< Waamuzi 9 >
1 Siku moja Abimeleki mwana wa Yerub-Baali akaenda kwa ndugu ya mama yake huko Shekemu na kuwaambia yeye na ukoo wote wa mama yake,
Now Abimelech, the son of Jerubbaal, went to Shechem to his mother's family, and said to them and to all the family of his mother's father,
2 “Waulizeni watu wote wa Shekemu, ‘Lipi lililo bora kwenu: Kutawaliwa na wana wote sabini wa Yerub-Baali, au mtu mmoja peke yake?’ Kumbukeni kwamba, mimi ni mfupa wenu nyama yenu hasa.”
Say now in the ears of all the townsmen of Shechem, Is it better for you to be ruled by all the seventy sons of Jerubbaal or by one man only? And keep in mind that I am your bone and your flesh.
3 Ndugu za mama yake walipowaeleza watu wote wa Shekemu, wakaelekea kumkubali Abimeleki, kwa kuwa walisema, “Yeye ni ndugu yetu.”
So his mother's family said all this about him in the ears of all the townsmen of Shechem: and their hearts were turned to Abimelech, for they said, He is our brother.
4 Wakampa shekeli sabini za fedha kutoka hekalu la Baal-Berithi, naye Abimeleki akaitumia kuajiri watu ovyo wasiojali, wakawa ndio wafuasi wake.
And they gave him seventy shekels of silver from the house of Baal-berith, with which Abimelech got the support of a number of uncontrolled and good-for-nothing persons.
5 Akaenda nyumbani kwa baba yake huko Ofra, na juu ya jiwe moja wakawaua ndugu zake sabini, ambao ni wana wa Yerub-Baali. Lakini Yothamu, mwana mdogo wa wote wa Yerub-Baali, akaokoka kwa kujificha.
Then he went to his father's house at Ophrah, and put his brothers, the seventy sons of Jerubbaal, to death on the same stone; however, Jotham, the youngest, kept himself safe by going away to a secret place.
6 Ndipo watu wote wa Shekemu na Beth-Milo wakakusanyika pamoja chini ya mti mkubwa wa mwaloni penye nguzo iliyoko Shekemu wakamvika Abimeleki taji kuwa mfalme.
And all the townsmen of Shechem and all Beth-millo came together and went and made Abimelech their king, by the oak of the pillar in Shechem.
7 Yothamu alipoambiwa hayo, akapanda juu ya kilele cha mlima Gerizimu, akawapazia sauti yake akawaambia, “Nisikilizeni enyi watu wa Shekemu, ili Mungu naye apate kuwasikiliza ninyi.
Now Jotham, on hearing of it, went to the top of Mount Gerizim, and crying out with a loud voice said to them, Give ear to me, you townsmen of Shechem, so that God may give ear to you.
8 Siku moja miti ilitoka ili kwenda kujitawazia mfalme. Ikauambia mzeituni, ‘Wewe uwe mfalme wetu.’
One day the trees went out to make a king for themselves; and they said to the olive-tree, Be king over us.
9 “Lakini mzeituni ukaijibu, ‘Je, niache kutoa mafuta yangu ambayo kwake miungu na wanadamu huheshimiwa, ili nikawe juu ya miti?’
But the olive-tree said to them, Am I to give up my wealth of oil, by which men give honour to God, and go waving over the trees?
10 “Kisha miti ikauambia mtini, ‘Njoo na uwe mfalme wetu!’
Then the trees said to the fig-tree, You come and be king over us.
11 “Lakini mtini ukaijibu, ‘Je, niache kutoa matunda yangu mazuri na matamu, ili niende nikawe juu ya miti?’
But the fig-tree said to them, Am I to give up my sweet taste and my good fruit and go waving over the trees?
12 “Ndipo miti ikauambia mzabibu, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
Then the trees said to the vine, You come and be king over us.
13 “Lakini mzabibu ukaijibu, ‘Je, niache kutoa divai yangu inayofurahisha miungu na wanadamu ili nikawe juu ya miti?’
But the vine said to them, Am I to give up my wine, which makes glad God and men, to go waving over the trees?
14 “Mwishoni miti yote ikauambia mti wa miiba, ‘Njoo na uwe mfalme wetu.’
Then all the trees said to the thorn, You come and be king over us.
15 “Nao mti wa miiba ukaijibu, ‘Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu, basi njooni mpate kupumzika chini ya kivuli changu. Lakini kama sivyo, moto na utoke kwenye mti wa miiba ukateketeze mierezi ya Lebanoni!’
