< Waamuzi 8 >

1 Basi Waefraimu wakamuuliza Gideoni, “Mbona mmetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakawalaumu kwa ukali sana.
Les hommes d'Éphraïm lui dirent: « Pourquoi nous as-tu traités de la sorte, en ne nous appelant pas quand tu es allé combattre Madian? » Ils le réprimandèrent vivement.
2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri?
Il leur répondit: « Qu'ai-je fait de plus que vous? La vendange d'Ephraïm ne vaut-elle pas mieux que celle d'Abiézer?
3 Mungu amewatia Orebu na Zeebu, hao viongozi wa Wamidiani, mikononi mwenu. Je, mimi niliweza kufanya nini kulinganisha na mlichofanya ninyi?” Aliposema hili, hasira yao dhidi yake ikatulia.
Dieu a livré entre vos mains les princes de Madian, Oreb et Zeeb! Qu'ai-je pu faire en comparaison de toi? » Leur colère s'apaisa à son égard après qu'il eut dit cela.
4 Gideoni akiwa pamoja na wale watu 300 waliofuatana naye, wakiwa wamechoka na wenye njaa lakini bado wakiwafuatia, wakafika Yordani na kuuvuka.
Gédéon arriva au Jourdain et le traversa, lui et les trois cents hommes qui étaient avec lui, faibles mais poursuivant.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali lipatieni jeshi langu mikate, kwa maana wamechoka, nami ningali ninawafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.”
Il dit aux hommes de Succoth: « Donnez, je vous prie, des pains aux gens qui me suivent, car ils sont épuisés, et je poursuis Zébah et Tsalmunna, les rois de Madian. »
6 Lakini maafisa wa Sukothi wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?”
Les princes de Succoth dirent: « Les mains de Zébah et de Tsalmunna sont-elles maintenant entre tes mains, pour que nous donnions du pain à ton armée? »
7 Gideoni akajibu, “Kwa ajili ya hilo tu, Bwana atakapowatia Zeba na Salmuna mkononi mwangu, nitaichana nyama ya miili yenu kwenye miiba ya nyikani na kwenye michongoma.”
Gédéon dit: « C'est pourquoi, lorsque Yahvé aura livré entre mes mains Zébah et Tsalmunna, je déchirerai votre chair avec les épines du désert et avec les ronces. »
8 Kutoka hapo alikwea mpaka Penieli na kutoa ombi lile lile, lakini nao watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu.
Il monta ensuite à Penuel, et leur parla de la même manière. Les hommes de Penuel lui répondirent comme les hommes de Succoth avaient répondu.
9 Hivyo akawaambia watu wa Penieli, “Nitakaporudi baada ya kushinda, nitaubomoa mnara huu.”
Il parla aussi aux hommes de Penuel, en disant: « Quand je reviendrai en paix, je démolirai cette tour. »
10 Wakati huu Zeba na Salmuna walikuwa Karkori wakiwa na jeshi lenye watu wapatao 15,000 wale wote waliokuwa wamesalia wa mataifa ya mashariki, kwa kuwa watu wapatao 120,000 wenye panga walikuwa wameuawa.
Or Zébah et Tsalmunna étaient à Karkor, et leurs armées avec eux, environ quinze mille hommes, tous ceux qui restaient de toute l'armée des fils de l'Orient; car il tomba cent vingt mille hommes qui tirèrent l'épée.
11 Basi Gideoni akakwea kwa njia ya wasafiri mashariki ya Noba na Yogbeha na kulishambulia jeshi ambalo halikushuku lolote.
Gédéon monta par le chemin de ceux qui habitaient dans des tentes à l'est de Nobah et de Jogbehah, et il frappa l'armée; car l'armée se sentait en sécurité.
12 Zeba na Salmuna, hao wafalme wawili wa Midiani, wakakimbia lakini yeye Gideoni akawafuata na kuwakamata, akalishinda hilo jeshi lao lote.
Zébah et Tsalmunna s'enfuirent et il les poursuivit. Il prit les deux rois de Madian, Zébah et Tsalmunna, et confondit toute l'armée.
13 Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kwa kupitia Mwinuko wa Heresi.
Gédéon, fils de Joas, revint de la bataille par la montée de Hérès.
14 Akamkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali, naye yule kijana akamwandikia majina ya maafisa sabini wa Sukothi, ambao ni viongozi wa mji.
Il prit un jeune homme parmi les hommes de Succoth, et le consulta; il lui décrivit les chefs de Succoth et ses anciens, soit soixante-dix-sept hommes.
15 Ndipo Gideoni akaja na kuwaambia watu wa Sukothi, “Tazama, hapa wapo Zeba na Salmuna mlionisimanga kwa ajili yao mkisema, ‘Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?’”
Il s'approcha des hommes de Succoth et dit: « Voyez Zébah et Tsalmunna, au sujet desquels vous m'avez raillé en disant: « Les mains de Zébah et de Tsalmunna sont-elles maintenant entre vos mains, pour que nous donnions du pain à vos hommes qui sont fatigués? ».
16 Akawachukua hao viongozi wa mji na kuwafundisha watu wa Sukothi somo kwa kuwaadhibu kwa miiba na michongoma ya nyikani.
Il prit les anciens de la ville, des épines du désert et des ronces, et avec eux il enseigna aux hommes de Succoth.
17 Pia akaubomoa mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji.
Il démolit la tour de Penuel, et il tua les hommes de la ville.
18 Kisha akawauliza Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliowaua huko Tabori?” Wakajibu, “Ni watu kama wewe, kila mmoja wao akiwa na nafasi ya uana wa mfalme.”
