< Waamuzi 8 >

1 Basi Waefraimu wakamuuliza Gideoni, “Mbona mmetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipokwenda kupigana na Wamidiani?” Wakawalaumu kwa ukali sana.
And the men of Ephraim said to him, Why have thou done thus to us, that thou did not call us when thou went to fight with Midian? And they chided with him sharply.
2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri?
And he said to them, What have I now done in comparison with you? Is not the gleaning of the grapes of Ephraim better than the vintage of Abiezer?
3 Mungu amewatia Orebu na Zeebu, hao viongozi wa Wamidiani, mikononi mwenu. Je, mimi niliweza kufanya nini kulinganisha na mlichofanya ninyi?” Aliposema hili, hasira yao dhidi yake ikatulia.
God has delivered into your hand the rulers of Midian, Oreb and Zeeb, and what was I able to do in comparison with you? Then their anger was abated toward him when he had said that.
4 Gideoni akiwa pamoja na wale watu 300 waliofuatana naye, wakiwa wamechoka na wenye njaa lakini bado wakiwafuatia, wakafika Yordani na kuuvuka.
And Gideon came to the Jordan, and passed over, he, and the three hundred men who were with him, faint, yet pursuing.
5 Akawaambia watu wa Sukothi, “Tafadhali lipatieni jeshi langu mikate, kwa maana wamechoka, nami ningali ninawafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.”
And he said to the men of Succoth, Give, I pray you, loaves of bread to the people who follow me, for they are faint, and I am pursuing after Zebah and Zalmunna, the kings of Midian.
6 Lakini maafisa wa Sukothi wakasema, “Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?”
And the rulers of Succoth said, Are the hands of Zebah and Zalmunna now in thy hand that we should give bread to thine army?
7 Gideoni akajibu, “Kwa ajili ya hilo tu, Bwana atakapowatia Zeba na Salmuna mkononi mwangu, nitaichana nyama ya miili yenu kwenye miiba ya nyikani na kwenye michongoma.”
And Gideon said, Therefore when Jehovah has delivered Zebah and Zalmunna into my hand, then I will tear your flesh with the thorns of the wilderness and with briers.
8 Kutoka hapo alikwea mpaka Penieli na kutoa ombi lile lile, lakini nao watu wa Penieli wakamjibu kama watu wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu.
And he went up from there to Penuel, and spoke to them in like manner, and the men of Penuel answered him as the men of Succoth had answered.
9 Hivyo akawaambia watu wa Penieli, “Nitakaporudi baada ya kushinda, nitaubomoa mnara huu.”
And he spoke also to the men of Penuel, saying, When I come again in peace, I will break down this tower.
10 Wakati huu Zeba na Salmuna walikuwa Karkori wakiwa na jeshi lenye watu wapatao 15,000 wale wote waliokuwa wamesalia wa mataifa ya mashariki, kwa kuwa watu wapatao 120,000 wenye panga walikuwa wameuawa.
Now Zebah and Zalmunna were in Karkor, and their armies with them, about fifteen thousand men, all who were left of all the army of the sons of the east, for there fell a hundred and twenty thousand men who drew a sword.
11 Basi Gideoni akakwea kwa njia ya wasafiri mashariki ya Noba na Yogbeha na kulishambulia jeshi ambalo halikushuku lolote.
And Gideon went up by the way of those who dwelt in tents on the east of Nobah and Jogbehah, and smote the army, for the army was confident.
12 Zeba na Salmuna, hao wafalme wawili wa Midiani, wakakimbia lakini yeye Gideoni akawafuata na kuwakamata, akalishinda hilo jeshi lao lote.
And Zebah and Zalmunna fled, and he pursued after them. And he took the two kings of Midian, Zebah and Zalmunna, and discomfited all the army.
13 Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kwa kupitia Mwinuko wa Heresi.
And Gideon the son of Joash returned from the battle from the ascent of Heres.
14 Akamkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali, naye yule kijana akamwandikia majina ya maafisa sabini wa Sukothi, ambao ni viongozi wa mji.
And he caught a young man of the men of Succoth, and inquired of him. And he described for him the rulers of Succoth, and the elders of it, seventy-seven men.
15 Ndipo Gideoni akaja na kuwaambia watu wa Sukothi, “Tazama, hapa wapo Zeba na Salmuna mlionisimanga kwa ajili yao mkisema, ‘Je, mikono ya Zeba na Salmuna tayari mnayo sasa ili tuweze kulipatia jeshi lako mikate?’”
And he came to the men of Succoth, and said, Behold Zebah and Zalmunna, concerning whom ye taunted me, saying, Are the hands of Zebah and Zalmunna now in thy hand, that we should give bread to thy men who are weary?
16 Akawachukua hao viongozi wa mji na kuwafundisha watu wa Sukothi somo kwa kuwaadhibu kwa miiba na michongoma ya nyikani.
And he took the elders of the city, and thorns of the wilderness and briers, and with them he taught the men of Succoth.
17 Pia akaubomoa mnara wa Penieli na kuwaua watu wa mji.
And he broke down the tower of Penuel, and killed the men of the city.
18 Kisha akawauliza Zeba na Salmuna, “Ni watu wa aina gani mliowaua huko Tabori?” Wakajibu, “Ni watu kama wewe, kila mmoja wao akiwa na nafasi ya uana wa mfalme.”