And the thorn said to the trees, If it is truly your desire to make me your king, then come and put your faith in my shade; and if not, may fire come out of the thorn, burning up the cedars of Lebanon.
16 “Basi ikiwa mmetenda kwa uaminifu na heshima kumfanya Abimeleki kuwa mfalme, na kama mmetendea vyema Yerub-Baali na jamaa yake kama ilivyostahili:
So now, if you have done truly and uprightly in making Abimelech king, and if you have done well to Jerubbaal and his house in reward for the work of his hands;
17 kwa kuwa baba yangu aliwapigania ninyi na kuhatarisha nafsi yake na kuwaokoa ninyi kutoka mikononi mwa Wamidiani
(For my father made war for you, and put his life in danger, and made you free from the hands of Midian;
18 (lakini leo mmeasi dhidi ya jamaa ya baba yangu, na kuwaua wanawe sabini juu ya jiwe moja, nanyi mkamfanya Abimeleki mwana wa mwanamke mtumwa kuwa mfalme juu ya Shekemu, kwa kuwa yeye ni ndugu yenu),
And you have gone against my father's family this day, and have put to death his sons, even seventy men on one stone, and have made Abimelech, the son of his servant-wife, king over the townsmen of Shechem because he is your brother; )
19 nanyi kama basi mmemtendea Yerub-Baali na jamaa yake kwa heshima na uaminifu, basi Abimeleki na awe furaha yenu, nanyi mwe furaha yake pia!
If then you have done what is true and upright to Jerubbaal and his family this day, may you have joy in Abimelech, and may he have joy in you;
20 Lakini kama sivyo, moto na utoke kwa Abimeleki na uwateketeze, ninyi watu wa Shekemu na Beth-Milo, nao moto utoke kwenu, watu wa Shekemu na Beth-Milo umteketeze Abimeleki!”
But if not, may fire come out from Abimelech, burning up the townsmen of Shechem and Beth-millo; and may fire come out from the townsmen of Shechem and Beth-millo, for the destruction of Abimelech.
21 Ndipo Yothamu akakimbia, akatoroka akaenda Beeri, akaishi huko, kwa sababu alimwogopa ndugu yake Abimeleki.
Then Jotham straight away went in flight to Beer, and was living there for fear of his brother Abimelech.
22 Baada ya Abimeleki kutawala Israeli kwa muda wa miaka mitatu,
So Abimelech was chief over Israel for three years.
23 Mungu akaruhusu roho mbaya kati ya Abimeleki na watu wa Shekemu, nao watu wa Shekemu wakamtendea Abimeleki kwa hila.
And God sent an evil spirit between Abimelech and the townsmen of Shechem; and the townsmen of Shechem were false to Abimelech;
24 Hili lilitokea ili ule ukatili waliotendewa hao wana sabini wa Yerub-Baali upatilizwe, na damu yao iwe juu ya Abimeleki ndugu yao aliyewaua, na pia iwe juu ya watu wa Shekemu, ambao walimsaidia kuua ndugu zake.
So that punishment for the violent attack made on the seventy sons of Jerubbaal, and for their blood, might come on Abimelech, their brother, who put them to death, and on the townsmen of Shechem who gave him their help in putting his brothers to death.
25 Hivyo, kutokana na uadui juu yake watu wa Shekemu wakaweka watu wa kumvizia katika vilele vya milima. Wakawanyangʼanya watu wote waliopita karibu nao, nayo haya yakaarifiwa kwa Abimeleki.
And the townsmen of Shechem put secret watchers on the tops of the mountains, and they made attacks on all who went by on the road and took their goods; and word of this came to Abimelech.
26 Basi Gaali mwana wa Ebedi akaenda pamoja na ndugu zake wakaingia Shekemu, nao watu wa huko wakamtumainia yeye.
Then Gaal, the son of Ebed, came with his brothers, and went over to Shechem; and the men of Shechem put their faith in him.
27 Wakaenda mashambani mwao kuvuna zabibu na kuzisindika hizo zabibu, wakafanya sikukuu katika hekalu la mungu wao. Wakati wakila na kunywa, wakamlaani Abimeleki.
And they went out into their fields and got in the fruit of their vines, and when the grapes had been crushed, they made a holy feast and went into the house of their god, and over their food and drink they were cursing Abimelech.
28 Gaali mwana wa Ebedi akasema, “Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie? Je, yeye si mwana wa Yerub-Baali? Naye Zebuli si ndiye msaidizi wake? Basi watumikieni watu wa Hamori, babaye Shekemu. Kwa nini tumtumikie Abimeleki?
