< Waamuzi 8 >

1 Basi Waefraimu wakamuuliza Gideoni, “Mbona mmetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakawalaumu kwa ukali sana.
Možje iz Efrájima so mu rekli: »Zakaj si nam tako služil, da nas nisi poklical, ko si odhajal, da bi se bojeval z Midjánci?« In ostro so se pričkali z njim.
2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri?
Rekel jim je: »Kaj sem torej storil v primerjavi z vami? Mar ni Efrájimovo paberkovanje boljše kakor Abiézerjeva trgatev?
3 Mungu amewatia Orebu na Zeebu, hao viongozi wa Wamidiani, mikononi mwenu. Je, mimi niliweza kufanya nini kulinganisha na mlichofanya ninyi?” Aliposema hili, hasira yao dhidi yake ikatulia.
Bog je v vaše roke izročil midjánska princa, Oréba in Zeéba. Kaj sem bil jaz zmožen storiti v primerjavi z vami?« Potem ko jim je to rekel, se je njihova jeza zoper njega zmanjšala.
4 Gideoni akiwa pamoja na wale watu 300 waliofuatana naye, wakiwa wamechoka na wenye njaa lakini bado wakiwafuatia, wakafika Yordani na kuuvuka.
Gideón je prišel do Jordana ter ga prečkal, on in tristo mož, ki so bili z njim, slabotni, vendar so jih zasledovali.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali lipatieni jeshi langu mikate, kwa maana wamechoka, nami ningali ninawafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.”
Možem iz Sukóta je rekel: »Dajte, prosim vas, hlebe kruha ljudstvu, ki mi sledi, kajti oslabeli so in jaz zasledujem midjánska kralja Zebaha in Calmunája.«
6 Lakini maafisa wa Sukothi wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?”
Princi iz Sukóta so rekli: » Mar so roke Zebaha in Calmunája sedaj v tvoji roki, da bi tvoji vojski dali kruha?«
7 Gideoni akajibu, “Kwa ajili ya hilo tu, Bwana atakapowatia Zeba na Salmuna mkononi mwangu, nitaichana nyama ya miili yenu kwenye miiba ya nyikani na kwenye michongoma.”
Gideón je rekel: »Torej ko Gospod Zebaha in Calmunája izroči v mojo roko, potem bom vaše meso raztrgal s trnjem iz divjine in z osatom.«
8 Kutoka hapo alikwea mpaka Penieli na kutoa ombi lile lile, lakini nao watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu.
Od tam je odšel gor do Penuéla in jim podobno govoril. Ljudje iz Penuéla so mu odgovorili podobno kot ljudje iz Sukóta.
9 Hivyo akawaambia watu wa Penieli, “Nitakaporudi baada ya kushinda, nitaubomoa mnara huu.”
Govoril je tudi ljudem iz Penuéla, rekoč: »Ko ponovno pridem v miru, bom porušil ta stolp.«
10 Wakati huu Zeba na Salmuna walikuwa Karkori wakiwa na jeshi lenye watu wapatao 15,000 wale wote waliokuwa wamesalia wa mataifa ya mashariki, kwa kuwa watu wapatao 120,000 wenye panga walikuwa wameuawa.
Torej Zebah in Calmunáj sta bila v Karkórju in njune vojske z njima, okoli petnajst tisoč mož, vsi, ki so preostali od vseh vojsk otrok vzhoda, kajti tam je padlo sto dvajset tisoč mož, ki so izdirali meč.
11 Basi Gideoni akakwea kwa njia ya wasafiri mashariki ya Noba na Yogbeha na kulishambulia jeshi ambalo halikushuku lolote.
Gideón je odšel gor po poti tistih, ki so prebivali v šotorih vzhodno od Nobaha in Jogbóhe in udaril vojsko, kajti vojska je bila brezskrbna.
12 Zeba na Salmuna, hao wafalme wawili wa Midiani, wakakimbia lakini yeye Gideoni akawafuata na kuwakamata, akalishinda hilo jeshi lao lote.
