaya mı gideyim?’ diye yanıtladı.
10 “Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’
“Bunun üzerine ağaçlar incir ağacına, ‘Gel sen kralımız ol’ dediler.
11 “Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’
“İncir ağacı, ‘Tatlılığımı ve güzel meyvemi bırakıp ağaçlar üzerinde sallanmaya mı gideyim?’ diye yanıtladı.
12 “Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
“Sonra ağaçlar asmaya, ‘Gel sen bizim kralımız ol’ dediler.
13 “Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’
Asma, ‘İlahlarla insanlara zevk veren yeni şarabımı bırakıp ağaçlar üzerinde sallanmaya mı gideyim?’ dedi.
14 “Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
“Sonunda ağaçlar karaçalıya, ‘Gel sen kralımız ol’ dediler.
15 “Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’
“Karaçalı, ‘Eğer gerçekten beni kendinize kral meshetmek istiyorsanız, gelin gölgeme sığının’ diye karşılık verdi, ‘Eğer sığınmazsanız, karaçalıdan çıkan ateş Lübnan'ın bütün sedir ağaçlarını yakıp kül edecektir.’
16 “Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili:
“Şimdi siz Avimelek'i kral yapmakla içten ve dürüst davrandığınızı mı sanıyorsunuz? Yerubbaal'la ailesine iyilik mi ettiniz? Ona hak ettiği gibi mi davrandınız?
17 kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani
Oysa babam sizi Midyanlılar'ın elinden kurtarmak için canını tehlikeye atarak sizin için savaştı.
18 (lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu),
Ama bugün siz babamın ailesine karşı ayaklandınız, yetmiş oğlunu bir taşın üzerinde kesip öldürdünüz. Cariyesinden doğan Avimelek kardeşiniz olduğu için onu Şekem'e kral yaptınız.
19 nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia!
Eğer bugün Yerubbaal'la ailesine içten ve dürüst davrandığınıza inanıyorsanız, Avimelek'le sevinin, o da sizinle sevinsin!
20 Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”
Ama öyle değilse, dilerim, Avimelek ateş olsun, Şekem ve Beytmillo halkını yakıp kül etsin. Ya da Şekem ve Beytmillo halkı ateş olsun, Avimelek'i yakıp kül etsin.”
21 Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.
Ardından Yotam kardeşi Avimelek'ten korktuğu için kaçtı, gidip Beer'e yerleşti.
22 Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu,
Avimelek İsrail'i üç yıl yönetti.
23 Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila.
Sonra Tanrı Avimelek'le Şekem halkını birbirine düşürdü; halk Avimelek'e başkaldırdı.
24 Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake.
Tanrı bunu Avimelek'i Yerubbaal'ın yetmiş oğluna yapılan zorbalığın aynısına uğratmak, kardeşlerini öldüren Avimelek'ten ve onu bu kırıma isteklendiren Şekem halkından akıttıkları kanın öcünü almak için yaptı.
25 Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.
Şekem halkı dağ başlarında Avimelek'e pusu kurdu. Oradan geçen herkesi soyuyorlardı. Bu durum Avimelek'e bildirildi.
26 Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye.
Ebet oğlu Gaal kardeşleriyle birlikte gelip Şekem'e yerleşti. Şekem halkı ona güvendi.
27 Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki.
Bağlara çıkıp üzümleri topladıktan, ezip şarap yaptıktan sonra bir şenlik düzenlediler. İlahlarının tapınağına gittiler; orada yiyip içerken Avimelek'e lanetler yağdırdılar.
28 Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki?
Ebet oğlu Gaal kalkıp şöyle dedi: “Avimelek kim ki, biz Şekem halkı ona hizmet edelim? Yerubbaal'ın oğlu değil mi o? Zevul da onun yardımcısı değil mi? Şekemliler'in babası Hamor'un soyundan gelenlere hizmet edin. Neden Avimelek'e hizmet edelim?
29 Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’”
Keşke bu halkı ben yönetseydim! Avimelek'i uzaklaştırır ve, ‘Ordunu güçlendir de öyle ortaya çık!’ derdim.”
30 Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana.
Kentin yöneticisi olan Zevul, Ebet oğlu Gaal'ın sözlerini duyunca öfkelendi.
31 Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako.
Avimelek'e gizlice gönderdiği ulaklar aracılığıyla şöyle dedi: “Ebet oğlu Gaal ve kardeşleri Şekem'e geldiler. Kenti sana karşı ayaklandırıyorlar.