And Gaal, the son of Ebed, said, Who is Abimelech and who is Shechem, that we are to be his servants? Is it not right for the son of Jerubbaal and Zebul his captain to be servants to the men of Hamor, the father of Shechem? But why are we to be his servants?
29 Laiti watu hawa wangekuwa chini ya amri yangu! Basi mimi ningemwondoa huyo Abimeleki. Ningemwambia Abimeleki, ‘Ondoa jeshi lako lote.’”
If only I had authority over this people! I would put Abimelech out of the way, and I would say to Abimelech, Make your army strong, and come out.
30 Zebuli aliyekuwa mtawala wa mji aliposikia aliyosema Gaali mwana wa Ebedi, akakasirika sana.
Now Zebul, the ruler of the town, hearing what Gaal, the son of Ebed, had said, was moved to wrath.
31 Akatuma ujumbe uende kwa Abimeleki kwa siri na kusema, “Gaali mwana wa Ebedi na ndugu zake wamekuja Shekemu, na wanauchochea mji huu kinyume chako.
And he sent to Abimelech at Arumah, saying, See, Gaal, the son of Ebed, and his brothers have come to Shechem, and they are working up the town against you.
32 Sasa, basi, usiku huu wewe uondoke na watu wako ili mje kuwavizia mashambani.
So now, get up by night, you and your people, and keep watch in the field secretly;
33 Kisha asubuhi wakati wa kuchomoza jua, amka mapema na ujipange dhidi ya huo mji. Wakati yeye na jeshi lililo pamoja naye watakapotoka kukabiliana nanyi, mwaweza kuwatendea kwa kadiri mnavyoweza.”
And in the morning, when the sun is up, get up early and make a rush on the town; and when he and his people come out against you, do to them whatever you have a chance to do.
34 Kwa hiyo Abimeleki pamoja na jeshi lake lote wakaondoka usiku na kujificha karibu na Shekemu wakiwa vikosi vinne.
So Abimelech and the people with him got up by night, in four bands, to make a surprise attack on Shechem.
35 Basi Gaali mwana wa Ebedi alikuwa ametoka nje akawa amesimama katika ingilio la mji wakati ule ule ambao Abimeleki na watu wake walipokuwa wanatoka sehemu zao za maficho.
And Gaal, the son of Ebed, went out, and took his place at the doorway into the town; then Abimelech and his people got up from the place where they had been waiting.
36 Gaali alipowaona, akamwambia Zebuli, “Tazama, watu wanashuka kutoka kwenye vilele vya milima!” Zebuli akajibu, “Wewe unaona vivuli vya milima kana kwamba ni watu.”
And when Gaal saw the people, he said to Zebul, See! people are coming down from the tops of the mountains. And Zebul said to him, You see the shade of the mountains like men.
37 Lakini Gaali akasema tena, “Tazama, watu wanashuka kutoka katikati ya nchi na kikosi kimoja kinakuja kutoka Tabur-Ezeri na kikosi kingine kutoka upande wa Elon-Meonenimu.”
And Gaal said again, See! people are coming down from the middle of the land, and one band is coming by way of the oak-tree of the Seers.
38 Ndipo Zebuli akamwambia, “Kuko wapi kujivuna kwako sasa, wewe uliyesema, ‘Huyo Abimeleki ni nani hata tumtumikie?’ Hawa si wale watu uliowadharau? Toka nje sasa ukapigane nao!”
Then Zebul said to him, Now where is your loud talk when you said, Who is Abimelech that we are to be his servants? Is this not the people whom you were rating so low? Go out now, and make war on them.
39 Basi Gaali akatoka akawaongoza watu wa Shekemu kupigana na Abimeleki.
So Gaal went out at the head of the townsmen of Shechem and made war on Abimelech.
40 Abimeleki akamfukuza, watu wengi wakajeruhiwa katika kukimbia huko, njia nzima hadi kwenye ingilio la lango.
And Abimelech went after him and he went in flight before him; and a great number were falling by the sword all the way up to the town.
41 Abimeleki akakaa Aruma, naye Zebuli akawafukuza Gaali na ndugu zake watoke Shekemu.
Then Abimelech went back to Arumah; and Zebul sent Gaal and his brothers away and would not let them go on living in Shechem.
42 Kesho yake watu wa Shekemu wakatoka wakaenda mashambani, Abimeleki akaambiwa juu ya jambo hili.
Now the day after, the people went out into the fields; and news of it came to Abimelech.
43 Hivyo akawachukua watu wake, akawagawanya katika vikosi vitatu na kuwaweka waviziao huko mashambani. Alipowaona watu wanatoka kwenda nje ya mji, akainuka dhidi yao na kuwashambulia.
