< Waamuzi 8 >

1 Basi Waefraimu wakamuuliza Gideoni, “Mbona mmetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakawalaumu kwa ukali sana.
And they said to him [the] man of Ephraim what? [is] the thing this [which] you have done to us to not to summon us that you went to fight against Midian and they quarreled! with him with force.
2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri?
And he said to them what? have I done now like you ¿ not good [are] [the] gleanings of Ephraim more than [the] grape harvest of Abiezer.
3 Mungu amewatia Orebu na Zeebu, hao viongozi wa Wamidiani, mikononi mwenu. Je, mimi niliweza kufanya nini kulinganisha na mlichofanya ninyi?” Aliposema hili, hasira yao dhidi yake ikatulia.
In hand your he has given God [the] commanders of Midian Oreb and Zeeb and what? have I been able to do like you then it relaxed spirit their from on him when said he the word this.
4 Gideoni akiwa pamoja na wale watu 300 waliofuatana naye, wakiwa wamechoka na wenye njaa lakini bado wakiwafuatia, wakafika Yordani na kuuvuka.
And he came Gideon the Jordan towards [was] passing over he and three hundred the man who [were] with him [were] exhausted and pursuing.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali lipatieni jeshi langu mikate, kwa maana wamechoka, nami ningali ninawafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.”
And he said to [the] people of Succoth give please round loaves of bread to the people which [is] at feet my for [are] exhausted they and I [am] pursuing after Zebah and Zalmunna [the] kings of Midian.
6 Lakini maafisa wa Sukothi wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?”
And he said [the] officials of Succoth ¿ [is] [the] hand of Zebah and Zalmunna now in hand your that we will give to army your bread.
7 Gideoni akajibu, “Kwa ajili ya hilo tu, Bwana atakapowatia Zeba na Salmuna mkononi mwangu, nitaichana nyama ya miili yenu kwenye miiba ya nyikani na kwenye michongoma.”
And he said Gideon therefore when gives Yahweh Zebah and Zalmunna in hand my and I will thresh flesh your with thorns of the wilderness and with briers.
8 Kutoka hapo alikwea mpaka Penieli na kutoa ombi lile lile, lakini nao watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu.
And he went up from there Penuel and he spoke to them like this and they answered him [the] men of Penuel just as they had answered [the] men of Succoth.
9 Hivyo akawaambia watu wa Penieli, “Nitakaporudi baada ya kushinda, nitaubomoa mnara huu.”
And he said also to [the] men of Penuel saying when return I in peace I will tear down the tower this.
10 Wakati huu Zeba na Salmuna walikuwa Karkori wakiwa na jeshi lenye watu wapatao 15,000 wale wote waliokuwa wamesalia wa mataifa ya mashariki, kwa kuwa watu wapatao 120,000 wenye panga walikuwa wameuawa.
And Zebah and Zalmunna [were] in Karkor and armies their [were] with them about fif-teen thousand all those [who] remained of all [the] army of [the] people of [the] east and those [who] fell [were] one hundred and twenty thousand man [who] drew [the] sword.
11 Basi Gideoni akakwea kwa njia ya wasafiri mashariki ya Noba na Yogbeha na kulishambulia jeshi ambalo halikushuku lolote.
And he went up Gideon [the] way of those [who] dwell in tents from [the] east of Nobah and Jogbehah and he attacked the army and the army it was security.
12 Zeba na Salmuna, hao wafalme wawili wa Midiani, wakakimbia lakini yeye Gideoni akawafuata na kuwakamata, akalishinda hilo jeshi lao lote.
And they fled Zebah and Zalmunna and he pursued after them and he captured [the] two - [the] kings of Midian Zebah and Zalmunna and all the army he routed.
13 Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kwa kupitia Mwinuko wa Heresi.
And he returned Gideon [the] son of Joash from the battle from to [the] ascent of Heres.
14 Akamkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali, naye yule kijana akamwandikia majina ya maafisa sabini wa Sukothi, ambao ni viongozi wa mji.
And he captured a young man one of [the] men of Succoth and he enquired of him and he wrote down to him [the] officials of Succoth and elders its seventy and seven man.
15 Ndipo Gideoni akaja na kuwaambia watu wa Sukothi, “Tazama, hapa wapo Zeba na Salmuna mlionisimanga kwa ajili yao mkisema, ‘Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?’”
And he came to [the] men of Succoth and he said here! Zebah and Zalmunna whom you taunted me saying ¿ [is] [the] hand of Zebah and Zalmunna now in hand your that we will give to men your weary bread.
16 Akawachukua hao viongozi wa mji na kuwafundisha watu wa Sukothi somo kwa kuwaadhibu kwa miiba na michongoma ya nyikani.
And he took [the] elders of the city and [the] thorns of the wilderness and the briers and he taught with them [the] men of Succoth.
17 Pia akaubomoa mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji.
And [the] tower of Penuel he tore down and he killed [the] men of the city.
18 Kisha akawauliza Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliowaua huko Tabori?” Wakajibu, “Ni watu kama wewe, kila mmoja wao akiwa na nafasi ya uana wa mfalme.”