Then he said to Zebah and Zalmunna, What manner of men were they whom ye killed at Tabor? And they answered, As thou are, so were they. Each one resembled the sons of a king.
19 Gideoni akajibu, “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu hasa. Hakika kama aishivyo Bwana, kama mngekuwa mmewaacha hai, mimi nisingewaua ninyi.”
And he said, They were my brothers, the sons of my mother. As Jehovah lives, if ye had saved them alive, I would not kill you.
20 Akamgeukia Yetheri, mwanawe mzaliwa wa kwanza, akasema, “Waue hawa!” Lakini Yetheri hakuufuta upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa kuwa alikuwa bado kijana mdogo tu.
And he said to Jether his firstborn, Up, and kill them. But the youth did not draw his sword, for he feared because he was yet a youth.
21 Zeba na Salmuna wakasema, “Njoo ufanye hivyo wewe mwenyewe. ‘Alivyo mtu, ndivyo zilivyo nguvu zake.’” Hivyo Gideoni akatoka mbele na kuwaua, naye akayaondoa mapambo kwenye shingo za ngamia zao.
Then Zebah and Zalmunna said, Rise thou, and fall upon us, for as the man is, so is his strength. And Gideon arose, and killed Zebah and Zalmunna, and took the crescents that were on their camels' necks.
22 Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, wanao na wana wa wana wako, kwa kuwa umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”
Then the men of Israel said to Gideon, Rule thou over us, both thou, and thy son, and thy son's son also, for thou have saved us out of the hand of Midian.
23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitatawala juu yenu, wala wanangu hawatatawala juu yenu. Bwana ndiye atakayetawala juu yenu ninyi.”
And Gideon said to them, I will not rule over you, neither shall my son rule over you. Jehovah shall rule over you.
24 Naye akasema, “Ninalo ombi moja, kwamba kila mmoja wenu anipatie kipuli kutoka kwenye fungu lake la nyara.” (Ilikuwa desturi ya Waishmaeli kuvaa vipuli vya dhahabu.)
And Gideon said to them, I would make a request of you, that ye would give me every man the earrings of his spoil. (For they had golden earrings, because they were Ishmaelites.)
25 Wakajibu, “Tutafurahi kuvitoa.” Hivyo wakatanda vazi chini na kila mwanaume akatupia juu yake pete kutoka kwenye fungu lake la nyara.
And they answered, We will willingly give them. And they spread a garment, and cast in it every man the earrings of his spoil.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba zilifikia shekeli 1,700, bila kuhesabu mapambo mengine, pete za masikio na mavazi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme wa Midiani, au mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia zao.
And the weight of the golden earrings that he requested was a thousand and seven hundred shekels of gold, besides the crescents, and the pendants, and the purple raiment that was on the kings of Midian, and besides the chains that were about their camels' necks.
27 Gideoni akatengeneza kisibau kwa kutumia ile dhahabu, ambacho alikiweka katika mji wake, yaani, Ofra. Waisraeli wote wakafanya uasherati kwa kukiabudu huko, nacho kikawa mtego kwa Gideoni na jamaa yake.
And Gideon made an ephod of it, and put it in his city, even in Ophrah. And all Israel played the harlot after it there, and it became a snare to Gideon, and to his house.
28 Hivyo Midiani ikashindwa mbele ya Israeli nayo haikuinua kichwa chake tena. Wakati wa siku za uhai wa Gideoni, nchi ikafurahia amani miaka arobaini.
So Midian was subdued before the sons of Israel, and they lifted up their heads no more. And the land had rest forty years in the days of Gideon.
29 Yerub-Baali mwana wa Yoashi akarudi kwenda kuishi katika nyumba yake.
And Jerubbaal the son of Joash went and dwelt in his own house.
30 Alikuwa na wana sabini wa kwake mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
And Gideon had seventy sons begotten from his body, for he had many wives.
31 Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, ambaye alimwita Abimeleki.
And his concubine who was in Shechem, she also bore him a son, and he called his name Abimelech.
32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa na umri mzuri wa uzee, na akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake huko Ofra ya Waabiezeri.
And Gideon the son of Joash died in a good old age, and was buried in the sepulcher of Joash his father, in Ophrah of the Abiezrites.
33 Mara tu alipofariki Gideoni, Waisraeli wakarudia hali ya uovu na kufanya uasherati kwa kuabudu Mabaali. Wakamsimamisha Baal-Berithi kuwa mungu wao na
And it came to pass, as soon as Gideon was dead, that the sons of Israel turned again, and played the harlot after the Baalim, and made Baal-berith their god.
34 wala hawakumkumbuka Bwana Mungu wao, aliyewaokoa kutoka mikononi mwa adui zao wote kutoka kila upande.
And the sons of Israel did not remember Jehovah their God, who had delivered them out of the hand of all their enemies on every side,
35 Pia wakashindwa kuitendea mema jamaa ya Yerub-Baali (yaani Gideoni) kwa ajili ya mambo yote mema aliyokuwa amefanya kwa ajili yao.
neither did they show kindness to the house of Jerubbaal, who is Gideon, according to all the goodness which he had shown to Israel.

< Waamuzi 8 >