Ko sta Zebah in Calmunáj pobegnila, ju je zasledoval in zajel dva midjánska kralja, Zebaha in Calmunája ter porazil vso vojsko.
13 Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kwa kupitia Mwinuko wa Heresi.
Joášev sin Gideón se je vrnil iz bitke, preden je vzšlo sonce.
14 Akamkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali, naye yule kijana akamwandikia majina ya maafisa sabini wa Sukothi, ambao ni viongozi wa mji.
Ujel je mladeniča izmed ljudi iz Sukóta in od njega poizvedel in ta mu je opisal prince iz Sukóta in njihove starešine, celó sedeminsedemdeset mož.
15 Ndipo Gideoni akaja na kuwaambia watu wa Sukothi, “Tazama, hapa wapo Zeba na Salmuna mlionisimanga kwa ajili yao mkisema, ‘Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?’”
Prišel je k možem iz Sukóta in rekel: »Glejte Zebaha in Calmunája, s katerima ste me ošteli, rekoč: ›Mar so roke Zebaha in Calmunája sedaj v tvoji roki, da naj bi dali kruha tvojim možem, ki so izmučeni.‹«
16 Akawachukua hao viongozi wa mji na kuwafundisha watu wa Sukothi somo kwa kuwaadhibu kwa miiba na michongoma ya nyikani.
Zgrabil je mestne starešine in trnje iz divjine in osat ter z njimi učil može iz Sukóta.
17 Pia akaubomoa mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji.
Podrl je stolp v Penuélu in usmrtil može iz mesta.
18 Kisha akawauliza Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliowaua huko Tabori?” Wakajibu, “Ni watu kama wewe, kila mmoja wao akiwa na nafasi ya uana wa mfalme.”
Potem je Zebahu in Calmunáju rekel: »Kakšne vrste možje so bili tisti, ki sta jih usmrtila pri Taboru?« Odgovorila sta: »Takšni so bili, kot si ti. Vsakdo je bil podoben kraljevemu otroku.«
19 Gideoni akajibu, “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu hasa. Hakika kama aishivyo Bwana, kama mngekuwa mmewaacha hai, mimi nisingewaua ninyi.”
Rekel je: » Bili so moji bratje, celó sinovi moje matere. Kakor živi Gospod, če bi jih rešila žive, vaju ne bi ubil.«
20 Akamgeukia Yetheri, mwanawe mzaliwa wa kwanza, akasema, “Waue hawa!” Lakini Yetheri hakuufuta upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa kuwa alikuwa bado kijana mdogo tu.
Svojemu prvorojencu Jeterju je rekel: »Vstani in ju ubij.« Toda mladostnik ni izvlekel svojega meča, kajti bal se je, ker je bil še mladostnik.
21 Zeba na Salmuna wakasema, “Njoo ufanye hivyo wewe mwenyewe. ‘Alivyo mtu, ndivyo zilivyo nguvu zake.’” Hivyo Gideoni akatoka mbele na kuwaua, naye akayaondoa mapambo kwenye shingo za ngamia zao.
Potem sta Zebah in Calmunáj rekla: »Vstani ti in padi na naju, kajti kakršen je mož, takšna je njegova moč.« Gideón je vstal in usmrtil Zebaha in Calmunája in odvzel ornamente, ki so bili na vratovih njunih kamel.
22 Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, wanao na wana wa wana wako, kwa kuwa umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”
Potem so možje iz Izraela rekli Gideónu: »Ti vladaj nad nami, oba, ti in tvoj sin in tudi sin tvojega sina, kajti osvobodil si nas iz roke Midjáncev.«
23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala wanangu hawatatawala juu yenu. Bwana ndiye atakayetawala juu yenu ninyi.”
Gideón jim je rekel: »Jaz ne bom vladal nad vami niti ne bo moj sin vladal nad vami. Gospod bo vladal nad vami.«
24 Naye akasema, “Ninalo ombi moja, kwamba kila mmoja wenu anipatie kipuli kutoka kwenye fungu lake la nyara.” (Ilikuwa desturi ya Waishmaeli kuvaa vipuli vya dhahabu.)