Puis il dit à Zébah et à Tsalmunna: « Quelle sorte d'hommes étaient ceux que vous avez tués au Thabor? » Ils répondirent: « Ils étaient comme vous. Ils ressemblaient tous aux enfants d'un roi. »
19 Gideoni akajibu, “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu hasa. Hakika kama aishivyo Bwana, kama mngekuwa mmewaacha hai, mimi nisingewaua ninyi.”
Il répondit: « Ce sont mes frères, les fils de ma mère. L'Éternel est vivant, si tu les avais sauvés vivants, je ne te tuerais pas. »
20 Akamgeukia Yetheri, mwanawe mzaliwa wa kwanza, akasema, “Waue hawa!” Lakini Yetheri hakuufuta upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa kuwa alikuwa bado kijana mdogo tu.
Il dit à Jether, son aîné: « Lève-toi et tue-les! » Mais le jeune homme ne tira pas son épée, car il avait peur, car il était encore jeune.
21 Zeba na Salmuna wakasema, “Njoo ufanye hivyo wewe mwenyewe. ‘Alivyo mtu, ndivyo zilivyo nguvu zake.’” Hivyo Gideoni akatoka mbele na kuwaua, naye akayaondoa mapambo kwenye shingo za ngamia zao.
Alors Zébah et Tsalmunna dirent: « Vous vous levez et vous tombez sur nous; car telle est la force de l'homme, telle est sa force. » Gédéon se leva, tua Zébah et Tsalmunna, et prit les croissants qui étaient au cou de leurs chameaux.
22 Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, wanao na wana wa wana wako, kwa kuwa umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”
Alors les hommes d'Israël dirent à Gédéon: « Domine sur nous, toi, ton fils et le fils de ton fils aussi, car tu nous as sauvés de la main de Madian. »
23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala wanangu hawatatawala juu yenu. Bwana ndiye atakayetawala juu yenu ninyi.”
Gédéon leur dit: « Je ne dominerai pas sur vous, et mon fils ne dominera pas sur vous. C'est Yahvé qui dominera sur vous. »
24 Naye akasema, “Ninalo ombi moja, kwamba kila mmoja wenu anipatie kipuli kutoka kwenye fungu lake la nyara.” (Ilikuwa desturi ya Waishmaeli kuvaa vipuli vya dhahabu.)
Gédéon leur dit: « J'ai une demande à faire: que chacun de vous me donne les boucles d'oreille de son butin. » (Car ils avaient des boucles d'oreilles en or, parce qu'ils étaient Ismaélites).
25 Wakajibu, “Tutafurahi kuvitoa.” Hivyo wakatanda vazi chini na kila mwanaume akatupia juu yake pete kutoka kwenye fungu lake la nyara.
Ils répondirent: « Nous les donnerons volontiers. » Ils étendirent un vêtement, et chacun y jeta les boucles d'oreilles de son butin.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilifikia shekeli 1,700, bila kuhesabu mapambo mengine, pete za masikio na mavazi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme wa Midiani, au mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia zao.
Le poids des boucles d'oreilles en or qu'il demanda était de mille sept cents sicles d'or, sans compter les croissants, les pendentifs, les vêtements de pourpre qui étaient sur les rois de Madian, et sans compter les chaînes qui étaient au cou de leurs chameaux.
27 Gideoni akatengeneza kisibau kwa kutumia ile dhahabu, ambacho alikiweka katika mji wake, yaani, Ofra. Waisraeli wote wakafanya uasherati kwa kukiabudu huko, nacho kikawa mtego kwa Gideoni na jamaa yake.
Gédéon en fit un éphod, et le mit à Ophra, sa ville. Tout Israël s'y prostitua, et ce fut un piège pour Gédéon et pour sa maison.
28 Hivyo Midiani ikashindwa mbele ya Israeli nayo haikuinua kichwa chake tena. Wakati wa siku za uhai wa Gideoni, nchi ikafurahia amani miaka arobaini.
Ainsi Madian fut soumis aux enfants d'Israël, et ils ne levèrent plus la tête. Le pays fut en repos pendant quarante ans aux jours de Gédéon.
29 Yerub-Baali mwana wa Yoashi akarudi kwenda kuishi katika nyumba yake.
Jerubbaal, fils de Joas, s'en alla et s'établit dans sa maison.
30 Alikuwa na wana sabini wa kwake mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
Gédéon eut soixante-dix fils conçus de son corps, car il avait beaucoup de femmes.
31 Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, ambaye alimwita Abimeleki.
Sa concubine qui était à Sichem lui enfanta aussi un fils, et il l'appela Abimélec.
32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa na umri mzuri wa uzee, na akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake huko Ofra ya Waabiezeri.
Gédéon, fils de Joas, mourut dans une bonne vieillesse, et il fut enterré dans le tombeau de Joas, son père, à Ophra, chez les Abiézrites.
33 Mara tu alipofariki Gideoni, Waisraeli wakarudia hali ya uovu na kufanya uasherati kwa kuabudu Mabaali. Wakamsimamisha Baal-Berithi kuwa mungu wao na
Dès que Gédéon fut mort, les enfants d'Israël se retournèrent, se prostituèrent aux Baals et firent de Baal Berith leur dieu.
34 wala hawakumkumbuka Bwana Mungu wao, aliyewaokoa kutoka mikononi mwa adui zao wote kutoka kila upande.
Les enfants d'Israël ne se souvinrent pas de Yahvé, leur Dieu, qui les avait délivrés de la main de tous leurs ennemis de toute part;
35 Pia wakashindwa kuitendea mema jamaa ya Yerub-Baali (yaani Gideoni) kwa ajili ya mambo yote mema aliyokuwa amefanya kwa ajili yao.
et ils ne firent pas preuve de bonté envers la maison de Jerubbaal, c'est-à-dire Gédéon, selon toute la bonté qu'il avait montrée à Israël.

< Waamuzi 8 >