32 Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani.
Gel, adamlarınla birlikte gece kırda pusuya yat.
33 Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”
Sabah güneş doğar doğmaz kalk, kenti bas. Gaal ile adamları sana saldırdığında onlara yapacağını yap.”
34 Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne.
Böylece Avimelek'le adamları gece kalkıp dört bölük halinde Şekem yakınında pusuya yattılar.
35 Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.
Ebet oğlu Gaal çıkıp kentin giriş kapısında durunca, Avimelek'le yanındakiler pusu yerinden fırladılar.
36 Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!” Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”
Gelenleri gören Gaal, Zevul'a, “Dağların tepesinden inip gelenlere bak!” dedi. Zevul, “Adam sandığın aslında dağların gölgesidir” diye karşılık verdi.
37 Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”
Ama Gaal ısrar etti: “Bak, topraklarımızın ortasında ilerleyenler var. Bir kısmı da Falcılar Meşesi yolundan geliyor.”
38 Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”
Bunun üzerine Zevul, “‘Avimelek kim ki, ona hizmet edelim’ diye övünen sen değil miydin?” dedi, “Küçümsediğin halk bu değil mi? Haydi şimdi git, onlarla savaş!”
39 Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki.
Şekem halkına öncülük eden Gaal, Avimelek'le savaşa tutuştu.
40 Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango.
Ama tutunamayıp kaçmaya başladı. Avimelek ardına düştü. Kentin giriş kapısına dek çok sayıda ölü yerde yatıyordu.
41 Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.
Avimelek Aruma'da kaldı. Zevul ise Gaal'ı ve kardeşlerini Şekem'den kovdu, kentte yaşamalarına izin vermedi.
42 Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili.
Savaşın ertesi günü Avimelek Şekemliler'in tarlalarına gittiklerini haber aldı.
43 Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia.
Adamlarını üç bölüğe ayırıp kırda pusuya yattı. Halkın kentten çıktığını görünce saldırıp onları öldürdü.
44 Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua.
Sonra yanındaki bölükle hızla ilerleyerek kentin giriş kapısına dayandı. Öbür iki bölükse tarlalardakilere saldırıp onları öldürdü.
45 Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.
Avimelek gün boyu kente karşı savaştı; kenti ele geçirdikten sonra halkını kılıçtan geçirdi. Kenti yıkıp üstüne tuz serpti.
46 Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi.
Şekem Kulesi'ndeki halk olup biteni duyunca, El-Berit Tapınağı'nın kalesine sığındı.
47 Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko,
Onların Şekem Kulesi'nde toplandığını haber alan Avimelek,
48 yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!”
yanındaki halkla birlikte Salmon Dağı'na çıktı. Eline bir balta alıp ağaçtan bir dal kesti, dalı omuzuna atarak yanındakilere, “Ne yaptığımı gördünüz” dedi, “Çabuk olun, siz de benim gibi yapın.”
49 Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.
Böylece hepsi birer dal kesip Avimelek'i izledi. Dalları kalenin dibinde yığıp ateşe verdiler. Şekem Kulesi'ndeki bin kadar kadın, erkek yanarak öldü.
50 Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka.
Bundan sonra Avimelek Teves üzerine yürüdü, kenti kuşatıp ele geçirdi.
51 Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara.
Kentin ortasında sağlam bir kule vardı. Kadın erkek bütün kent halkı oraya sığındı. Kapıları kapayıp kulenin damına çıktılar.
52 Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto,
Avimelek gelip kuleyi kuşattı. Ateşe vermek için kapısına yaklaştığında,
53 mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.
bir kadın değirmenin üst taşını Avimelek'in üzerine atıp başını yardı.
54 Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa.
Avimelek hemen silahlarını taşıyan uşağını çağırdı ve, “Kılıcını çek, beni öldür” dedi, “Hiç kimse, ‘Avimelek'i bir kadın öldürdü’ demesin.” Uşak kılıcını Avimelek'e saplayıp onu öldürdü.
55 Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.
Avimelek'in öldüğünü görünce İsrailliler evlerine döndüler.
56 Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini.
Böylece Tanrı yetmiş kardeşini öldürerek babasına büyük kötülük eden Avimelek'i cezalandırdı.
57 Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.
Tanrı Şekem halkını da yaptıkları kötülüklerden ötürü cezalandırdı. Yerubbaal'ın oğlu Yotam'ın lanetine uğradılar.