Gideón jim je rekel: »Od vas bi želel prošnjo, da bi mi dal vsak mož uhane od svojega plena.« (Kajti imeli so zlate uhane, ker so bili Izmaelci.)
25 Wakajibu, “Tutafurahi kuvitoa.” Hivyo wakatanda vazi chini na kila mwanaume akatupia juu yake pete kutoka kwenye fungu lake la nyara.
Odgovorili so: »Voljno jih bomo dali.« Razširili so obleko in nanjo je vsak mož vrgel uhane od svojega plena.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilifikia shekeli 1,700, bila kuhesabu mapambo mengine, pete za masikio na mavazi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme wa Midiani, au mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia zao.
Teža zlatih uhanov, ki jih je zahteval, je bila tisoč sedemsto šeklov zlata, poleg ornamentov in obeskov za ušesa in škrlatnega oblačila, ki je bil na midjánskih kraljih in poleg verižic, ki so bile okoli vratov njihovih kamel.
27 Gideoni akatengeneza kisibau kwa kutumia ile dhahabu, ambacho alikiweka katika mji wake, yaani, Ofra. Waisraeli wote wakafanya uasherati kwa kukiabudu huko, nacho kikawa mtego kwa Gideoni na jamaa yake.
Gideón je iz njih naredil efód in ga dal v svoje mesto, v Ofro. Ves Izrael se je odšel tja vlačugat za njim. Ta stvar je postala zanka Gideónu in njegovi hiši.
28 Hivyo Midiani ikashindwa mbele ya Israeli nayo haikuinua kichwa chake tena. Wakati wa siku za uhai wa Gideoni, nchi ikafurahia amani miaka arobaini.
Tako je bil Midján podjarmljen pred Izraelovimi otroki, tako da niso več vzdignili svojih glav. In dežela je bila v Gideónovih dneh v spokojnosti štirideset let.
29 Yerub-Baali mwana wa Yoashi akarudi kwenda kuishi katika nyumba yake.
Joášev sin Jerubáal je odšel in prebival v svoji lastni hiši.
30 Alikuwa na wana sabini wa kwake mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
Gideón je imel sedemdeset sinov, rojenih od njegovega telesa, kajti imel je mnogo žena.
31 Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, ambaye alimwita Abimeleki.
Njegova priležnica, ki je bila v Sihemu, mu je prav tako rodila sina, čigar ime je imenoval Abiméleh.
32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa na umri mzuri wa uzee, na akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake huko Ofra ya Waabiezeri.
Joášev sin Gideón je umrl v dobri visoki starosti in bil pokopan v mavzoleju njegovega očeta Joáša v Ofri Abiézerjevcev.
33 Mara tu alipofariki Gideoni, Waisraeli wakarudia hali ya uovu na kufanya uasherati kwa kuabudu Mabaali. Wakamsimamisha Baal-Berithi kuwa mungu wao na
Takoj, ko je bil Gideón mrtev, se je pripetilo, da so se Izraelovi otroci ponovno obrnili in se šli vlačugat za Báali in si naredili Baal-berita za svojega boga.
34 wala hawakumkumbuka Bwana Mungu wao, aliyewaokoa kutoka mikononi mwa adui zao wote kutoka kila upande.
Izraelovi otroci se niso spominjali Gospoda, svojega Boga, ki jih je osvobodil iz rok vseh njihovih sovražnikov na vsaki strani
35 Pia wakashindwa kuitendea mema jamaa ya Yerub-Baali (yaani Gideoni) kwa ajili ya mambo yote mema aliyokuwa amefanya kwa ajili yao.
niti niso izkazali prijaznosti Jerubáalovi hiši, namreč Gideónu, glede na vso dobroto, ki jo je izkazal Izraelu.

< Waamuzi 8 >