< Waamuzi 7 >

1 Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
Therfor Jerobaal, which also Gedeon, roos bi nyyt, and al the puple with hym, and cam to the welle which is clepid Arad. Sotheli the tentis of Madian weren in the valey, at the north coost of the hiy hil.
2 Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
And the Lord seide to Gedeon, Myche puple is with thee, and Madian schal not be bitakun in to the hondis `ther of, lest Israel haue glorie ayens me, and seie, Y am delyuerid bi my strengthis.
3 kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
Speke thou to the puple, and preche thou, while alle men heren, He that is ferdful `in herte, and dredeful `with outforth, turne ayen. And thei yeden awei fro the hil of Galaad, and two and twenti thousynde of men turniden ayen fro the puple; and oneli ten thousynde dwelliden.
4 Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
And the Lord seide to Gedeon, Yet the puple is myche; lede thou hem to the watris, and there Y schal preue hem, and he go, of whom Y schal seye, that he go; turne he ayen, whom Y schal forbede to go.
5 Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
And whanne the puple hadde go doun to watris, the Lord seide to Gedeon, Thou schalt departe hem bi hem silf, that lapen watris with hond and tunge, as doggis ben wont to lape; sotheli thei, that drynken with knees bowid, schulen be in the tothir part.
6 Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
And so the noumbre of hem, that lapiden watris bi hond castynge to the mouth, was thre hundrid men; forsothe al the tothir multitude drank knelynge.
7 Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
And the Lord seide to Gedeon, In thre hundrid men, that lapiden watris, Y schal delyuere you, and Y schal bitake Madian in thin hond; but al the tothir multitude turne ayen in to her place.
8 Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
And so whanne thei hadden take meetis and trumpis for the noumbre, he comaundide al the tothir multitude to go to her tabernaclis; and he, with thre hundrid men, yaf hym silf to batel. Sothely the tentis of Madian weren bynethe in the valey.
9 Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
In the same nyyt the Lord seyde to hym, Ryse thou, and go doun in to `the castels of Madian, for Y haue bitake hem in thin hond;
10 Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
sotheli if thou dredist to go aloon, Phara, thi child, go doun with thee.
11 nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
And whanne thou schalt here what thei speken, thanne thin hondis schulen be coumfortid, and thou schalt do down sikerere to the tentis of enemyes. Therfor he yede doun, and Phara, his child, in to the part of tentis, where the watchis of armed men weren.
12 Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
Forsothe Madian, and Amalech, and alle the puplis of the eest layen spred in the valey, as the multitude of locustis; sotheli the camelis weren vnnoumbrable, as grauel that liggith in the `brenke of the see.
13 Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
And whanne Gedeon hadde come, a man tolde a dreem to his neiybore, and telde bi this maner that, that he hadde seyn, I siy a dreem, and it semyde to me, that as `o loof of barly bakun vndur the aischis was walewid, and cam doun in to the tentis of Madian; and whanne it hadde come to a tabernacle, it smoot and distriede `that tabernacle, and made euene outirly to the erthe.
14 Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
That man answeride, to whom he spak, This is noon other thing, no but the swerd of Gedeon, `sone of Joas, a man of Israel; for the Lord hath bitake Madian and alle `tentis therof in to the hondis of Gedeon.
15 Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
And whanne Gedeon had herd the dreem, and `the interpretyng therof, he worschypide the Lord, and turnede ayen to the tentis of Israel, and seide, Ryse ye; for the Lord hath bitake in to oure hondis the tentis of Madian.
16 Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
And he departide thre hundrid men in to thre partis, and he yaf trumpis in her hondis, and voyde pottis, and laumpis in the myddis of the pottis.
17 Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
And he seide to hem, Do ye this thing which ye seen me do; Y schal entre in to a part of the tentis, and sue ye that, that Y do.
18 Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
Whanne the trumpe in myn hond schal sowne, sowne ye also `bi the cumpas of tentis, and crye ye togidere, To the Lord and to Gedeon.
19 Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
And Gedeon entride, and thre hundrid men that weren with hym, `in to a part of the tentis, whanne the watchis of mydnyyt bigunnen; and whanne the keperis weren reysid, thei bigunnen to sowne with trumpis, and to bete togidere the pottis among hem silf.
20 Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
And whanne thei sowneden in thre places bi cumpas, and hadden broke the pottis, thei helden laumpis in the left hondis, and sownynge trumpis in the riyt hondis; and thei crieden, The swerd of the Lord and of Gedeon; and stoden alle in her place,
21 Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
`bi the cumpas of the tentis of enemyes. And so alle `the tentis weren troblid; and thei crieden, and yelliden, and fledden;
22 Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
and neuertheles the thre hundrid men contynueden, sownynge with trumpis. And the Lord sente swerd in alle the castels, and thei killiden hem silf bi deeth ech other;
23 Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
and thei fledden `til to Bethsecha, and bi the side, fro Elmonla in to Thebbath. Sotheli men of Israel crieden togidere, of Neptalym, and of Aser, and of alle Manasses, and pursueden Madian; and the Lord yaf victorie to the puple of Israel in that day.
24 Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
And Gedeon sente messangeris in to al the hil of Effraym, and seide, Come ye doun ayens the comyng of Madian, and ocupie ye the watris `til to Bethbera and Jordan. And al Effraym criede, and bifore ocupide the watris and Jordan `til to Bethbera.
25 Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.
And Effraym killide twei men of Madian, Oreb and Zeb; he killide Oreb in the ston of Oreb, forsothe `he killide Zeb in the pressour of Zeb; and `thei pursueden Madian, and baren the heedis of Oreb and of Zeb to Gedeon, ouer the flodis of Jordan.

< Waamuzi 7 >