And he took his people, separating them into three bands, and was waiting secretly in the field; and when he saw the people coming out of the town, he went up and made an attack on them.
44 Abimeleki pamoja na vile vikosi wakaharakisha kwenda mbele kwenye nafasi, mahali pa ingilio la lango la mji. Vile vikosi viwili vikawawahi wale waliokuwa mashambani na kuwaua.
And Abimelech with his band made a rush, and took up their position at the doorway into the town; and the other two bands made a rush on all those who were in the fields, and overcame them.
45 Siku hiyo nzima Abimeleki akazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji hadi akawa ameuteka na kuwaua watu wa huo mji. Kisha akauangamiza mji na kusambaza chumvi juu yake.
And all that day Abimelech was fighting against the town; and he took it, and put to death the people who were in it, and had the town pulled down and covered with salt.
46 Kwa kusikia jambo hili watu wote katika mnara wa Shekemu, wakaingia kwenye ngome ya hekalu la El-Berithi.
Then all the townsmen of the tower of Shechem, hearing of it, went into the inner room of the house of El-berith.
47 Abimeleki aliposikia kuwa wamekusanyika huko,
And word was given to Abimelech that all the men of the tower of Shechem were there together.
48 yeye na watu wake wote wakakwea kwenye Mlima Salmoni. Abimeleki akachukua shoka, akakata baadhi ya matawi, ambayo aliyachukua mabegani. Akawaagiza wale watu waliokuwa pamoja naye kuwa, “Fanyeni kile mlichoona mimi nikifanya!”
Then Abimelech went up to Mount Zalmon, with all his people; and Abimelech took an axe in his hand and, cutting down branches of trees, took them and put them on his back. And he said to the people who were with him, Be quick and do as you have seen me do.
49 Basi watu wote wakakata matawi na kumfuata Abimeleki. Wakayakusanya hayo matawi juu ya ngome na kuitia moto ili kuwachoma wale watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo watu wote katika mnara wa Shekemu, karibia watu 1,000 waume kwa wake, pia wakafa.
So all the people got branches, every man cutting down a branch, and they went with Abimelech at their head and, massing the branches against the inner room, put fire to the room over them; so all those who were in the tower of Shechem, about a thousand men and women, were burned to death with it.
50 Baadaye Abimeleki akaenda Thebesi na kuuzingira kwa jeshi na kuuteka.
Then Abimelech went to Thebez, and put his army in position against Thebez and took it.
51 Hata hivyo, ndani ya huo mji kulikuwa na mnara imara, ambako watu wote wa mji wanaume na wanawake, watu wote wa mji, walikimbilia ndani yake. Wakajifungia ndani yake na kupanda juu ya paa la mnara.
But in the middle of the town there was a strong tower, to which all the men and women of the town went in flight and, shutting themselves in, went up to the roof of the tower.
52 Abimeleki akaja kwenye ule mnara na kuushambulia, lakini alipokaribia kwenye ingilio la mnara ili kuuchoma kwa moto,
And Abimelech came to the tower and made an attack on it, and got near to the door of the tower for the purpose of firing it.
53 mwanamke mmoja akaangusha sehemu ya juu ya jiwe la kusagia juu ya kichwa cha Abimeleki, likapasua fuvu la kichwa chake.
But a certain woman sent a great stone, such as is used for crushing grain, on to the head of Abimelech, cracking the bone.
54 Akamwita kwa haraka kijana yule aliyechukua silaha zake, na kumwambia, “Chukua upanga wako na uniue, watu wasije wakasema kwamba, ‘Mwanamke amemuua.’” Basi yule kijana akamchoma upanga, naye akafa.
Then quickly crying out to his body-servant, he said to him, Take out your sword and put an end to me straight away, so that men may not say of me, His death was the work of a woman. So the young man put his sword through him, causing his death.
55 Waisraeli walipoona kuwa Abimeleki amekufa, kila mtu akaenda nyumbani kwake.
And when the men of Israel saw that Abimelech was dead, they went away, every man to his place.
56 Hivyo ndivyo Mungu alivyolipiza uovu ule ambao Abimeleki alikuwa ameutenda kwa baba yake kwa kuwaua ndugu zake sabini.
In this way Abimelech was rewarded by God for the evil he had done to his father in putting his seventy brothers to death;
57 Mungu akawapatiliza watu wa Shekemu uovu wao juu ya vichwa vyao, na juu yao ikaja laana ya Yothamu mwana wa Yerub-Baali.
And God sent back on to the heads of the men of Shechem all the evil they had done, and the curse of Jotham, the son of Jerubbaal, came on them.