And he said to Zebah and to Zalmunna where? [are] the men whom you killed at Tabor (and they said *L(abh)*) like you like them one [was] like [the] appearance of [the] sons of the king.
19 Gideoni akajibu, “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu hasa. Hakika kama aishivyo Bwana, kama mngekuwa mmewaacha hai, mimi nisingewaua ninyi.”
And he said [were] brothers my [the] sons of mother my they [by] [the] life of Yahweh if you had let live them not I killed you.
20 Akamgeukia Yetheri, mwanawe mzaliwa wa kwanza, akasema, “Waue hawa!” Lakini Yetheri hakuufuta upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa kuwa alikuwa bado kijana mdogo tu.
And he said to Jether firstborn his arise kill them and not he drew the young man sword his for he was afraid for still he [was] a young man.
21 Zeba na Salmuna wakasema, “Njoo ufanye hivyo wewe mwenyewe. ‘Alivyo mtu, ndivyo zilivyo nguvu zake.’” Hivyo Gideoni akatoka mbele na kuwaua, naye akayaondoa mapambo kwenye shingo za ngamia zao.
And he said Zebah and Zalmunna arise you and fall on us for [is] like the man strength his and he arose Gideon and he killed Zebah and Zalmunna and he took the ornaments which [were] on [the] necks of camels their.
22 Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, wanao na wana wa wana wako, kwa kuwa umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”
And they said [the] man of Israel to Gideon rule over us both you as well as son your as well as [the] son of son your for you have delivered us from [the] hand of Midian.
23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala wanangu hawatatawala juu yenu. Bwana ndiye atakayetawala juu yenu ninyi.”
And he said to them Gideon not I will rule I over you and not he will rule son my over you Yahweh he will rule over you.
24 Naye akasema, “Ninalo ombi moja, kwamba kila mmoja wenu anipatie kipuli kutoka kwenye fungu lake la nyara.” (Ilikuwa desturi ya Waishmaeli kuvaa vipuli vya dhahabu.)
And he said to them Gideon let me ask from you a petition and give to me everyone earring of plunder his for earrings of gold [belonged] to them for [were] Ishmaelites they.
25 Wakajibu, “Tutafurahi kuvitoa.” Hivyo wakatanda vazi chini na kila mwanaume akatupia juu yake pete kutoka kwenye fungu lake la nyara.
And they said certainly we will give [them] and they spread out the garment and they threw there towards everyone earring of plunder his.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilifikia shekeli 1,700, bila kuhesabu mapambo mengine, pete za masikio na mavazi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme wa Midiani, au mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia zao.
And it was [the] weight of [the] earrings of gold which he asked for one thousand and seven hundred gold apart from the ornaments and the pendants and [the] garments of purple that [were] on [the] kings of Midian and apart from the necklaces which [were] on [the] necks of camels their.
27 Gideoni akatengeneza kisibau kwa kutumia ile dhahabu, ambacho alikiweka katika mji wake, yaani, Ofra. Waisraeli wote wakafanya uasherati kwa kukiabudu huko, nacho kikawa mtego kwa Gideoni na jamaa yake.
And he made it Gideon into an ephod and he placed it in city his in Ophrah and they acted as prostitutes all Israel after it there and it became for Gideon and for household his a snare.
28 Hivyo Midiani ikashindwa mbele ya Israeli nayo haikuinua kichwa chake tena. Wakati wa siku za uhai wa Gideoni, nchi ikafurahia amani miaka arobaini.
And it was subdued Midian before [the] people of Israel and not they repeated to lift up head their and it was at peace the land forty year[s] in [the] days of Gideon.
29 Yerub-Baali mwana wa Yoashi akarudi kwenda kuishi katika nyumba yake.
And he went Jerub-Baal [the] son of Joash and he dwelt in own house his.
30 Alikuwa na wana sabini wa kwake mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And to Gideon they belonged seventy sons [who] came out of thigh his for wives many they belonged to him.
31 Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, ambaye alimwita Abimeleki.
And concubine his who [was] in Shechem she bore to him also she a son and he made name his Abimelech.
32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa na umri mzuri wa uzee, na akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake huko Ofra ya Waabiezeri.
And he died Gideon [the] son of Joash in old age good and he was buried in [the] tomb of Joash father his in Ophrah of [the] Abi-ezrite[s].
33 Mara tu alipofariki Gideoni, Waisraeli wakarudia hali ya uovu na kufanya uasherati kwa kuabudu Mabaali. Wakamsimamisha Baal-Berithi kuwa mungu wao na
And it was just when he had died Gideon and they turned back [the] people of Israel and they acted as prostitutes after the Baals and they made for themselves Baal-Berith into god.
34 wala hawakumkumbuka Bwana Mungu wao, aliyewaokoa kutoka mikononi mwa adui zao wote kutoka kila upande.
And not they remembered [the] people of Israel Yahweh God their who delivered them from [the] hand of all enemies their from round about.
35 Pia wakashindwa kuitendea mema jamaa ya Yerub-Baali (yaani Gideoni) kwa ajili ya mambo yote mema aliyokuwa amefanya kwa ajili yao.
And not they did loyalty with [the] house of Jerub-Baal Gideon according to all the good which he had done with Israel.

< Waamuzi 8 >